< Mwanzo 47 >

1 Kisha Yusufu akaingia kwa Farao na kumwambia, “Baba yangu na ndugu zangu, kondoo wao, mbuzi wao, na yote waliyonayo, wamefika kutoka katika nchi ya Kanaani. Tazama, wapo katika nchi ya Gosheni.”
Józef więc przyszedł i powiedział faraonowi: Mój ojciec i moi bracia ze swymi owcami, wołami i ze wszystkim, co mają, przybyli z ziemi Kanaan; oto są w ziemi Goszen.
2 Akawachukua watano katika ndugu zake na kuwatambulisha kwa Farao.
A spośród swych braci wziął pięciu mężczyzn i przedstawił ich faraonowi.
3 Farao akawambia ndugu zake, “Kazi yenu ni nini?” Wakamwambia Farao, “Watumishi wako ni wafugaji, kama mababu zetu.”
I faraon zapytał jego braci: Czym się zajmujecie? A [oni] odpowiedzieli faraonowi: Twoi słudzy [są] pasterzami, my i nasi ojcowie.
4 Kisha wakamwambia Farao, “Tumekuja kukaa kwa muda katika nchi. Hakuna malisho kwa ajili ya makundi ya watumishi wako, kwa maana njaa ni kali sana katika nchi ya Kanaani. Hivyo, tafadhari waache watumishi wako wakae katika nchi ya Gosheni.”
Powiedzieli jeszcze do faraona: Przyszliśmy, aby przebywać w tej ziemi, bo nie ma paszy dla stad, które [mają] twoi słudzy, gdyż ciężki głód [panuje] w ziemi Kanaan. Teraz prosimy, pozwól, aby twoi słudzy mieszkali w ziemi Goszen.
5 Kisha Farao akamwambia Yusufu, kusema, “Baba yako na ndugu zako wamekuja kwako.
Wtedy faraon powiedział do Józefa: Twój ojciec i twoi bracia przybyli do ciebie.
6 Nchi ya Misri iko mbele yako. Mkalishe baba yako na ndugu zako katika eneo zuri, nchi ya Gosheni. Ikiwa unafahamu watu wenye uwezo miongoni mwao, uwaweke kuwatunza wanyama wangu.”
Ziemia Egiptu jest przed tobą. W najlepszym [miejscu] tej ziemi osadź twego ojca i twoich braci, niech mieszkają w ziemi Goszen. A jeśli wiesz, że są wśród nich dzielni ludzie, uczyń ich przełożonymi nad moimi stadami.
7 Kisha Yusufu akamwingiza Yakobo baba yake na kumweka mbele ya Farao. Yakobo akambariki Farao.
I Józef przyprowadził swego ojca Jakuba, i postawił go przed faraonem. A Jakub błogosławił faraona.
8 Farao akamwambia Yakobo, “Umeishi kwa muda gani?”
Faraon zapytał Jakuba: Ile lat życia sobie liczysz?
9 Yakobo akamwambia Farao, “Miaka ya safari zangu ni mia moja na thelathini. Miaka ya maisha yangu imekuwa mifupi na ya maumivu. Siyo kama miaka ya baba zangu.”
Jakub odpowiedział faraonowi: Liczba lat mego pielgrzymowania to sto trzydzieści. Krótkie i złe były lata mego życia i nie osiągnąłem wieku moich ojców podczas ich pielgrzymowania.
10 Kisha Yakobo akambariki Farao na kuondoka mbele zake.
Potem Jakub pobłogosławił faraona i odszedł sprzed jego oblicza.
11 Kisha Yusufu akamweka baba yake na ndugu zake. Akawapa eneo katika nchi ya Misri, sehemu nzuri sana ya nchi, katika eneo la Ramesesi, kama Farao alivyokuwa ameagiza.
Wtedy Józef osiedlił swego ojca i swoich braci i dał im posiadłość w ziemi Egiptu, w najlepszym [miejscu] tej krainy, w ziemi Ramses, jak rozkazał faraon.
12 Yusufu akamhudumia baba yake kwa chakula, ndugu zake, na nyumba yote ya baba yake, kulingana na hesabu ya wahitaji wao.
