< Hosea 1 >

1 Hili ni neno la Bwana lililofika kwa Hosea mwana wa Beeri siku za Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi, mfalme wa Israeli.
THE WORD of the LORD that came unto Hosea the son of Beeri, in the days of Uzziah, Jotham, Ahaz, and Hezekiah, kings of Judah, and in the days of Jeroboam the son of Joash, king of Israel.
2 Wakati Bwana alipozungumza kwanza kupitia Hosea, akamwambia, “Nenda ukajitwalie mke ambaye ni kahaba. Atakuwa na watoto ambao ni matokeo ya ukahaba wake. Kwa maana nchi inafanya uzinzi mkubwa kwa kumwacha Bwana.”
When the LORD spoke at first with Hosea, the LORD said unto Hosea: 'Go, take unto thee a wife of harlotry and children of harlotry; for the land doth commit great harlotry, departing from the LORD.'
3 Basi Hosea akaenda akamwoa Gomeri binti Diblaimu, naye akachukua mimba, akazaa mtoti mwanamume.
So he went and took Gomer the daughter of Diblaim; and she conceived, and bore him a son.
4 Bwana akamwambia Hosea, Mwite jina lake Yezreeli. Kwa maana kwa muda mfupi nitaiadhibu nyumba ya Yehu kwa sababu ya kumwaga damu huko Yezreeli; nami nitamaliza ufalme wa nyumba ya Israeli.
And the LORD said unto him: 'Call his name Jezreel; for yet a little while, and I will visit the blood of Jezreel upon the house of Jehu, and will cause to cease the kingdom of the house of Israel.
5 Itatokea siku ile nitakapovunja upinde wa Israeli katika bonde la Yezreeli.
And it shall come to pass at that day, that I will break the bow of Israel in the valley of Jezreel.'
6 Gomeri akachukua mimba tena akamzaa binti. Ndipo Bwana akamwambia Hosea, “Mwite jina lake Lo Ruhama; kwa maana sitawahurumia tena nyumba ya Israeli, nisije nikawasamehe kwa njia yoyote.
And she conceived again, and bore a daughter. And He said unto him: 'Call her name Lo-ruhamah; for I will no more have compassion upon the house of Israel, that I should in any wise pardon them.
7 Hata hivyo nitawahurumia nyumba ya Yuda, nami nitawaokoa mwenyewe, Bwana, Mungu wao. Sitawaokoa kwa upinde, upanga, vita, farasi, au wapanda farasi. '
But I will have compassion upon the house of Judah, and will save them by the LORD their God, and will not save them by bow, nor by sword, nor by battle, nor by horses, nor by horsemen.'
8 Baada ya Gomeri kumwachisha Lo Ruhama, alipata mimba na kuzaa mtoto mwingine mwanamume.
Now when she had weaned Lo-ruhamah, she conceived, and bore a son.
9 Ndipo Bwana akasema, “Mwite jina la Lo Ami; kwa kuwa ninyi si watu wangu, wala mimi si Mungu wenu.”
And He said: 'Call his name Lo-ammi; for ye are not My people, and I will not be yours.'
10 Hata hivyo idadi ya watu wa Israeli itakuwa kama mchanga wa bahari, ambayo haiwezi kupimwa au kuhesabiwa. Itakuwa pale ambapo waliambiwa, “Ninyi si watu wangu,” wataambiwa, “Ninyi ni watu wa Mungu aliye hai.”
Yet the number of the children of Israel shall be as the sand of the sea, which cannot be measured nor numbered; and it shall come to pass that, instead of that which was said unto them: 'Ye are not My people', it shall be said unto them: 'Ye are the children of the living God.'
11 Watu wa Yuda na watu wa Israeli watakusanyika pamoja. Wao wataweka kiongozi mmoja wao wenyewe, na watatoka kutoka nchi, kwa maana itakuwa siku ya Yezreeli kuu.
And the children of Judah and the children of Israel shall be gathered together, and they shall appoint themselves one head, and shall go up out of the land; for great shall be the day of Jezreel.

< Hosea 1 >