< Hosea 5 >

1 Sikilizeni haya, makuhani! kuweni makini, nyumba ya Israeli! Sikilizeni, nyumba ya mfalme! Kwa maana hukumu itakuja juu yenu nyote. Mmekuwa mtego huko Mizpa na wavu uliosambazwa juu ya Tabori.
Hear this, O ye priests, and hearken, ye house of Israel, and give ear, O house of the king, for unto you pertain the judgment; for ye have been a snare at Mizpah, and a net spread upon Tabor.
2 Waasi husimama sana katika mauaji, lakini nitawaadhibu wote.
And the revolters are gone deep in making slaughter; but I am a rebuker of them all.
3 Najua Efraimu, na Israeli hajajificha kwangu. Efraimu, sasa umekuwa kama kahaba; Israeli ni unajisi.
I know Ephraim, and Israel is not hid from me: for now, O Ephraim, thou hast committed whoredom, Israel is defiled.
4 Matendo yao hayawataruhusu kumgeukia Mungu, maana mawazo ya uzinzi yako ndani yao, na hawatamjua Bwana.
Their doings will not suffer them to turn unto their God: for the spirit of whoredom is within them, and they know not the LORD.
5 Kiburi cha Israeli kinawashuhudia; Kwa hiyo Israeli na Efraimu watajikwaa kwa hatia zao; na Yuda pia wataanguka pamoja nao.
And the pride of Israel doth testify to his face: therefore Israel and Ephraim shall stumble in their iniquity; Judah also shall stumble with them.
6 Watakwenda pamoja na kondoo zao na ng'ombe zao kumtafuta Bwana, lakini hawatamuona, kwa kuwa amejiondoa kutoka kwao.
They shall go with their flocks and with their herds to seek the LORD; but they shall not find him: he hath withdrawn himself from them.
7 Walikuwa wasio waaminifu kwa Bwana, kwa kuwa wamezaa watoto haramu. Sasa sherehe mpya za mwezi zitawaangamiza na mashamba yao.
They have dealt treacherously against the LORD; for they have borne strange children: now shall the new moon devour them with their fields.
8 Piga tarumbeta huko Gibea, na tarumbeta huko Rama. Sauti ya kilio cha vita huko Beth Aveni 'Tutakufuata, Benyamini!'
Blow ye the cornet in Gibeah, and the trumpet in Ramah: sound an alarm at Beth-aven; behind thee, O Benjamin.
9 Efraimu itakuwa ukiwa siku ya adhabu. Miongoni mwa makabila ya Israeli nimetangaza habari itakayotokea.
Ephraim shall become a desolation in the day of rebuke: among the tribes of Israel have I made known that which shall surely be.
10 Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaondoao jiwe la mipaka. Nami nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama maji.
The princes of Judah are like them that remove the landmark: I will pour out my wrath upon them like water.
11 Efraimu ameangamizwa; ameangamizwa kwa hukumu, kwa sababu ametembea kwa hiari kufuata sanamu.
Ephraim is oppressed, he is crushed in judgment; because he was content to walk after the command.
12 Kwa hiyo nitakuwa kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa nyumba ya Yuda.
Therefore am I unto Ephraim as a moth, and to the house of Judah as rottenness.
13 Efraimu alipoona ugonjwa wake, Yuda akaona jeraha lake; Efraimu akaenda Ashuru; Yuda akatuma wajumbe kwa mfalme mkuu. Lakini hakuweza kuwaponya watu au kuponya jeraha lako.
When Ephraim saw his sickness, and Judah [saw] his wound, then went Ephraim to Assyria, and sent to king Jareb: but he is not able to heal you, neither shall he cure you of your wound.
14 Kwa hiyo nitakuwa kama simba kwa Efraimu, na kama simba kwa nyumba ya Yuda. Mimi, naam mimi, nitapotea na kwenda mbali; Nitawachukua, na hakutakuwa na mtu wa kuwaokoa.
For I will be unto Ephraim as a lion, and as a young lion to the house of Judah: I, even I, will tear and go away; I will carry off, and there shall be none to deliver.
15 Nitakwenda na kurudi mahali pangu, mpaka watambue hatia yao na kutafuta uso wangu, hata wakanitafute kwa bidii katika dhiki yao.
I will go and return to my place, till they acknowledge their offence, and seek my face: in their affliction they will seek me earnestly.

< Hosea 5 >