I Józef żywił chlebem swego ojca i swoich braci, i cały dom swego ojca, aż do najmniejszego.
13 Basi hakukuwa na chakula katika nchi yote; kwani njaa ilikuwa kali sana. Nchi ya Misri na nchi ya Kanaani ikaharibika kwa sababu ya njaa.
A w całej ziemi nie [było] chleba, bo panował bardzo ciężki głód i była utrapiona przez głód ziemia Egiptu i ziemia Kanaan.
14 Yusufu akakusanya pesa yote iliyokuwa katika nchi ya Misri na nchi ya Kanaani, kwa kuwauzia wakaaji wake chakula. Kisha Yusufu akaleta ile pesa katika kasri la Farao.
Józef zebrał więc wszystkie pieniądze, które znajdowały się w ziemi Egiptu i w ziemi Kanaan, za żywność, którą kupowano. I Józef wniósł te pieniądze do skarbu faraona.
15 Pesa yote ya nchi za Misri na Kanaani ilipokwisha, Wamisri wote wakaja kwa Yusufu wakisema, “Tupe chakula! Kwa nini tufe mbele zako kwa maana pesa yetu imekwisha?”
A gdy zabrakło pieniędzy w ziemi Egiptu i w ziemi Kanaan, wszyscy Egipcjanie przyszli do Józefa i powiedzieli: Daj nam chleba. Dlaczego mamy umierać na twoich oczach? Gdyż nam już zabrakło pieniędzy.
16 Yusufu akasema, “Ikiwa pesa yenu imekwisha, leteni wanyama wenu nami nitawapa chakula badala ya wanyama wenu.”
Józef na to odpowiedział: Dajcie wasze bydła, a dam wam [żywność] za wasze bydła, skoro zabrakło [wam] pieniędzy.
17 Hivyo wakaleta wanyama wao kwa Yusufu. Yusufu akawapa chakula kwa kubadilishana na farasi, kondoo, mbuzi na kwa punda. Akawalisha kwa mkate kwa kubadilisha na wanyama wao mwaka ule.
Przyprowadzili więc swoje bydła do Józefa; i Józef dał im chleb za konie, za trzody owiec, za stada wołów i za osły. W tym roku zaopatrywał ich w żywność w zamian za wszelkie ich bydło.
18 Mwaka ule ulipokwisha, wakaja kwake mwaka uliofuata na kumwambia, “Hatutaficha kwa bwana wangu kwamba pesa yetu yote imekwisha, na wanyama ni wa bwana wangu. Hakuna kilichobaki mbele za bwana wangu, isipokuwa miili yetu na nchi yetu.
A gdy minął ten rok, przyszli do niego w następnym roku i powiedzieli: Nie ukryjemy przed naszym panem, że już skończyły się nam pieniądze, a stada bydła [należą] do naszego pana. Nie zostaje [nam] nic przed naszym panem jak tylko nasze ciała i nasze pole.
19 Kwa nini tufe mbele za macho yake, sisi na nchi yetu? Utununue sisi na nchi yetu badala ya chakula, na sisi na nchi yetu tutakuwa watumishi wa Farao. Tupe mbegu ili kwamba tuishi na tusife, na kwamba nchi isiwe tupu bila watu.
Dlaczego mamy umierać na twoich oczach, zarówno my, jak i nasza ziemia? Kupuj za chleb nas i nasze pole, a my i nasza ziemia będziemy w niewoli u faraona. Daj [nam] tylko ziarno, abyśmy żyli, a nie pomarli, i by ziemia nie opustoszała.
20 Hivyo Yusufu akamnunulia Farao nchi yote ya Misri. Kwani kila Mmisri akauza shamba lake, kwa sababu njaa ilikuwa kali sana. Kwa njia hii, nchi ikawa mali ya Farao.
I tak kupił Józef [całą] ziemię Egiptu dla faraona, bo każdy Egipcjanin sprzedał swoje pole, gdyż wzmógł się wśród nich głód. I cała ziemia stała się [własnością] faraona.
21 Na watu, akawafanya kuwa watumwa kutoka mpaka mmoja wa Misri hata mkapa mwingine.
I przeniósł lud do miast, od jednego krańca Egiptu do drugiego.
