< Habakuki 2 >

1 Nitasimama kwenye nguzo yangu ya ulinzi na kujiweka mwenyewe juu ya mnara wa mlinzi, na nitatazama kwa makini kuona yeye atasema nini kwangu na namna gani nitageuka kutoka kwenye lawama yangu.
I will stand upon my watch, and mount upon the rock, and watch to see what he will say by me, and what I shall answer when I am reproved.
2 Yahwe alinijibu na alisema, “Rekodi maono haya, na uandike dhahiri juu ya kibao ili kwamba anayesoma anaweza kukimbia.
And the Lord answered me and said, Write the vision, and [that] plainly on a tablet, that he that reads it may run.
3 Sababu maono haya bado ni kwa wakati ujao na hatimaye atazungumza bila kuanguka. Ingawa inachelewa, isubiri. Sababu kwa hakika itatakuja na haitachelewa.
For the vision [is] yet for a time, and it shall shoot forth at the end, and not in vain: though he should tarry, wait for him; for he will surely come, and will not tarry.
4 Tazama! yule ambae hamu yake siyo sawa ndani yake anapumua kwa nguvu. Lakini mwenye haki ataishi kwa imani.
If he should draw back, my soul has no pleasure in him: but the just shall live by my faith.
5 Sababu mvinyo ni msaliti wa kijana mwenye kiburi ili kwamba asistahimili, lakini hukuza tamaa yake kama kaburi na, kama kifo, haitaweza kuridhishwa. Yeye anajikusanyia kila taifa na anakusanya kwaajili yake watu wote. (Sheol h7585)
But the arrogant man and the scorner, the boastful man, shall not finish anything; who has enlarged his desire as the grave, and like death he is never satisfied, and he will gather to himself all the nations, and will receive to himself all the peoples. (Sheol h7585)
6 Haya yote hayatatengeneza usemi kumdhihaki na wimbo wa dhihaka unaomhusu, 'ole wake yule aongezaye visivyo vya kwake! kwa muda gani utaongeza uzito wa dhamana uliyochukua?'
Shall not all these take up a parable against him? and a proverb to tell against him? and they shall say, Woe to him that multiplies to himself the possessions which are not his! how long? and who heavily loads his yoke.
7 Wale wanao ngojea kwako hawatainuka ghafla? na wale wanaokutetemesha kuamka? Utakuwa mwathirika kwaajili yao.
For suddenly there shall arise up those that bite him, and they that plot against thee shall awake, and thou shalt be a plunder to them.
8 Kwasababu umeteka nyara watu wengi, mabaki yote ya watu, yatakuteka nyara wewe. Sababu umemwaga damu nyingi za watu na umetenda kwa uasi kinyume cha nchi, miji, na wote wanaokaa ndani yake.
Because thou hast spoiled many nations, all the nations that are left shall spoil [thee], because of the blood of men, and the sins of the land and city, and of all that dwell in it.
9 Ole kwa yule anayechonga mapato maovu kwaajili ya nyumba yake, hivyo anaweza kutengeneza kiota chake juu kumweka yeye salama mbali na mikono ya uovu.
Woe to him that covets an evil covetousness to his house, that he may set his nest on high, that he may be delivered from the power of evils.
10 Umebuni aibu kwa nyumba yako kwa kuwakata watu wengi, na umefanya dhambi dhidi yako mwenyewe.
Thou hast devised shame to thy house, thou hast utterly destroyed many nations, and thy soul has sinned.
11 Sababu jiwe litapaza sauti kutoka ukutani, na pao la mbao litawajibu,
For the stone shall cry out of the wall, and the beetle out of the timber shall speak.
12 'Ole wake yule ajengaye mji kwa damu, na anayeimarisha mji kwa katika uovu.
Woe to him that builds a city with blood, and establishes a city by unrighteousness.
13 Hii haitoki kwa Yahwe wa majeshi kwamba watu wafanye kazi kwa moto na mataifa yote mengine yanachakaa menyewe bila kitu?
Are not these things of the Lord Almighty? surely many people have been exhausted in the fire, and many nations have fainted.
14 Bado nchi itajaa maarifa ya utukufu wa Yahwe kama maji yanavyojaza bahari.
For the earth shall be filled with the knowledge of the glory of the Lord; it shall cover them as water.
15 'Ole wake yule anayemfanya jirani yake alewe, wewe ambaye unaye ongeza sumu uwafanye walewe ili uweze kutazama uchi wao.
Woe to him that gives his neighbour to drink the thick lees [of wine], and intoxicates [him], that he may look upon their secret parts.
16 Utavimbiwa na aibu zaidi kuliko utukufu. Kunywa hiyo vilevile, na funua uchi wako mwenyewe. Kikombe cha mkono wa kuume wa Yahwe utakuja katika kukugeukia wewe, na aibu itafunika heshima yako.
Drink thou also [thy] fill of disgrace instead of glory: shake, O heart, and quake, the cup of the right hand of the Lord has come round upon thee, and dishonour has gathered upon thy glory.
17 Vurugu iliyofanywa kwa Lebanoni itakufunika na uharibifu wa wanyama utakuogopesha. Sababu umemwaga damu za watu na umetenda kwa uasi dhidi ya ile nchi, miji, na wote wanaokaa humo.
For the ungodliness of Libanus shall cover thee, and distress because of wild beasts shall dismay thee, because of the blood of men, and the sins of the land and city, and of all that dwell in it.
18 Sanamu iliyochongwa inakufaidia nini? Sababu yule aliyeichonga hiyo, au ambaye kaisubu kwa kuiyeyusha metali, ni mwalimu wa uongo; Sababu anaiamini kazi ya mikono yake anapotengeneza miungu hii isiyoongea.
What profit it the graven image, that they have graven it? [one] has made it a molten work, a false image; for the maker has trusted in his work, to make dumb idols.
19 'Ole kwa yule anayeuambia ubao, Amka! Au kwa jiwe lisiloongea, Inuka!' Vitu hivi vinafundisha? Angalia, hiki juu kimefunikwa kwa dhahabu na fedha, lakini ndani yake hakipumui kabisa.
Woe to him that says to the wood, Awake, arise; and to the stone, Be thou exalted! whereas it is an image, and this is a casting of gold and silver, and there is no breath in it.
20 Lakini Yahwe yumo katika hekalu lake takatifu! Nchi yote iwe kimya mbele zake.
But the Lord is in his holy temple: let all the earth fear before him.

< Habakuki 2 >