< Mwanzo 48 >

1 Ikawa baada ya mambo haya, mmojawapo akamwambia Yusufu, “Tazama, baba yako ni mgonjwa.” Hivyo akaondoka pamoja na wanawe wawili, Manase na Efrahimu.
And it came about after these things that someone said to Joseph, "Look, your father is sick." And taking with him his two sons, Manasseh and Ephraim, he went to Jacob.
2 Yakobo alipoambiwa, “Tazama, mwanao Yusufu amekuja kukuona,” Israeli akakusanya nguvu na kukaa juu ya kitanda.
And someone reported to Jacob, and said, "Look, your son Joseph has come to you." Then Israel strengthened himself and sat up in the bed.
3 Yakobo akamwambia Yusufu, Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani. Akanibariki na
And Jacob said to Joseph, "El Shaddai appeared to me at Luz in the land of Canaan and blessed me,
4 kuniambia, 'Tazama, nitakupa uzao mwingi, na kukuzidisha. Nitakufanya kuwa kusanyiko la mataifa. Nitakupa nchi hii wewe na uzao wako kuwa milki ya milele.'
and said to me, 'Look, I will make you fruitful and multiply you, and I will make of you a company of peoples, and will give this land to your descendants after you as an everlasting possession.'
5 Na sasa wanao wawili, waliozaliwa kwako katika nchi ya Misri kabla sijaja Misri, ni wangu. Efrahimu na Manase watakuwa wangu, kama walivyo Rubeni na Simioni.
And now your two sons, who were born to you in the land of Egypt before I came to you into Egypt, are mine; Ephraim and Manasseh will be mine, as Reuben and Simeon are.
6 Watoto utakaowapata baada ya hapo ni wako; watahesabiwa katika majina ya ndugu zao katika urithi wao.
And your offspring born to you after them will be yours. But in their inheritance they are to be called after the names of their brothers.
7 Lakini kwangu mimi, nilipokuja kutoka Padani, kwa uzuni yangu Raheli alikufa njiani katika nchi ya Kanaani, wakati kungalipo kitambo kwenda Efrathi. Nilimzika pale katika njia iendayo Efrathi” (ndio, Bethlehemu).
But as for me, when I came from Paddan Aram, Rachel died, in my sorrow, in the land of Canaan on the journey, when there was still some distance to go to Ephrath. And I buried her there on the way to Ephrath (that is, Bethlehem)."
8 Israeli alipowaona wana wa Yusufu, akasema, “Ni nani hawa?”
Then Israel saw Joseph's sons, and said, "Who are these?"
9 Yusufu akamwambia baba yake, “Hawa ni wanangu, Mungu alionipa hapa:” Israeli akasema, “Walete kwangu, kwamba niwabariki.”
And Joseph said to his father, "They are my sons, whom God has given me here." And he said, "Please bring them to me, so that I can bless them."
10 Basi macho ya Israeli yalikuwa yanashindwa kwa ajili ya umri wake, hivyo hakuweza kuona. Hivyo Yusufu akawasogeza karibu yake, na akawabusu na kuwakumbatia.
Now the eyes of Israel were failing because of his age, so that he couldn't see. Then he brought them near to him, and he kissed them and embraced them.
11 Israeli akamwambia Yusufu, “Sikutazamia kuuona uso wako tena, Lakini Mungu ameniruhusu kuwaona hata wanao.”
And Israel said to Joseph, "I did not expect to see your face, but look, God has let me see your offspring as well."
12 Yusufu akawaondoa kati ya magoti ya Israeli, na kisha akainama na uso wake juu ya nchi.
Then Joseph brought them out from between his knees, and he bowed himself with his face to the ground.
13 Yusufu akawachukua wote wawili, Efrahimu katika mkono wake wa kulia kuelekea mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kulia kuelekea mkono wa kulia wa Israeli, na akawasogeza kwake.
And Joseph took them both, Ephraim in his right hand toward Israel's left hand, and Manasseh in his left hand toward Israel's right hand, and brought them near to him.
14 Israeli akainua mkono wake wa kulia na kuuweka juu ya kichwa cha Efrahimu, aliyekuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto juu ya kichwa cha Manase. Akaipishanisha mikono yake, kwani Manase ndiye alikuwa mzaliwa wa kwanza.
And Israel stretched out his right hand and placed it on Ephraim's head, who was the younger, and his left hand on Manasseh's head, crossing his hands, although Manasseh was the firstborn.
15 Israeli akambariki Yusufu, akisema, Mungu ambaye mbele zake baba zangu Ibrahimu na Isaka walitembea, Mungu aliyenilinda hata leo,
Then he blessed Joseph, and said, "The God before whom my fathers Abraham and Isaac walked, the God who has been my shepherd all my life to this day,
16 malaika walionilinda na madhara yote, awabariki vijana hawa. Jina langu na litajwe kwao, na majina ya baba zangu Ibrahimu na Isaka. Na wawe makutano ya watu juu ya nchi.”
the Angel who has redeemed me from all evil, bless the boys. And may my name be carried on in them, and the names of my fathers Abraham and Isaac. And may they grow into a multitude upon the earth."
17 Yusufu alipoona baba yake ameweka mkono wake wa kulia juu ya kichwa cha Efrahimu, haikumpendeza. Akauchukuwa mkono wa baba yake auweke katika kichwa cha Manase.
When Joseph saw that his father placed his right hand on the head of Ephraim, it displeased him, and he grasped his father's hand to move it from Ephraim's head to Manasseh's head.
18 Yusufu akamwambia baba yake, “Sivyo babangu; kwani huyu ndiye mzaliwa wa kwanza. Uweke mkono wako juu ya kichwa chake.”
And Joseph said to his father, "Not so, my father, for this one is the firstborn. Put your right hand on his head."
19 Baba yake akakataa na kusema, “Ninafahamu, mwanangu, nafahamu. Yeye naye atakuwa watu, naye pia atakuwa mkuu. Lakini mdogo wake atakuwa mkuu kuliko yeye, na uzao wake utakuwa wingi wa mataifa.”
But his father refused, and said, "I know, my son, I know. He also will become a people, and he also will be great. However, his younger brother will be greater than he, and his descendants will become a multitude of nations."
20 Israeli akawabariki siku hiyo kwa maneno haya, “Watu wa Israeli watatamka baraka kwa majina yenu wakisema, Mungu na akufanye kama Efrahimu na kama Manase'. “Kwa njia hii, Israeli akamweka Efrahimu mbele ya Manase.
So he blessed them that day, saying, "By you Israel will pronounce blessing, saying, 'God make you as Ephraim and as Manasseh.'" Thus he put Ephraim before Manasseh.
21 Israeli akamwambia Yusufu, “Tazama, ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
Then Israel said to Joseph, "Look, I am about to die, but God will be with you, and God will bring you back from this land to the land of your fathers.
22 Kwako wewe, kwa kuwa uko juu ya ndugu zako, ninakupa mtelemko wa mlima niliouchukuwa kutoka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”
Moreover, I give to you one portion more than your brothers, which I took out of the hand of the Amorites with my sword and with my bow."

< Mwanzo 48 >