< Mwanzo 37 >

1 Yakobo akaishi katika nchi aliyokaa babaye, katika nchi ya Kanaani.
And Jacob dwelleth in the land of his father's sojournings — in the land of Canaan.
2 Haya ndiyo matukio yaliyomhusu Yakobo. Yusufu, aliyekuwa kijana wa miaka kumi na saba, alikuwa akilichunga kundi pamoja na ndugu zake. Alikuwa pamoja na wana wa Bilha na pamoja na wana wa Zilpa, wake wa baba yake. Yusufu akaleta taarifa yao mbaya kwa baba yao.
These [are] births of Jacob: Joseph, a son of seventeen years, hath been enjoying himself with his brethren among the flock, (and he [is] a youth, ) with the sons of Bilhah, and with the sons of Zilpah, his father's wives, and Joseph bringeth in an account of their evil unto their father.
3 Basi Israeli akampenda Yusufu kuliko wanawe wote kwa sababu alikuwa mwana wa uzee wake. Akamshonea vazi zuri.
And Israel hath loved Joseph more than any of his sons, for he [is] a son of his old age, and hath made for him a long coat;
4 Ndugu zake wakaona kwamba baba yao alimpenda sana kuliko ndugu zake wote. Wakamchukia na hawakuongea naye vema.
and his brethren see that their father hath loved him more than any of his brethren, and they hate him, and have not been able to speak [to] him peaceably.
5 Yusufu akaota ndoto, na akawambia ndugu zake. Wakamchukia zaidi.
And Joseph dreameth a dream, and declareth to his brethren, and they add still more to hate him.
6 Aliwambia, “Tafadhari sikilizeni ndoto hii niliyoiota.
And he saith unto them, 'Hear ye, I pray you, this dream which I have dreamed:
7 Tazama, tulikuwa tukifunga miganda ya nafaka shambani na tazama, mganda wangu ukainuka na kusimama wima, na tazama, miganda yenu ikasogea na kuuinamia mganda wangu”
that, lo, we are binding bundles in the midst of the field, and lo, my bundle hath arisen, and hath also stood up, and lo, your bundles are round about, and bow themselves to my bundle.'
8 Ndugu zake wakamwambia, “Je ni kweli utatutawala? Je utatutawala juu yetu? Hata wakamchukia zaidi kwa ajili ya ndoto zake na maneno yake.
And his brethren say to him, 'Dost thou certainly reign over us? dost thou certainly rule over us?' and they add still more to hate him, for his dreams, and for his words.
9 Akaota ndoto nyingine na kuwasimulia ndugu zake. Alisema, “Tazama, nimeota ndoto nyingine: Jua na mwezi na nyota kumi na moja ziliniinamia.”
And he dreameth yet another dream, and recounteth it to his brethren, and saith, 'Lo, I have dreamed a dream again, and lo, the sun and the moon, and eleven stars, are bowing themselves to me.'
10 Akamwambia baba yake vile vile alivyowambia ndugu zake, na baba yake akamkemea. Akamwambia, Je umeota ndoto ya namna gani hii? Je mama yako na mimi na ndugu zako kweli tutakuja kukuinamia mpaka chini?”
And he recounteth unto his father, and unto his brethren; and his father pusheth against him, and saith to him, 'What [is] this dream which thou hast dreamt? do we certainly come — I, and thy mother, and thy brethren — to bow ourselves to thee, to the earth?'
11 Ndugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akaliwema jambo hilo moyoni.
and his brethren are zealous against him, and his father hath watched the matter.
12 Ndugu zake wakaenda kulichunga kundi la baba yao huko Shekemu.
And his brethren go to feed the flock of their father in Shechem,
13 Israeli akamwambia Yusufu, 'Je ndugu zako hawalichungi kundi huko Shekemu? Njoo, nami nitakutuma kwao.” Yusufu akamwambia, “nipo tayari.”
and Israel saith unto Joseph, 'Are not thy brethren feeding in Shechem? come, and I send thee unto them;' and he saith to him, 'Here [am] I;'
14 Akamwambia, “Basi nenda, uwaone ndugu zako na kundi wanaendeleaje, na uniletee neno.” Hivyo Yakobo akamtuma kutoka katika bonde la Hebroni, na Yusufu akaenda Shekemu.
and he saith to him, 'Go, I pray thee, see the peace of thy brethren, and the peace of the flock, and bring me back word;' and he sendeth him from the valley of Hebron, and he cometh to Shechem.
15 Mtu mmoja akamwona Yusufu. Tazama, Yusufu alikuwa akizunguka kondeni. Yule mtu akamwuliza, “Unatafuta nini?”
And a man findeth him, and lo, he is wandering in the field, and the man asketh him, saying, 'What seekest thou?'
16 Yusufu akamwambia, “Nawatafuta ndugu zangu. Tafadhari, niambie, wananalichunga wapi kundi.”
and he saith, 'My brethren I am seeking, declare to me, I pray thee, where they are feeding?'
17 Yule mtu akasema, “Waliondoka mahali hapa, kwa maana niliwasikia wakisema, 'Haya twende Dothani.” Yusufu akawafuata ndugu zake na kuwaona huko Dothani.
And the man saith, 'They have journeyed from this, for I have heard some saying, Let us go to Dothan,' and Joseph goeth after his brethren, and findeth them in Dothan.
18 Wakamwona kutokea mbali, na kabla hajawakaribia, wakapanga njama ya kumwua.
And they see him from afar, even before he draweth near unto them, and they conspire against him to put him to death.
