< Mwanzo 9 >

1 Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
و خدا، نوح و پسرانش را برکت داده، بدیشان گفت: «بارور و کثیر شوید و زمین را پر سازید.۱
2 Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
و خوف شما و هیبت شما بر همه حیوانات زمین و بر همه پرندگان آسمان، و بر هرچه بر زمین می‌خزد، و بر همه ماهیان دریا خواهدبود، به‌دست شما تسلیم شده‌اند.۲
3 Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
و هرجنبنده‌ای که زندگی دارد، برای شما طعام باشد. همه را چون علف سبز به شما دادم،۳
4 Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
مگرگوشت را با جانش که خون او باشد، مخورید.۴
5 Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
وهر آینه انتقام خون شما را برای جان شما خواهم گرفت. از دست هر حیوان آن را خواهم گرفت. واز دست انسان، انتقام جان انسان را از دست برادرش خواهم گرفت.۵
6 Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
هر‌که خون انسان ریزد، خون وی به‌دست انسان ریخته شود. زیرا خداانسان را به صورت خود ساخت.۶
7 Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
و شما بارور وکثیر شوید، و در زمین منتشر شده، در آن بیفزایید.»۷
8 Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
و خدا نوح و پسرانش را با وی خطاب کرده، گفت:۸
9 “Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
«اینک من عهد خود را با شما و بعداز شما با ذریت شما استوار سازم،۹
10 na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
و با همه جانورانی که با شما باشند، از پرندگان و بهایم و همه حیوانات زمین با شما، با هر‌چه از کشتی بیرون آمد، حتی جمیع حیوانات زمین.۱۰
11 Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
عهدخود را با شما استوار می‌گردانم که بار دیگر هرذی جسد از آب طوفان هلاک نشود، و طوفان بعداز این نباشد تا زمین را خراب کند.»۱۱
12 Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
و خدا گفت: «اینست نشان عهدی که من می‌بندم، در میان خود و شما، و همه جانورانی که با شما باشند، نسلا بعد نسل تا به ابد:۱۲
13 Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
قوس خود را در ابر می‌گذارم، و نشان آن عهدی که درمیان من و جهان است، خواهد بود.۱۳
14 Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
و هنگامی که ابر را بالای زمین گسترانم، و قوس در ابر ظاهرشود،۱۴
15 ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
آنگاه عهد خود را که در میان من و شما وهمه جانوران ذی جسد می‌باشد، بیاد خواهم آورد. و آب طوفان دیگر نخواهد بود تا هرذی جسدی را هلاک کند.۱۵
16 Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
و قوس در ابرخواهد بود، و آن را خواهم نگریست تا بیاد آورم آن عهد جاودانی را که در میان خدا و همه جانوران است، از هر ذی جسدی که بر زمین است.»۱۶
17 Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
و خدا به نوح گفت: «این است نشان عهدی که استوار ساختم در میان خود و هرذی جسدی که بر زمین است.»۱۷
18 Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
و پسران نوح که از کشتی بیرون آمدند، سام و حام و یافث بودند. و حام پدر کنعان است.۱۸
19 Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
اینانند سه پسر نوح، و از ایشان تمامی جهان منشعب شد.۱۹
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
و نوح به فلاحت زمین شروع کرد، وتاکستانی غرس نمود.۲۰
21 Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
و شراب نوشیده، مست شد، و در خیمه خود عریان گردید.۲۱
22 Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
و حام، پدر کنعان، برهنگی پدر خود را دید و دو برادرخود را بیرون خبر داد.۲۲
23 Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
و سام و یافث، ردا راگرفته، بر کتف خود انداختند، و پس رفته، برهنگی پدر خود را پوشانیدند. و روی ایشان بازپس بود که برهنگی پدر خود را ندیدند.۲۳
24 Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
و نوح از مستی خود به هوش آمده، دریافت که پسرکهترش با وی چه کرده بود.۲۴
25 Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
پس گفت: «کنعان ملعون باد! برادران خود را بنده بندگان باشد.»۲۵
26 Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
وگفت: «متبارک باد یهوه خدای سام! و کنعان، بنده او باشد.۲۶
27 Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
خدا یافث را وسعت دهد، و درخیمه های سام ساکن شود، و کنعان بنده او باشد.»۲۷
28 Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
و نوح بعد از طوفان، سیصد و پنجاه سال زندگانی کرد.۲۸
29 Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.
پس جمله ایام نوح نهصد وپنجاه سال بود که مرد.۲۹

< Mwanzo 9 >