< Mwanzo 46 >

1 Israeli akasafiri na yote aliyokuwa nayo na akaja Beersheba. Pale akatoa sadaka kwa Mungu wa Isaka baba yake.
Israel [God prevails] traveled with all that he had, and came to Be'er-Sheva [Well of Seven, Well of an Oath], and offered sacrifices to the God of his father, Isaac [Laughter].
2 Mungu akamwambia Israeli katika ndoto usiku, akisema, “Yakobo, Yakobo.”
God spoke to Israel [God prevails] in the visions of the night, and said, “Jacob [Supplanter], Jacob [Supplanter]!” He said, “Here I am.”
3 Akasema, “Mimi hapa.” Akasema, “Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako. Usiogope kushuka Misri, kwa maana nitakufanya taifa kubwa huko.
He said, “I am God, the God of your father. Don’t be afraid to go down into Egypt [Abode of slavery], for there I will make of you a great nation.
4 Nitakwenda pamoja nawe huko Misri, Nami nitakupandisha huku tena bila shaka. Na Yusufu akayafunika macho yako kwa mikono wake.”
I will go down with you into Egypt [Abode of slavery]. I will also surely bring you up again. Joseph [May he add] will close your eyes.”
5 Yakobo akainuka kutoka Beersheba. Wana wa Israeli wakamsafirisha Yakobo baba yao, watoto wao, na wake wao, katika mikokotene ambayo Farao alikuwa ameipeleka kuwachukua.
Jacob [Supplanter] rose up from Be'er-Sheva [Well of Seven, Well of an Oath], and the sons of Israel [God prevails] carried Jacob [Supplanter], their father, their little ones, and their wives, in the wagons which Pharaoh had sent to carry him.
6 Wakachukua mifugo yao na mali zao walizokuwa wamezipata katika nchi ya Kanaani. Wakaja Misri, Yakobo na uzao wake wote pamoja naye.
They took their livestock, and their goods, which they had gotten in the land of Canaan [Humbled], and came into Egypt [Abode of slavery]— Jacob, and all his offspring with him,
7 Akaja Misri pamoja na wanawe na wana wa wanawe, binti zake na wana wa binti zake, na uzao wake wote.
his sons, and his sons’ sons with him, his daughters, and his sons’ daughters, and he brought all his offspring with him into Egypt [Abode of slavery].
8 Haya ni majina ya watoto wa Israeli waliokuja Misri, Yakobo na wanawe: Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Yakobo;
These are the names of the children of Israel [God prevails], who came into Egypt [Abode of slavery], Jacob [Supplanter] and his sons: Reuben [See, a son!], Jacob [Supplanter]’s firstborn.
9 wana wa Rubeni Hanoki na Palu na Hezroni na Karmi;
The sons of Reuben [See, a son!]: Hanoch, Pallu, Hezron, and Carmi.
10 wana wa Simoni, Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli, wana wa mwanamke Mkanaani;
The sons of Simeon [Hearing]: Jemuel, Jamin, Ohad, Jachin, Zohar, and Shaul [Asked for] the son of a Canaanite [Descendant of Humbled] woman.
11 wana wa Lawi Gershoni, Kohathi, na Merari.
The sons of Levi [United with]: Gershon, Kohath, and Merari.
12 Wana wa Yuda: Eri, Shela, Peresi, na Zera, (Lakini Eri na Onani walikufa katika nchi ya Kanaani). Na wana wa Peresi walikuwa Hezroni na Hamuli.
The sons of Judah [Praised]: Er, Onan, Shelah, Perez, and Zerah; but Er and Onan died in the land of Canaan [Humbled]. The sons of Perez were Hezron and Hamul.
13 Wana wa Isakari walikuwa Tola, Puva, Lobu, na Shimroni;
The sons of Issachar [Hire, Reward]: Tola, Puvah, Job [Persecuted], and Shimron.
14 Wana wa Zabuloni walikuwa Seredi, Eloni, na Yahleeli
The sons of Zebulun [Living together]: Sered, Elon, and Jahleel.
15 Hawa walikuwa wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padani Aramu, pamoja na na Dina binti yake. Wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
These are the sons of Leah [Weary], whom she bore to Jacob [Supplanter] in Paddan Aram [Elevated], with his daughter Dinah. All the souls of his sons and his daughters were thirty-three.
16 Wana wa Gadi walikuwa Zifioni, Hagi, Shuni, Ezboni, Eri, Arodi, na Areli.
The sons of Gad [Good fortune]: Ziphion, Haggi, Shuni, Ezbon, Eri, Arodi, and Areli.
17 Wana wa Asheri walikuwa Imna, Ishva, Ishvi, na Beria; na Sera alikuwa dada yao. Wana wa Beria walikuwa Heberi na Malkieli.
The sons of Asher [Happy]: Imnah, Ishvah, Ishvi, Beriah, and Serah their sister. The sons of Beriah: Heber and Malchiel.
18 Hawa walikuwa wana wa Zilpa, ambaye Labani alikuwa amempa Lea binti yake. Wana aliomzalia Yakobo wote walikuwa kumi na sita.