19 Ndugu zake wakaambiana wao kwa wao, “Tazama, mwotaji anakaribia.
And they say one unto another, 'Lo, this man of the dreams cometh;
20 Njoni sasa, na tumwue na kumtupa katika mojawapo ya mashimo haya. Nasi tutasema, 'Mnyama mkali amemrarua.' Nasi tutaona ndoto zake zitakuwaje.”
and now, come, and we slay him, and cast him into one of the pits, and have said, An evil beast hath devoured him; and we see what his dreams are.'
21 Rubeni alilisikia hilo na kumwokoa kutoka katika mikono yao. Alisema, “Tusiuondoe uhai wake.”
And Reuben heareth, and delivereth him out of their hand, and saith, 'Let us not smite the life;'
22 Rubeni aliwambia, “Msimwage damu. Mtupeni katika shimo hili lililopo nyikani, lakini msiweke mikono yenu juu yake” - ili kwamba aweze kumwokoa katika mikono yao na kumrudisha kwa baba yake.
and Reuben saith unto them, 'Shed no blood; cast him into this pit which [is] in the wilderness, and put not forth a hand upon him,' — in order to deliver him out of their hand, to bring him back unto his father.
23 Ikawa Yusufu alipowafikia ndugu zake, walimvua vazi lake zuri.
And it cometh to pass, when Joseph hath come unto his brethren, that they strip Joseph of his coat, the long coat which [is] upon him,
24 Wakamchukua na kumtupa shimoni. Shimo lilikuwa tupu bila maji.
and take him and cast him into the pit, and the pit [is] empty, there is no water in it.
25 Wakakaa chini kula mkate. Walipoinua macho yao na kuangalia, na, tazama, msafara wa Waishmaeli ulikuwa ukija kutoka Gileadi, pamoja na ngamia wao waliochukua viungo, malhamu na manemane. Walikuwa wakisafiri kuvichukua kuelekea Misri.
And they sit down to eat bread, and they lift up their eyes, and look, and lo, a company of Ishmaelites coming from Gilead, and their camels bearing spices, and balm, and myrrh, going to take [them] down to Egypt.
26 Yuda akawambia ndugu zake, “Ni faida gani kama tutamwua ndugu yetu na kufunika damu yake?
And Judah saith unto his brethren, 'What gain when we slay our brother, and have concealed his blood?
27 Haya, na tumwuze kwa Waishmaeli na wala tusiweke mikono yetu juu yake. Kwani yeye ni ndugu yetu, nyama yetu.” Ndugu zake wakamsikiliza.
Come, and we sell him to the Ishmaelites, and our hands are not on him, for he [is] our brother — our flesh;' and his brethren hearken.
28 Wafanyabiashara wa Kimidiani wakapita. Ndugu zake wakamwinua na kumtoa Yusufu shimoni. Wakamwuza Yusufu kwa Waishmaeli kwa vipande ishirini vya fedha. Waishmaeli wakamchukua Yusufu mpaka Misri.
And Midianite merchantmen pass by and they draw out and bring up Joseph out of the pit, and sell Joseph to the Ishmaelites for twenty silverlings, and they bring Joseph into Egypt.
29 Rubeni akarudi kwenye shimo, na, tazama, Yusufu hakuwemo shimoni. Akararua mavazi yake.
And Reuben returneth unto the pit, and lo, Joseph is not in the pit, and he rendeth his garments,
30 Akarudi kwa ndugu zake na kusema, “Kijana yuko wapi? Na mimi, je niende wapi?”
and he returneth unto his brethren, and saith, 'The lad is not, and I — whither am I going?'
31 Wakachinja mbuzi na kisha wakalichukua vazi la Yusufu na kulichovya katika damu.
And they take the coat of Joseph, and slaughter a kid of the goats, and dip the coat in the blood,
32 Kisha wakalipeleka kwa baba yao na kusema, “Tumeiona hii. Tafadhari angalia kwamba ni vazi la mwanao au hapana.”
and send the long coat, and they bring [it] in unto their father, and say, 'This have we found; discern, we pray thee, whether it [is] thy son's coat or not?'
33 “Yakobo akaitambua na kusema, “Ni nguo ya mwanangu. Mnyama wa mwitu amemrarua. Bila shaka Yusufu ameraruliwa katika vipande.
And he discerneth it, and saith, 'My son's coat! an evil beast hath devoured him; torn — torn is Joseph!'
34 Yakobo akararua mavazi yake na kuvaa mavazi ya magunia katika viuno vyake. Akaomboleza kwa ajili ya mwanawe siku nyingi.
And Jacob rendeth his raiment, and putteth sackcloth on his loins, and becometh a mourner for his son many days,
35 Wanawe na binti zake wote wakainuka na kumfariji, lakini alikataa kufarijiwa. Akasema, “Hakika nitashuka kuzimu nikimwombolezea mwanangu.” Babaye akamlilia. (Sheol h7585)
and all his sons and all his daughters rise to comfort him, and he refuseth to comfort himself, and saith, 'For — I go down mourning unto my son, to Sheol,' and his father weepeth for him. (Sheol h7585)
36 Wamidiani wakamwuza huko Misri kwa Potifa, afisa wa Farao, kepteni wa walinzi.
And the Medanites have sold him unto Egypt, to Potiphar, a eunuch of Pharaoh, head of the executioners.

< Mwanzo 37 >