< Hosea 7 >

1 Wakati wowote ninapotaka kuponya Israeli, dhambi ya Efraimu inafunuliwa, pamoja na matendo maovu ya Samaria, kwa sababu wanafanya udanganyifu; mwizi huingia, na kundi la wanyang'anyi hushambulia mitaani.
When heal I Israel and it is revealed [the] iniquity of Ephraim and [the] evil deeds of Samaria for they do falsehood and a thief he comes it attacks a marauding band in the street.
2 Hawatambui mioyoni mwao kwamba ninakumbuka matendo yao mabaya. Sasa matendo yao huwazunguka; yapo mbele ya uso wangu.
And not they say to heart their all evil their I remember now they have surrounded them deeds their before face my they are.
3 Kwa sababu ya uovu wao wamemfanya mfalme awe na furaha, na maofisa wao kwa uongo wao.
By evil their they make glad [the] king and by lies their princes.
4 Wote ni wazinzi, kama tanuru iliyochomwa na mwokaji, ambaye huacha kuuchochea moto tangu kukanda unga mpaka kuwa chachu.
All of them [are] adulterers like an oven burning from a baker [who] he ceases stirring up from kneading [the] dough until is leavened it.
5 Siku ya mfalme wetu, viongozi walijifanya wagonjwa na ukali wa divai. Alinyoosha mkono wake kwa wale waliokuwa wakidhihaki.
[the] day of King our they became sick princes fever from wine he stretched out hand his with scorners.
6 kwa mioyo kama tanuri, wao hupanga mipango yao ya udanganyifu. Hasira zao hulala usiku wote; asubuhi huwaka juu kama moto.
For they have brought near like oven heart their in ambush their all the night [is] sleeping baker their morning it [is] burning like a fire of flame.
7 Wote wamepata moto kama tanuru, na huwaangamiza wale wanaowatawala. Wafalme wao wote wameanguka; hakuna hata mmoja wao ananiita.
All of them they are hot like oven and they devour rulers their all kings their they have fallen there not [is one who] calls among them to me.
8 Efraimu anajichanganya mwenyewe kati ya watu. Efraimu ni mkate ambayo haujawahi kugeuzwa.
Ephraim among the peoples he he mixes himself Ephraim he has become a bread cake not turned over.
9 Wageni wamekula nguvu zake, lakini hajui. Nywele za mvi hunyunyiza juu yake, lakini hajui.
They have consumed strangers strength his and he not he knows also gray hair it has sneaked in on him and he not he knows.
10 Kiburi cha Israeli kinawashuhudia; hata hivyo, hawajarudi kwa Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta licha ya hayo yote.
And it testifies [the] pride of Israel in face its and not they have returned to Yahweh God their and not they have sought him for all this.
11 Efraimu ni kama njiwa, baradhuli na asiye na busara, humwita kwenda Misri, kisha huruka kwenda Ashuru.
And he has become Ephraim like a dove silly there not [is] heart Egypt they have called Assyria they have gone.
12 Wakienda, nitasambaza wavu wangu juu yao, nami nitawaangusha kama ndege wa angani. Nitawaadhibu katika kusonga kwao pamoja.
Just when they will go I will spread over them net my like [the] bird[s] of the heavens I will bring down them I will chasten them according to a report to assembly their.
13 Ole wao! Kwa maana wamepotea kutoka kwangu. Uharibifu unawajia! Wao wameasi dhidi yangu! Napenda kuwaokoa, lakini waliongea uongo dhidi yangu.
Woe! to them for they have fled from me devastation [belongs] to them for they have transgressed against me and I I will redeem them and they they have spoken on me lies.
14 Wala hawakunililia kwa moyo wao wote, lakini wanaomboleza kwenye vitanda vyao. Wanakusanyika kwa ajili ya nafaka na divai mpya, nao wananiasi mimi.
And not they have cried out to me with heart their if they wail on beds their on grain and new wine they assemble themselves they turn aside against me.
15 Ingawa niliwafundisha na kuimarisha mikono yao, sasa wanapanga mabaya dhidi yangu.
And I I instructed [them] I strengthened arms their and against me they plot evil.
16 Wanarudi, lakini harudi kwangu, Niliye Juu. Wao ni kama upinde usiotumainika. Maofisa wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya udhalimu wa vinywa. Hii itakuwa ni aibu yao katika nchi ya Misri.
They turn - not height they have become like a bow of slackness they will fall by the sword leaders their from [the] indignation of tongue their this [will be] mockery their in [the] land of Egypt.

< Hosea 7 >