These are the sons of Zilpah [Frailty], whom Laban [White] gave to Leah [Weary], his daughter, and these she bore to Jacob [Supplanter], even sixteen souls.
19 Wana wa Raheli mkewe Yakobo walikuwa Yusufu na Benjamini.
The sons of Rachel [Ewe sheep], Jacob [Supplanter]’s wife: Joseph [May he add] and Benjamin [Son of right hand, Son of south].
20 Huko Misri Manase na Efraimu walizaliwa kwa Yusufu na Asenathi, binti Potifera kuhani wa Oni.
To Joseph [May he add] in the land of Egypt [Abode of slavery] were born Manasseh [Causing to forget] and Ephraim [Fruit], whom Asenath, the daughter of Potiphera, priest of On, bore to him.
21 Wana wa Benjamini walikuwa Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu, na Ardi.
The sons of Benjamin [Son of right hand, Son of south]: Bela, Becher, Ashbel, Gera, Naaman, Ehi, Rosh, Muppim, Huppim, and Ard.
22 Hawa walikuwa wana wa Raheli waliozaliwa kwa Yakobo - jumla yao kumi na wanne.
These are the sons of Rachel [Ewe sheep], who were born to Jacob [Supplanter]: all the souls were fourteen.
23 Mwana wa Dani alikuwa Hushimu.
The son of Dan [He judged]: Hushim.
24 Wana wa Naftali walikuwa Yahzeeli, Guni, Yezeri, na Shilemi.
The sons of Naphtali [My wrestling]: Jahzeel, Guni, Jezer, and Shillem.
25 Hawa walikuwa wana Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alimpa Raheli binti yake - wote walikuwa saba.
These are the sons of Bilhah [Bashful], whom Laban [White] gave to Rachel [Ewe sheep], his daughter, and these she bore to Jacob [Supplanter]: all the souls were seven.
26 Wate waliokwenda na Yakobo, waliokuwa uzao wake, bila kuhesabu wake wa wana wa Yakobo walikuwa sitini na sita.
All the souls who came with Jacob [Supplanter] into Egypt [Abode of slavery], who were his direct offspring, besides Jacob [Supplanter]’s sons’ wives, all the souls were sixty-six.
27 Pamoja na wana wawili wa Yusufu waliozaliwa kwake huko Misri, watu wa familia yake waliokwenda Misri walikuwa sabini jumla yao.
The sons of Joseph [May he add], who were born to him in Egypt [Abode of slavery], were two souls. All the souls of the house of Jacob [Supplanter], who came into Egypt [Abode of slavery], were seventy.
28 Yakobo akamtuma Yuda kuwatangulia mbele kwa Yusufu kuonesha njia mbele yake kwenda Gosheni, nao wakaja katika eneo la Gosheni.
He sent Judah [Praised] before him to Joseph [May he add], to show the way before him to Goshen [Drawing near], and they came into the land of Goshen [Drawing near].
29 Yusufu akaandaa kibandawazi chake na akaenda kumlaki baba yake huko Gosheni. Akamwona, akaikumbatia shingo yake, na akalia shingoni mwake kwa kitambo.
Joseph [May he add] prepared his chariot, and went up to meet Israel [God prevails], his father, in Goshen [Drawing near]. He presented himself to him, and fell on his neck, and wept on his neck a good while.
30 Israeli akamwambia Yusufu, “Basi na nife sasa, kwa kuwa nimeuona uso wako, kwamba bado uko hai.”
Israel [God prevails] said to Joseph [May he add], “Now let me die, since I have seen your face, that you are still alive.”
31 Yusufu akawambia ndungu zake na nyumba ya baba yake, “Nitakwenda na kumwambia Farao, kusema, 'Ndugu zangu na nyumba ya baba yangu, waliokuwa katika nchi ya Kanaani, wamenijia.
Joseph [May he add] said to his brothers, and to his father’s house, “I will go up, and speak with Pharaoh, and will tell him, ‘My brothers, and my father’s house, who were in the land of Canaan [Humbled], have come to me.
32 Watu hawa ni wafugaji, kwani wamekuwa watunza wanyama. Wamekuja na makundi yao ya kondoo, na mbuzi, na vyote walivyonavyo.'
These men are shepherds, for they have been keepers of livestock, and they have brought their flocks, and their herds, and all that they have.’
33 Itakuwa, Farao atakapowaita na kuwauliza, 'Kazi yenu ni ipi?'
It will happen, when Pharaoh summons you, and will say, ‘What is your occupation?’
34 mwambieni, 'Watumishi wako wamekuwa watunza wanyama tangu ujana wetu mpaka sasa, sisi, na baba zetu.' Fanyeni hivyo ili mweze kuishi katika nchi ya Gosheni, kwani kila mfugaji ni chukizo kwa Wamisri.”
that you shall say, ‘Your servants have been keepers of livestock from our youth even until now, both we, and our fathers:’ that you may dwell in the land of Goshen [Drawing near]; for every shepherd is an abomination to the Egyptians [people from Abode of slavery].”

< Mwanzo 46 >