< Mwanzo 42 >

1 Basi Yakobo akafahamu kwamba kuna nafaka huko Misri. Akawambia wanawe, “Kwa nini mnatazamana?
Now Jacob saw that there was corn in Egypt, and Jacob said unto his sons: 'Why do ye look one upon another?'
2 Akasema, “Tazama, nimesikia kwamba kuna nafaka huko Misri. Shukeni huko mkatununulie chakula ili tuishi wala tusife.”
And he said: 'Behold, I have heard that there is corn in Egypt. Get you down thither, and buy for us from thence; that we may live, and not die.'
3 Ndugu kumi wa Yusufu wakashuka Misri kununua chakula.
And Joseph's ten brethren went down to buy corn from Egypt.
4 Lakini Benjamini, ndugu wa Yusufu, Yakobo hakumtuma na ndugu zake, kwani alihofu kwamba madhara yaweza kumpata.
But Benjamin, Joseph's brother, Jacob sent not with his brethren; for he said: 'Lest peradventure harm befall him.'
5 Wana wa Israeli wakaja kununua miongoni mwao waliokuja, kwani njaa ilikuwapo katika nchi ya Kanaani.
And the sons of Israel came to buy among those that came; for the famine was in the land of Caanan.
6 Basi Yusufu alikuwa mtawala juu ya nchi. Ndiye aliyekuwa akiwauzia watu wote wa nchi. Ndugu zake Yusufu wakaja na kumwinamia na nyuso zao hata chini.
And Joseph was the governor over the land; he it was that sold to all the people of the land. And Joseph's brethren came, and bowed down to him with their faces to the earth.
7 Yusufu akawaona ndugu zake na kuwatambua, lakini alijibadili kwao na kuongea nao kwa ukali. Akawambia, “Mmetoka wapi?” Wakasema, “Kutoka nchi ya Kanaani ili kununua chakula.”
And Joseph saw his brethren, and he knew them, but made himself strange unto them, and spoke roughly with them; and he said unto them: 'Whence come ye?' And they said: 'From the land of Canaan to buy food.'
8 Yusufu akawatambua ndugu zake, lakini wao hawakumtambua.
And Joseph knew his brethren, but they knew him not.
9 Yusufu akazikumbuka ndoto aliyoziota kuhusu wao. Akawambia, “Ninyi ni wapelelezi. Mmekuja kuona sehemu za nchi zisizolindwa.”
And Joseph remembered the dreams which he dreamed of them, and said unto them: 'Ye are spies; to see the nakedness of the land ye are come.'
10 Wakamwambia, “Hapana, bwana wangu. Watumishi wako wamekuja kununua chakula.
And they said unto him: 'Nay, my lord, but to buy food are thy servants come.
11 Sisi sote ni wana wa baba mmoja. Ni watu wa kweli. Watumishi wako siyo wapelelezi.”
We are all one man's sons; we are upright men, thy servants are no spies.'
12 Akawambia, “Hapana, mmekuja kuangalia sehemu za nchi zisizolindwa.”
And he said unto them: 'Nay, but to see the nakedness of the land ye are come.'
13 Wakasema, “Sisi watumishi wako tupo ndugu kumi na wawili, wana wa baba mmoja katika nchi ya Kanaani. Tazama, mdogo yupo na baba yetu, na mwingine hayupo hai tena.”
And they said: 'We thy servants are twelve brethren, the sons of one man in the land of Canaan; and, behold, the youngest is this day with our father, and one is not.'
14 Yusufu akawambia, “Ndivyo nilivyowambia; ninyi ni wapelelezi.
And Joseph said unto them: 'That is it that I spoke unto you, saying: Ye are spies.
15 Mtajaribiwa kwa njia hii. Kama aishivyo Farao, hamtaondoka hapa, mdogo wenu asipokuja hapa.
Hereby ye shall be proved, as Pharaoh liveth, ye shall not go forth hence, except your youngest brother come hither.
16 Mtumeni mmoja wenu amlete mdogo wenu. Mtabaki gerezani, hata maneno yenu yatakapothibitishwa, kwamba kuna ukweli ndani yenu.”
Send one of you, and let him fetch your brother, and ye shall be bound, that your words may be proved, whether there be truth in you; or else, as Pharaoh liveth, surely ye are spies.'
17 Akawaweka kifungoni kwa siku tatu.
And he put them all together into ward three days.
18 Katika siku ya tatu Yusufu akaongea nao, “Fanyeni hivi nanyi mtaishi, kwani ninamcha Mungu.
And Joseph said unto them the third day. 'This do, and live; for I fear God:
19 Kama ninyi ni watu wa kweli, mmoja wenu atazuiliwa hapa gerezani, lakini ninyi nendeni, chukueni nafaka kwa ajili ya nyumba zenu.
if ye be upright men, let one of your brethren be bound in your prison-house; but go ye, carry corn for the famine of your houses;
20 Mleteni mdogo wenu kwangu ili kwamba maneno yenu yathibitishwe nanyi hamtakufa.” Wakafanya hivyo.
and bring your youngest brother unto me; so shall your words be verified, and ye shall not die.' And they did so.
21 Wakasemezana wao kwa wao, “Kwa kweli tuna hatia juu ya ndugu yetu kwani tuliona tabu ya nafsi yake alipotusihi nasi hatukusikia. Kwa hiyo taabu hii imeturudia.”
And they said one to another: 'We are verily guilty concerning our brother, in that we saw the distress of his soul, when he besought us, and we would not hear; therefore is this distress come upon us.'
