< Mwanzo 36 >

1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (aliyeitwa pia Edom).
Now these are the generations of Esau (the same is Edom).
2 Esau akachukua wakeze kutoka kwa Wakanaani. Hawa walikuwa wake zake: Ada binti Eloni Mhiti; Oholibama binti Ana, mjukuu wa Zibeoni Mhivi; na
Esau took his wives of the daughters of Canaan; Adah the daughter of Elon the Hittite, and Oholibamah the daughter of Anah, the daughter of Zibeon the Hivite;
3 Basemathi, binti Ishmaeli, dada wa Nebayothi.
and Basemath Ishmael’s daughter, sister of Nebaioth.
4 Ada akamzaa Elifazi kwa Esau, na Basemathi akamzaa Reueli.
And Adah bare to Esau Eliphaz; and Basemath bare Reuel;
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu, na Kora. Hawa walikuwa wana wa Esau waliozaliwa kwake katika nchi ya Kananaani.
and Oholibamah bare Jeush, and Jalam, and Korah: these are the sons of Esau, which were born unto him in the land of Canaan.
6 Esau akawachukua wakeze, wanawe, binti zake, na watu wote wa nyumba yake, mifugo wake - wanyama wake wote, na mali yake yote, aliyokuwa amekusanya katika nchi ya Kanaani, na akaenda katika nchi iliyoko mbali kutoka kwa Yakobo nduguye.
And Esau took his wives, and his sons, and his daughters, and all the souls of his house, and his cattle, and all his beasts, and all his possessions, which he had gathered in the land of Canaan; and went into a land away from his brother Jacob.
7 Alifanya hivi kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana kwa wao kuishi pamoja. Nchi waliyokuwa wamekaa isingeweza kuwafaa kwa mifugo yao.
For their substance was too great for them to dwell together; and the land of their sojournings could not bear them because of their cattle.
8 Hivyo Esau, aliyejulikana pia kama Edomu, akakaa katika nchi ya kilima Seiri.
And Esau dwelt in mount Seir: Esau is Edom.
9 Hivi ndivyo vizazi vya Esau, babu wa Waedomu katika nchi ya mlima Seiri.
And these are the generations of Esau the father of the Edomites in mount Seir:
10 Haya yalikuwa majina ya wana wa Esau: Elifazi mwana wa Ada, mkewe Esau; Reueli mwana wa Basemathi, mkewe Esau.
these are the names of Esau’s sons; Eliphaz the son of Adah the wife of Esau, Reuel the son of Basemath the wife of Esau.
11 Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Zefo, Gatamu, na Kenazi.
And the sons of Eliphaz were Teman, Omar, Zepho, and Gatam, and Kenaz.
12 Timna, suria wa Elifazi, mwana wa Esau, akamzaa Amaleki. Hawa walikuwa wajukuu wa Ada, mkewe Esau.
And Timna was concubine to Eliphaz Esau’s son; and she bare to Eliphaz Amalek: these are the sons of Adah Esau’s wife.
13 Hawa walikuwa wana wa Reueli: Nahathi, Zera, Shama, na Miza. Hawa walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
And these are the sons of Reuel; Nahath, and Zerah, Shammah, and Mizzah: these were the sons of Basemath Esau’s wife.
14 Hawa walikuwa wana wa Oholibama, mkewe Esau, aliyekuwa binti Ana na mjukuu wa Zibeoni. Alimzalia Esau Yeushi, Yalamu, na Kora.
And these were the sons of Oholibamah the daughter of Anah, the daughter of Zibeon, Esau’s wife: and she bare to Esau Jeush, and Jalam, and Korah.
15 Hizi zilikuwa koo kati ya vizazi vya Esau: uzao wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau: Temani, Omari, Zefo, Kenazi, Kora,
These are the dukes of the sons of Esau: the sons of Eliphaz the firstborn of Esau; duke Teman, duke Omar, duke Zepho, duke Kenaz,
16 Gatamu, na Amaleki. Hivi vilikuwa vizazi vya koo kutoka kwa Elifazi katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Ada.
duke Korah, duke Gatam, duke Amalek: these are the dukes that came of Eliphaz in the land of Edom; these are the sons of Adah.
17 Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli, mwana wa Esau: Nahathi, Zera, Shama, Miza. Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
And these are the sons of Reuel Esau’s son; duke Nahath, duke Zerah, duke Shammah, duke Mizzah: these are the dukes that came of Reuel in the land of Edom; these are the sons of Basemath Esau’s wife.
18 Hizi zilikuwa koo za Oholibama, mkewe Esau: Yeushi, Yalamu, Kora. Hizi ni koo zilizotoka kwa Oholibama mkewe Esau, binti Ana.
And these are the sons of Oholibamah Esau’s wife; duke Jeush, duke Jalam, duke Korah: these are the dukes that came of Oholibamah the daughter of Anah, Esau’s wife.
19 Hawa walikuwa wana wa Esau na koo zao.
These are the sons of Esau, and these are their dukes: the same is Edom.