22 Ilikuwa ni nchi ya makuhani pekee ambayo Yusufu hakuinunua, kwa maana makuhani walikuwa wakipewa posho. Walikula katika sehemu aliyowapa Farao. Kwa hiyo hawakuuza nchi yao.
Nie kupił tylko ziemi kapłanów, bo kapłani mieli [żywność] przydzieloną im przez faraona i żywili się swoją żywnością, którą dał im faraon. Dlatego nie sprzedali swej ziemi.
23 Kisha Yusufu akawambia watu, “Tazama, nimewanunua ninyi na nchi yenu leo kwa ajili ya Farao. Basi mbegu hii hapa kwa ajili yenu, nanyi mtapanda katika nchi.
Potem Józef powiedział do ludu: Oto teraz kupiłem was i waszą ziemię dla faraona. Macie tu ziarno, obsiejcie nim pola.
24 Wakati wa mavuno, mtampa Farao sehemu ya tano, na sehemu nne zitakuwa zenu, kwa mbegu za shamba na kwa chakula cha nyumba zenu na watoto wenu.”
A piątą część [waszych] plonów oddacie faraonowi, cztery zaś części będą wasze – na obsianie pól i na żywność dla tych, którzy są w waszych domach, i na żywność [dla] waszych dzieci.
25 Wakasema, “Umeokoa maisha yetu. Na tupate kibali machoni pako. Tutakuwa watumishi wa Farao.”
Wtedy odpowiedzieli: Uratowałeś nam życie! Obyśmy znaleźli łaskę w oczach swego pana, a będziemy niewolnikami faraona.
26 Hivyo Yusufu akaifanya kuwa sheria inayofanya kazi hata leo katika nchi ya Misri, kwamba moja ya tano ni ya Farao. Eneo la makuhani peke yake ndo halikufanywa kuwa la Farao.
I Józef ustanowił to jako prawo aż do dziś w ziemi Egiptu, aby faraonowi [oddawano] piątą część [plonów]. Tylko ziemia samych kapłanów nie stała się [własnością] faraona.
27 Hivyo Israeli akaishi katika nchi ya Misri, katika eneo la Gosheni. Watu wake wakapata umiliki pale. Walikuwa wenye kuzaa na kuongezeka sana.
Izrael mieszkał w ziemi Egiptu, w ziemi Goszen. Nabywali w niej posiadłości na własność, byli płodni i bardzo się rozmnożyli.
28 Yakobo akaishi katika nchi ya Misri miaka kumi na saba, kwa hiyo miaka ya maisha ya Yakobo ilikuwa miaka mia moja arobaini na saba.
I Jakub żył w ziemi Egiptu siedemnaście lat. A w sumie Jakub przeżył sto czterdzieści siedem lat.
29 Wakati wa kufa kwake Yakobo ulipokaribia, alimwita Yusufu mwanaye na kumwambia, “Ikiwa nimepata kibali mbele zako, weka mkono wako chini ya paja langu, na unitendee kwa uaminifu na kweli. Tafadhari usinizike Misri.
I zbliżył się czas śmierci Izraela. Wezwał więc swego syna Józefa i powiedział do niego: Jeśli teraz znalazłem łaskę w twoich oczach, połóż, proszę, twoją rękę pod moje biodro, a wyświadcz mi tę łaskę i wierność: Proszę, nie chowaj mnie w Egipcie;
30 Nitakapolala na baba zangu, utanitoa Misri na kunizika katika eneo la kuzikia la baba zangu.” Yusufu akasema, “Nitafanya kama ulivyosema.”
Ale [gdy] zasnę z moimi ojcami, wywieziesz mnie z Egiptu i pochowasz mnie w ich grobie. A on powiedział: Uczynię według twego słowa.
31 Israeli akasema, “Niapie,” na Yusufu akamwapia. Kisha Israeli akainama chini mbele ya kitanda chake.
A [Jakub] powiedział: Przysięgnij mi. I przysiągł mu. Potem Izrael pokłonił się na wezgłowie łoża.

< Mwanzo 47 >