22 Rubeni akawajibu, “Je sikuwambia, 'Msitende dhambi juu ya kijana,' lakini hamkusikia? Basi, tazama, damu yake inatakiwa juu yetu.”
And Reuben answered them, saying: 'Spoke I not unto you, saying: Do not sin against the child; and ye would not hear? therefore also, behold, his blood is required.'
23 Lakini hawakuja kwamba Yusufu anawaelewa, kwani kulikuwa na mkalimani kati yao.
And they knew not that Joseph understood them; for the interpreter was between them.
24 Akatoka kwao na kulia. Akarudi kwao na kuongea nao. Akamchukua Simoni miongoni mwao na kumfunga mbele ya macho yao.
And he turned himself about from them, and wept; and he returned to them, and spoke to them, and took Simeon from among them, and bound him before their eyes.
25 Kisha Yusufu akaagiza watumishi kujaza mifuko yao kwa nafaka, na kurudisha pesa ya kila mmoja katika gunia lake, nakuwapa mahitaji kwa safari. Wakatendewa hivyo.
Then Joseph commanded to fill their vessels with corn, and to restore every man's money into his sack, and to give them provision for the way; and thus was it done unto them.
26 Hawa ndugu wakapandisha chakula chao juu ya punda zao na kuondoka pale.
And they laded their asses with their corn, and departed thence.
27 Mmoja wao alipofungua gunia lake ili kumlisha punda wao katika sehemu waliyokuwa, akaona pesa yake. Tazama, ilikuwa mdomoni mwa gunia lake.
And as one of them opened his sack to give his ass provender in the lodging-place, he espied his money; and, behold, it was in the mouth of his sack.
28 Akawambia ndugu zake, “Pesa yangu imerudishwa. Tazama, imo katika gunia langu.”Mioyo yao ikazimia na wakageukiana kila mmoja huku wakitetemeka. Wakasema, “Ni nini hiki alichotutendea Mungu?”
And he said unto his brethren: 'My money is restored; and, lo, it is even in my sack.' And their heart failed them, and they turned trembling one to another, saying: 'What is this that God hath done unto us?'
29 Wakaenda kwa Yakobo, baba yao katika nchi ya Kanaani na kumwambia yote yaliyowapata.
And they came unto Jacob their father unto the land of Canaan, and told him all that had befallen them, saying:
30 Wakasema, “Yule mtu, bwana wa nchi, aliongea nasi kwa ukali na kutudhania kuwa wapelelezi katika nchi.
'The man, the lord of the land, spoke roughly with us, and took us for spies of the country.
31 Tukamwambia, 'Tu watu wa kweli sisi. Sisi siyo wapelelezi.
And we said unto him: We are upright men; we are no spies.
32 Tupo ndugu kumi na wawili, wana wa baba yetu. Mmoja hayupo hai tena, na mdogo yupo na baba yetu katika nchi ya Kanaani.”
We are twelve brethren, sons of our father; one is not, and the youngest is this day with our father in the land of Canaan.
33 Yule mtu, bwana wa nchi, akatwambia, 'Kwa hili nitajua kwamba ni watu wa kweli ninyi. Mwacheni mmojawapo wa ndugu zenu, chukueni chakula kwa ajili ya njaa katika nyumba zenu, na mwondoke.
And the man, the lord of the land, said unto us: Hereby shall I know that ye are upright men: leave one of your brethren with me, and take corn for the famine of your houses, and go your way.
34 Mleteni mdogo wenu kwangu. Ndipo nitakapojua kwamba ninyi si wapelelezi, lakini ni watu wa kweli. Kisha nitamwachilia ndugu yenu, na mtafanya biashara katika nchi.”
And bring your youngest brother unto me; then shall I know that ye are no spies, but that ye are upright men; so will I deliver you your brother, and ye shall traffic in the land.'
35 Ikawa walipoyafungua magunia yao, na tazama, kila mfuko wa fedha wa mmojawao ulikuwa katika gunia lake. Wakati wao na baba yao walipoona mifuko yao ya fedha, wakaogopa.
And it came to pass as they emptied their sacks, that, behold, every man's bundle of money was in his sack; and when they and their father saw their bundles of money, they were afraid.
36 Yakobo baba yao akawambia, “Mmeniharibia watoto wao. Yusufu hayupo hai tena, Simoni ameondoka, nanyi mmpeleke Benjamini naye. Mambo haya yote ni kunyume changu.”
And Jacob their father said unto them: 'Me have ye bereaved of my children: Joseph is not, and Simeon is not, and ye will take Benjamin away; upon me are all these things come.'
37 Rubeni akamwambia baba yake, kusema, “Unaweza kuwaua wanangu wawili nisipomrudisha Benjamini kwako. Mweke mikononi mwangu, nami nitamrudisha tena kwako.”
And Reuben spoke unto his father, saying: 'Thou shalt slay my two sons, if I bring him not to thee; deliver him into my hand, and I will bring him back to thee.'
38 Yakobo akasema, “Mwanangu atashuka pamoja nanyi. Kwani ndugu yake amekufa na yeye peke yake amebaki. Ikiwa madhara yatampata katika njia mnayoiendea, ndipo mtakapozishusha mvi zangu kaburini kwa huzuni.” (Sheol h7585)
And he said: 'My son shall not go down with you; for his brother is dead, and he only is left; if harm befall him by the way in which ye go, then will ye bring down my gray hairs with sorrow to the grave. (Sheol h7585)

< Mwanzo 42 >