20 Hawa walikuwa wana wa Seiri Mhori, wenyeji wa nchi hiyo: Lotani, Shobali, Zibeoni, Ana,
These are the sons of Seir the Horite, the inhabitants of the land; Lotan and Shobal and Zibeon and Anah,
21 Dishoni, Ezeri, na Dishani. Hizi zilikuwa koo the Wahori, wenyeji wa Seiri katika nchi ya Edomu.
and Dishon and Ezer and Dishan: these are the dukes that came of the Horites, the children of Seir in the land of Edom.
22 Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemani, na Timna alikuwa dada wa Lotani.
And the children of Lotan were Hori and Hemam; and Lotan’s sister was Timna.
23 Hawa walikuwa wana wa Shobali: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo, na Onamu.
And these are the children of Shobal; Alvan and Manahath and Ebal, Shepho and Onam.
24 Hawa walikuwa wana wa Zibeoni: Aia na Ana. Huyu ndiye Ana aliyeona chemichemi za moto nyikani, alipokuwa akichunga punda wa Zibeoni babaye.
And these are the children of Zibeon; Aiah and Anah: this is Anah who found the hot springs in the wilderness, as he fed the asses of Zibeon his father.
25 Hawa walikuwa watoto wa Ana: Dishoni na Oholibama, binti Ana.
And these are the children of Anah; Dishon and Oholibamah the daughter of Anah.
26 Hawa walikuwa wana wa Dishoni: Hemdani, Eshbani, Ithrani, na Kerani.
And these are the children of Dishon; Hemdan and Eshban and Ithran and Cheran.
27 Hawa walikuwa wana wa Ezeri: Bilhani, Zaavani, na Akani.
These are the children of Ezer; Bilhan and Zaavan and Akan.
28 Hawa walikuwa wana wa Dishani: Uzi na Arani.
These are the children of Dishan; Uz and Aran.
29 Hizi zilikuwa koo za Wahori: Lotani, Shobali, Zibeoni, na Ana,
These are the dukes that came of the Horites; duke Lotan, duke Shobal, duke Zibeon, duke Anah,
30 Dishoni, Ezeri, Dishani: hizi zilikuwa koo za Wahori, kulingana na ukoo ulivyoorodheshwa katika nchi ya Seiri.
duke Dishon, duke Ezer, duke Dishan: these are the dukes that came of the Horites, according to their dukes in the land of Seir.
31 Hawa walikuwa wafalme waliomiliki katika nchi ya Edomu kabla ya mfalme yeyote kumilika juu ya Waisraeli:
And these are the kings that reigned in the land of Edom, before there reigned any king over the children of Israel.
32 Bela mwana wa Beori, alitawala huko Edomu, na jina la mji wake lilikuwa Dinhaba.
And Bela the son of Beor reigned in Edom; and the name of his city was Dinhabah.
33 Bela alipofariki, kisha Yobabu mwana wa Zera kutoka Bozra, akatawala mahali pake.
And Bela died, and Jobab the son of Zerah of Bozrah reigned in his stead.
34 Yobabu alipofariki, Hushamu aliyekuwa wa nchi ya Watemani, akatawala mahali pake.
And Jobab died, and Husham of the land of the Temanites reigned in his stead.
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi aliyewashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu, akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Avithi.
And Husham died, and Hadad the son of Bedad, who smote Midian in the field of Moab, reigned in his stead: and the name of his city was Avith.
36 Hadadi alipofariki, kisha Samla wa Masreka akatawala mahali pake.
And Hadad died, and Samlah of Masrekah reigned in his stead.
37 Samla alipofariki, kisha Shauli wa Rehobothi kando ya mto alitawala mahali pake.
And Samlah died, and Shaul of Rehoboth by the River reigned in his stead.
38 Shauli alipofariki, kisha Baali Hanani mwana wa Akbori akatawala mahali pake.
And Shaul died, and Baal-hanan the son of Achbor reigned in his stead.
39 Baali Hanani mwana wa Akbori, alipokufa, kisha Hadari akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Pau. Jina la mkewe lilikuwa Mehetabeli, binti Matredi, mjukuu wa Me Zahabu.
And Baal-hanan the son of Achbor died, and Hadar reigned in his stead: and the name of his city was Pau; and his wife’s name was Mehetabel, the daughter of Matred, the daughter of Me-zahab.
40 Haya ndiyo yalikuwa majina ya wakuu wa koo kutoka uzao wa Esau, kwa kufuata koo zao na maeneo yao, kwa majina yao: Timna, Alva, Yethethi,
And these are the names of the dukes that came of Esau, according to their families, after their places, by their names; duke Timna, duke Alvah, duke Jetheth;
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
duke Oholibamah, duke Elah, duke Pinon;
42 Kenazi, Temani, Mbza,
duke Kenaz, duke Teman, duke Mibzar;
43 Magdieli, na Iramu. Hawa walikuwa wakuu wa ukoo wa Edomu, kwa kufuata makao yao katika nchi waliyomiliki. Nao ni Esau, baba wa Waedomu.
duke Magdiel, duke Iram: these be the dukes of Edom, according to their habitations in the land of their possession. This is Esau the father of the Edomites.

< Mwanzo 36 >