< Hosea 9 >

1 Usifurahi, Israeli, kwa furaha kama watu wengine. Kwa maana haukuwa mwaminifu, umemuacha Mungu wako. Unapenda kulipa mshahara kwa kahaba kwenye sakafu zote za nafaka.
Rejoice not, O Israel, unto exultation, like the peoples, for thou hast gone astray from thy God, thou hast loved a harlot's hire upon every corn-floor.
2 Lakini sakafu na divai hazitawalisha; divai mpya itampungukia.
The threshing-floor and the wine-press shall not feed them, and the new wine shall fail her.
3 Hawawezi kuendelea kuishi katika nchi ya Bwana; badala yake, Efraimu atarudi Misri, na siku moja watakula chakula kichafu katika Ashuru.
They shall not dwell in the LORD'S land; but Ephraim shall return to Egypt, and they shall eat unclean food in Assyria.
4 Hawatamtolea Bwana sadaka za divai, wala hawatamfurahisha. Dhabihu zao zitakuwa kwao kama chakula cha matanga wote wanaolila watakuwa wamejisikia. Maana chakula chao kitakuwa chao pekee; hautakuingia nyumbani mwa Bwana.
They shall not pour out wine-offerings to the LORD, neither shall they be pleasing unto Him; their sacrifices shall be unto them as the bread of mourners, all that eat thereof shall be polluted; for their bread shall be for their appetite, it shall not come into the house of the LORD.
5 Utafanya nini siku ya sikukuu iliyowekwa rasmi, siku ya sikukuu ya Yahweh?
What will ye do in the day of the appointed season, and in the day of the feast of the LORD?
6 Kwa maana, angalia, wamekimbia uharibifu, Misri itawakusanya, na Nofu itawazika. Maana hazina zao za pesa za fedha zitakuwa nao, na miiba itajaza hema zao.
For, lo, they are gone away from destruction, yet Egypt shall gather them up, Memphis shall bury them; their precious treasures of silver, nettles shall possess them, thorns shall be in their tents.
7 Siku za adhabu zinakuja; siku za kulipiza kisasi zinakuja. Waisraeli wote wajue mambo haya. Nabii ni mpumbavu, na mtu aliyevuviwa ni mwendawazimu, kwa sababu ya uovu wako mkubwa na uadui mkubwa.
The days of visitation are come, the days of recompense are come, Israel shall know it. The prophet is a fool, the man of the spirit is mad! For the multitude of thine iniquity, the enmity is great.
8 Nabii ndiye mlinzi wa Mungu wangu juu ya Efraimu. Lakini mtego wa ndege ni juu ya njia zake zote, na uadui umo katika nyumba ya Mungu wake.
Ephraim is a watchman with my God; as for the prophet, a fowler's snare is in all his ways, and enmity in the house of his God.
9 Wamejiharibu wenyewe kama siku za Gibea. Mungu atawakumbusha uovu wao, naye atawaadhibu dhambi zao.
They have deeply corrupted themselves, as in the days of Gibeah; He will remember their iniquity, He will punish their sins.
10 Bwana asema, “Nilipoikuta Israeli, ilikuwa kama kutafuta zabibu jangwani. Kama matunda ya kwanza ya msimu kwenye mtini, nimewaona baba zenu. Lakini wakaenda Baal Peori, nao wakajitoa kwenye sanamu ya aibu. Walikuwa chukizo kama sanamu waliyoipenda.
I found Israel like grapes in the wilderness, I saw your fathers as the first-ripe in the fig-tree at her first season; but so soon as they came to Baal-peor, they separated themselves unto the shameful thing, and became detestable like that which they loved.
11 Na kwa ajili ya Efraimu, utukufu wao utatoka kama ndege. Hakutakuwa na kuzaa, hakuna mimba, wala achukuaye mimba.
As for Ephraim, their glory shall fly away like a bird; there shall be no birth, and none with child, and no conception.
12 Ingawa wameleta watoto, nitawachukua ili asibaki hata mmoja. Ole wao nikiwaacha!
Yea, though they bring up their children, yet will I bereave them, that there be not a man left; yea, woe also to them when I depart from them!
13 Nimeiona Efraimu, kama vile Tiro, alipandwa katika mlima, lakini Efraimu atatoa watoto wake kwa mtu atakayewaua.
Ephraim, like as I have seen Tyre, is planted in a pleasant place; but Ephraim shall bring forth his children to the slayer.
14 Wape, Bwana-utawapa nini? Wape tumbo lenye kuharibu mimba na matiti ambayo haitoi maziwa.
Give them, O LORD, whatsoever Thou wilt give; give them a miscarrying womb and dry breasts.
15 'Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali, ndivyo nilipowachukia. Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi, nitawafukuza nje ya nyumba yangu. Sitawapenda tena; maofisa wao wote ni waasi.
All their wickedness is in Gilgal, for there I hated them; because of the wickedness of their doings I will drive them out of My house; I will love them no more, all their princes are rebellious.
16 Efraimu ni mgonjwa, na mizizi yao imekauka; hawazai matunda. Hata ikiwa wana watoto, nitawaua watoto wao wapendwa.
Ephraim is smitten, their root is dried up, they shall bear no fruit; yea, though they bring forth, yet will I slay the beloved fruit of their womb.
17 Mungu wangu atawakataa kwa sababu hawakumtii. Watakuwa watu wa kutangatanga kati ya mataifa.
My God will cast them away, because they did not hearken unto Him; and they shall be wanderers among the nations.

< Hosea 9 >