< Hosea 13 >

1 Efraimu alipozungumza, kulikuwa na tetemeko. Alijikuza katika Israeli, lakini akawa na hatia kwa sababu ya ibada ya Baali, naye akafa.
When Ephraim spoke, there was trembling. He exalted himself in Israel, but when he became guilty in Baal, he died.
2 Sasa wanafanya dhambi zaidi na zaidi. Wanatengeneza sanamu za chuma kutoka kwenye fedha zao, sanamu kwa kadiri ya ufanisi wao, zote ni kazi ya mafundi. Watu wanasema juu yao, 'Watu hawa watoao dhabihu na kumbusu ndama.'
Now they sin more and more, and have made themselves molten images of their silver, even idols according to their own understanding, all of them the work of the craftsmen. They say of them, 'They offer human sacrifice and kiss the calves.'
3 Kwa hiyo watakuwa kama mawingu ya asubuhi, kama umande unaoondoka mapema, kama makapi yanayotokana na upepo kutoka kwenye sakafu, na kama moshi utokao kwenye bomba.
Therefore they will be like the morning mist, and like the dew that passes away early, like the chaff that is driven with the whirlwind out of the threshing floor, and like the smoke out of the chimney.
4 Lakini mimi ndimi Bwana, Mungu weko, tangu nchi ya Misri. Hutamjua Mungu mwingine bali mimi; wala zaidi yangu, hakuna mkombozi mwingine.
"Yet I am Jehovah your God from the land of Egypt; and you shall acknowledge no god but me, and besides me there is no savior.
5 Nilikujua jangwani, katika nchi yenye kame.
I fed you in the wilderness, in the land of great drought.
6 Wakati ulipokuwa na malisho, ulishiba; na wakati uliposhiba, moyo wako ukainuliwa. Kwa sababu hiyo umenisahau.
According to their pasture, so were they filled; they were filled, and their heart was exalted. Therefore they have forgotten me.
7 Nitakuwa kama simba; kama chui nitaangalia kando ya njia.
Therefore I am like a lion to them. Like a leopard, I will lurk by the path.
8 Nitawaangamiza kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake. Nami nitararua vifua vyao, na huko nitawaangamiza kama simba, kama vile mnyama wa mwitu atakayerarua vipande vipande.
I will meet them like a bear that is bereaved of her cubs, and will tear the covering of their heart. There I will devour them like a lioness. The wild animal will tear them.
9 Nitawaangamiza, Israeli; nani atakayekusaidia?
You are destroyed, Israel, because you are against me, against your help.
10 Mfalme wako yuko wapi, ili akuokoe katika miji yako yote? Wako wapi wakuu, ambao kwao umeniambia hivi, 'Nipe mfalme na wakuu'?
Where is your king now, that he may save you in all your cities? And your judges, of whom you said, 'Give me a king and princes?'
11 Nimekupa mfalme kwa hasira yangu, nikamchukua kwa ghadhabu yangu.
I have given you a king in my anger, and have taken him away in my wrath.
12 Uovu wa Efraimu umehifadhiwa; hatia yake imehifadhiwa.
The guilt of Ephraim is stored up. His sin is stored up.
13 Atakuwa na uchungu wa kujifungua, lakini ni mwana mjinga, kwa maana wakati wa kuzaliwa, hatatoka tumboni.
The sorrows of a travailing woman will come on him. He is an unwise son; for when it is time, he doesn't come to the opening of the womb.
14 Je, nitawaokoa na mkono wa kaburi? Je, nitawaokoa na kifo? Ewe Mauti yako wapi mapigo yako? Ewe kaburi kuko wapi kuharibu kwako? Huruma itafichwa na macho yangu. (Sheol h7585)
I will ransom them from the power of Sheol. I will redeem them from death. Death, where is your victory? Sheol, where is your sting? "Compassion will be hidden from my eyes. (Sheol h7585)
15 Ingawa Efraimu anafanikiwa kati ya ndugu zake, upepo wa mashariki utakuja; upepo wa Bwana utapiga kutoka jangwani. Kijito cha maji cha Efraimu kitauka, na kisima chake hakitakuwa na maji. Adui yake atapora ghala lake la kila kitu cha thamani.
Though he is fruitful among his brothers, an east wind will come, the breath of Jehovah coming up from the wilderness; and his spring will become dry, and his fountain will be dried up. He will plunder the storehouse of treasure.
16 Samaria itakuwa na hatia, kwa sababu amemuasi dhidi ya Mungu wake. Wataanguka kwa upanga; watoto wao wadogo watavunjwa, na wanawake wao wajawazito watatambuliwa wazi.
Samaria will bear her guilt; for she has rebelled against her God. They will fall by the sword. Their infants will be dashed in pieces, and their pregnant women will be ripped open."

< Hosea 13 >