< Hosea 7 >

1 Wakati wowote ninapotaka kuponya Israeli, dhambi ya Efraimu inafunuliwa, pamoja na matendo maovu ya Samaria, kwa sababu wanafanya udanganyifu; mwizi huingia, na kundi la wanyang'anyi hushambulia mitaani.
Al curar Yo a Israel, se ha descubierto la iniquidad de Efraím y la perversidad de Samaria: practican la mentira; por dentro hay ladrones, y por fuera roban bandidos.
2 Hawatambui mioyoni mwao kwamba ninakumbuka matendo yao mabaya. Sasa matendo yao huwazunguka; yapo mbele ya uso wangu.
No piensan en su corazón que Yo me acuerdo de todas sus maldades. Ahora los rodean sus obras que están ante mi vista.
3 Kwa sababu ya uovu wao wamemfanya mfalme awe na furaha, na maofisa wao kwa uongo wao.
Regocijan al rey con sus perversidades, y a los príncipes con sus mentiras.
4 Wote ni wazinzi, kama tanuru iliyochomwa na mwokaji, ambaye huacha kuuchochea moto tangu kukanda unga mpaka kuwa chachu.
Son adúlteros todos, como horno encendido por el hornero; este cesa de atizar (el fuego), mientras se amasa, hasta la fermentación.
5 Siku ya mfalme wetu, viongozi walijifanya wagonjwa na ukali wa divai. Alinyoosha mkono wake kwa wale waliokuwa wakidhihaki.
En la fiesta de nuestro rey, los príncipes loquearon tomados de vino; y él tendió su mano a los burladores.
6 kwa mioyo kama tanuri, wao hupanga mipango yao ya udanganyifu. Hasira zao hulala usiku wote; asubuhi huwaka juu kama moto.
Porque ellos se acercaron, siendo como horno su corazón mientras le acechaban. Toda la noche durmió su hornero, y a la mañana el (horno) ardió cual llama abrasadora.
7 Wote wamepata moto kama tanuru, na huwaangamiza wale wanaowatawala. Wafalme wao wote wameanguka; hakuna hata mmoja wao ananiita.
Todos están encendidos como un horno; devoran a sus jueces, todos sus reyes han caído; no hay entre ellos quien clame a Mí.
8 Efraimu anajichanganya mwenyewe kati ya watu. Efraimu ni mkate ambayo haujawahi kugeuzwa.
Efraím se ha mezclado con los pueblos; Efraím es una torta a la cual no se ha dado vuelta.
9 Wageni wamekula nguvu zake, lakini hajui. Nywele za mvi hunyunyiza juu yake, lakini hajui.
Los extranjeros han devorado su fuerza, y él no se dio cuenta; también las canas se esparcieron sobre él sin que lo advirtiera.
10 Kiburi cha Israeli kinawashuhudia; hata hivyo, hawajarudi kwa Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta licha ya hayo yote.
La soberbia de Israel se manifiesta en su misma cara; pero no se convierten a Yahvé su Dios, y con todo esto no lo buscan.
11 Efraimu ni kama njiwa, baradhuli na asiye na busara, humwita kwenda Misri, kisha huruka kwenda Ashuru.
Efraím ha venido a ser como una paloma tonta y falta de entendimiento: llaman a Egipto, acuden a Asiria.
12 Wakienda, nitasambaza wavu wangu juu yao, nami nitawaangusha kama ndege wa angani. Nitawaadhibu katika kusonga kwao pamoja.
Pero mientras vayan, tenderé sobre ellos mi red; los haré caer cual ave del cielo; los castigaré según lo anunciado en sus asambleas.
13 Ole wao! Kwa maana wamepotea kutoka kwangu. Uharibifu unawajia! Wao wameasi dhidi yangu! Napenda kuwaokoa, lakini waliongea uongo dhidi yangu.
¡Ay de ellos porque se han apartado de Mí! ¡Ruina sobre ellos, por cuanto contra Mí se han rebelado! Yo iba a salvarlos, pero ellos hablaban mentiras de Mí.
14 Wala hawakunililia kwa moyo wao wote, lakini wanaomboleza kwenye vitanda vyao. Wanakusanyika kwa ajili ya nafaka na divai mpya, nao wananiasi mimi.
Y no me invocan de corazón cuando gimen sobre sus camas; es por el trigo y el vino por lo que se preocupan; así se apartan de Mí.
15 Ingawa niliwafundisha na kuimarisha mikono yao, sasa wanapanga mabaya dhidi yangu.
Yo les he enseñado, he dado vigor a sus brazos, pero ellos maquinan contra Mí el mal.
16 Wanarudi, lakini harudi kwangu, Niliye Juu. Wao ni kama upinde usiotumainika. Maofisa wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya udhalimu wa vinywa. Hii itakuwa ni aibu yao katika nchi ya Misri.
Vuelven a sacudir el yugo, son como arco engañoso. Sus príncipes caerán a espada, en castigo de la saña de su lengua. Por eso se mofarán de ellos en la tierra de Egipto.

< Hosea 7 >