< Mwanzo 5 >

1 Hii ni orodha ya vizazi vya Adamu. Katika siku ambayo Mungu alimuumba mtu, aliwaumba katika mfano wake mwenyewe.
This is the book of the generations of Adam. In the day that God created man, in the likeness of God made He him;
2 Mwanaume na mwanamke aliwaumba. Akawabariki na akawaita Adam wakati walipoumbwa.
male and female created He them, and blessed them, and called their name Adam, in the day when they were created.
3 Wakati Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, akamzaa mwana katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake, na akamuita jina lake Sethi.
And Adam lived a hundred and thirty years, and begot a son in his own likeness, after his image; and called his name Seth.
4 Baada ya Adamu kumzaa Sethi, aliishi miaka mia nane. Akawazaa wana wengi waume na wake.
And the days of Adam after he begot Seth were eight hundred years; and he begot sons and daughters.
5 Adamu akaishi miaka 930 kisha akafariki.
And all the days that Adam lived were nine hundred and thirty years; and he died.
6 Wakati Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
And Seth lived a hundred and five years, and begot Enosh.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, akaishi miaka 807 na akawazaa wana wengi waume na wake.
And Seth lived after he begot Enosh eight hundred and seven years, and begot sons and daughters.
8 Sethi akaishi miaka 912 kisha akafariki.
And all the days of Seth were nine hundred and twelve years; and he died.
9 Wakati Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
And Enosh lived ninety years, and begot Kenan.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
And Enosh lived after he begot Kenan eight hundred and fifteen years, and begot sons and daughters.
11 Enoshi aliishi miaka 905 na kisha akafariki.
And all the days of Enosh were nine hundred and five years; and he died.
12 Wakati Kanani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
And Kenan lived seventy years, and begot Mahalalel.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
And Kenan lived after he begot Mahalalel eight hundred and forty years, and begot sons and daughters.
14 Kenani aliishi miaka 910, na kisha akafariki.
And all the days of Kenan were nine hundred and ten years; and he died.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, alimzaa Yaredi.
And Mahalalel lived sixty and five years, and begot Jared.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
And Mahalalel lived after he begot Jared eight hundred and thirty years, and begot sons and daughters.
17 Mahalaleli aliishi miaka 895 na kisha akafariki.
And all the days of Mahalalel were eight hundred ninety and five years; and he died.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, alimzaa Henoko.
And Jared lived a hundred sixty and two years, and begot Enoch.
19 Baada ya kumzaa Henoko, Yaredi aliishi miaka mianane. Akazaa wana wengi waume na wake.
And Jared lived after he begot Enoch eight hundred years, and begot sons and daughters.
20 Yaredi aliishi miaka 962 na kisha akafariki.
And all the days of Jared were nine hundred sixty and two years; and he died.
21 Henoko alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, akamzaa Methusela.
And Enoch lived sixty and five years, and begot Methuselah.
22 Henoko akaenenda na Mungu miaka miatatu baada ya kumzaa Methusela. Aliwazaa wana wengi wa ume na wake.
And Enoch walked with God after he begot Methuselah three hundred years, and begot sons and daughters.
23 Henoko aliishi miaka 365.
And all the days of Enoch were three hundred sixty and five years.
24 Henoko alienenda na Mungu, na kisha alitoweka, kwa kuwa Mungu alimtwaa.
And Enoch walked with God, and he was not; for God took him.
25 Wakati Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, alimzaa Lameki.
And Methuselah lived a hundred eighty and seven years, and begot Lamech.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
And Methuselah lived after he begot Lamech seven hundred eighty and two years, and begot sons and daughters.
27 Methusela aliishi miaka 969. Kisha akafariki.
And all the days of Methuselah were nine hundred sixty and nine years; and he died.
28 Wakati Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
And Lamech lived a hundred eighty and two years, and begot a son.
29 Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
And he called his name Noah, saying: 'This same shall comfort us in our work and in the toil of our hands, which cometh from the ground which the LORD hath cursed.'
30 Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
And Lamech lived after he begot Noah five hundred ninety and five years, and begot sons and daughters.
31 Lameki aliishi miaka 777. Kisha akafariki.
And all the days of Lamech were seven hundred seventy and seven years; and he died.
32 Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.
And Noah was five hundred years old; and Noah begot Shem, Ham, and Japheth.

< Mwanzo 5 >