< Hosea 3 >

1 Bwana akaniambia, “Nenda tena, mpendeni mwanamke, aliyependwa na mumewe; lakini ni mzinzi. Mpende kama mimi, Bwana, ninavyowapenda watu wa Israeli, ingawa wanaigeukia miungu mingine na kupenda mikate ya zabibu.”
And the LORD said unto me: 'Go yet, love a woman beloved of her friend and an adulteress, even as the LORD loveth the children of Israel, though they turn unto other gods, and love cakes of raisins.
2 Kwa hiyo nimemnunulia mwenyewe kwa vipande kumi na tano vya fedha na homeri na letheki ya shayiri.
So I bought her to me for fifteen pieces of silver and a homer of barley, and a half-homer of barley;
3 Nilimwambia, “Lazima uishi pamoja nami siku nyingi. Huwezi kuwa kahaba au kuwa na mtu mwingine yeyote. Kwa njia hiyo hiyo, nitakuwa pamoja nanyi.”
and I said unto her: 'Thou shalt sit solitary for me many days; thou shalt not play the harlot, and thou shalt not be any man's wife; nor will I be thine.'
4 Kwa maana wana wa Israeli wataishi kwa siku nyingi bila mfalme, mtu mkuu, dhabihu, nguzo ya mawe, efodi au sanamu za nyumbani.
For the children of Israel shall sit solitary many days without king, and without prince, and without sacrifice, and without pillar, and without ephod or teraphim;
5 Baadaye watu wa Israeli watarudi na kumtafuta Bwana Mungu wao na Daudi mfalme wao. Na katika siku za mwisho, watakuja wakitetemeka mbele za Bwana na wema wake.
afterward shall the children of Israel return, and seek the LORD their God, and David their king; and shall come trembling unto the LORD and to His goodness in the end of days.

< Hosea 3 >