< Mwanzo 8 >

1 Mungu akamtazama Nuhu, wanyama wote wa mwitu, na wanyama wote wa kufugwa ambao walikuwa pamoja naye kwenye safina. Mungu akafanya upepo uvume juu ya nchi, na maji yakaanza kuzama chini.
And he remembered God Noah and every animal and all the livestock which [were] with him in the ark and he made to pass God a wind over the earth and they subsided the waters.
2 Chemichemi za vilindi pamoja na madirisha ya mbingu vikafungwa, na mvua ikakoma kunyesha.
And they were shut up [the] springs of [the] deep and [the] floodgates of the heavens and it was restrained the rain from the heavens.
3 Maji ya gharika yakaanza kuzama kidogo kidogo katika nchi. na mwisho wa siku miamoja na hamsini maji yakawa yamezama chini.
And they turned back the waters from on the earth going and turning back and they decreased the waters from [the] end of fifty and one hundred day[s].
4 safina ikatulia katika mwezi wa saba, siku ya kumi na saba ya mwezi, juu ya milima ya Ararati.
And it rested the ark in the month seventh on [the] seven-teen day of the month on [the] mountains of Ararat.
5 Maji yakaendelea kuzama chini hadi mwezi wa kumi. Siku ya kwanza ya mwezi, vilele vya milima vikaonekana.
And the waters they were going and decreasing until the month tenth in the tenth [month] on [day] one of the month they were seen [the] tops of the mountains.
6 Ikatokea kwamba baada ya siku arobaini Nuhu alifungua dirisha la safina ambayo aliitengeneza.
And it was from [the] end of forty day[s] and he opened Noah [the] window of the ark which he had made.
7 Akatuma kunguru na akaruka hadi maji yalipo kauka katika nchi.
And he sent out the raven and it went out continuously and returned until dried up the waters from on the earth.
8 Kisha akatuma njiwa kuona kama maji yamezama chini kutoka kwenye uso wa nchi,
And he sent out the dove from with him to see ¿ were they abated the waters from on [the] surface of the ground.
9 lakini njiwa hakuona sehemu ya kutua unyayo wake, na akarudi kwake ndani ya safina, kwa kuwa maji yalikuwa bado yamefunika nchi yote. Akanyoosha mkono wake, akamchukua na kumuweka ndani ya safina pamoja naye.
And not found the dove a resting place for [the] sole of foot its and it returned to him into the ark for water [was] on [the] surface of all the earth and he stretched out hand his and he took it and he brought it to him into the ark.
10 Akasubiri siku saba zingine akatuma tena njiwa kutoka kwenye safina.
And he waited again seven days other and he repeated to send out the dove from the ark.
11 Njiwa akarudi kwake jioni. Tazama! katika mdomo wake kulikuwa na jani bichi la mzeituni lililochumwa. Kwa hiyo Nuhu akatambua kuwa maji yamekwisha zama chini ya nchi.
And it came to him the dove to [the] time of evening and there! a leaf of olive freshly plucked [was] in mouth its and he knew Noah that they were abated the waters from on the earth.
12 Akasubiri siku saba zingine na akamtuma njiwa tena. Njiwa hakurudi kwake tena.
And he waited again seven days other and he sent out the dove and not it repeated to return to him again.
13 Ikawa kwamba katika mwaka wa mia sita na moja, katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, maji yalikuwa yamekauka katika nchi. Nuhu akaondoa kifuniko cha safina, akatazama nje, na akaona kwamba, Tazama, uso wa nchi ulikuwa umekauka.
And it was in one and six hundred year in the first [month] on [day] one of the month they were dried up the waters from on the earth and he removed Noah [the] covering of the ark and he saw and there! they were dried up [the] surface of the ground.
14 Katika mwezi wa pili, siku ya ishirini na saba ya mwezi, nchi ilikuwa imekauka.
And in the month second on [the] seven and twenty day of the month was dry the earth.
15 Mungu akamwambia Nuhu,
And he spoke God to Noah saying.
16 “Toka nje ya safina, wewe, mke wako, wanao wa kiume, na wake wa wanao pamoja nawe.
Go out from the ark you and wife your and sons your and [the] wives of sons your with you.
17 Wachukuwe utoke nje pamoja nao kila kiumbe hai chenye mwili ambacho kiko nawe - ndege, wanyama wa kufugwa, na kila kitambaacho ambacho hutambaa juu ya nchi - ili kwamba viweze kukua na kuwa na idadi kubwa zaidi ya viumbe hai katika nchi yote, kwa kuzaliana na kuongezeka juu ya nchi.”
Every animal which [is] with you some of all flesh among the bird[s] and among the livestock and among every creeping thing which creeps on the earth (bring out *Qk) with you and they will swarm on the earth and they will be fruitful and they will multiply on the earth.
18 Kwa hiyo Nuhu akatoka nje pamoja na watoto wake wa kiume, mke wake, na wake wa wa wanawe pamoja naye.
And he went out Noah and sons his and wife his and [the] wives of sons his with him.
19 Kila kiumbe hai, kila kitambaacho, na kila ndege, na kila kiendacho juu ya nchi, kwa kabila zao, wakaiacha safina.
Every animal every creeping thing and every bird every creeping [thing] on the earth to families their they went out from the ark.
20 Nuhu akajenga madhabahu kwa Yahwe. Akachukua baadhi ya wanyama walio safi na baadhi ya ndege walio safi, na kutoa sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
And he built Noah an altar to Yahweh and he took some of all - the livestock clean and some of every bird clean and he offered up burnt offerings on the altar.
21 Yahwe akanusa harufu nzuri ya kuridhisha na akasema moyoni mwake, “Sita laani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, ingawa nia za mioyo yao ni mbaya tokea utoto. Wala sita haribu kilakitu chenye uhai, kama nilivyo fanya.
And he smelled Yahweh [the] odor of soothing and he said Yahweh to heart his not I will repeat to curse again the ground for sake of humankind for [the] inclination of [the] heart of humankind [is] evil since youth his and not I will repeat again to strike down every living [thing] just as I have done.
22 Wakati nchi isaliapo, majira ya kupanda mbegu na mavuno, baridi na joto, kiangazi na majira ya baridi, mchana na usiku havitakoma.”
Again all [the] days of the earth seed and harvest and cold and heat and summer and winter and day and night not they will cease.

< Mwanzo 8 >

A Dove is Sent Forth from the Ark
A Dove is Sent Forth from the Ark