< Mwanzo 36 >

1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (aliyeitwa pia Edom).
Now these are the generations of Esau (that is, Edom).
2 Esau akachukua wakeze kutoka kwa Wakanaani. Hawa walikuwa wake zake: Ada binti Eloni Mhiti; Oholibama binti Ana, mjukuu wa Zibeoni Mhivi; na
Esau took his wives from the daughters of Canaan: Adah the daughter of Elon, the Hethite; and Oholibamah the daughter of Anah, the daughter of Zibeon, the Hivite;
3 Basemathi, binti Ishmaeli, dada wa Nebayothi.
and Basemath, Ishmael's daughter, sister of Nebaioth.
4 Ada akamzaa Elifazi kwa Esau, na Basemathi akamzaa Reueli.
Adah bore to Esau Eliphaz. Basemath bore Reuel.
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu, na Kora. Hawa walikuwa wana wa Esau waliozaliwa kwake katika nchi ya Kananaani.
Oholibamah bore Jeush, and Jalam, and Korah. These are the sons of Esau, who were born to him in the land of Canaan.
6 Esau akawachukua wakeze, wanawe, binti zake, na watu wote wa nyumba yake, mifugo wake - wanyama wake wote, na mali yake yote, aliyokuwa amekusanya katika nchi ya Kanaani, na akaenda katika nchi iliyoko mbali kutoka kwa Yakobo nduguye.
Esau took his wives, his sons, his daughters, and all the people of his household, with his livestock, all his animals, and all of the property he had acquired in the land of Canaan, and went out from the land of Canaan away from the presence of his brother Jacob.
7 Alifanya hivi kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana kwa wao kuishi pamoja. Nchi waliyokuwa wamekaa isingeweza kuwafaa kwa mifugo yao.
For their possessions were too great for them to remain together, and the land in which they were traveling could not support them because of their livestock.
8 Hivyo Esau, aliyejulikana pia kama Edomu, akakaa katika nchi ya kilima Seiri.
And Esau (also known as Edom) settled in the hill country of Seir.
9 Hivi ndivyo vizazi vya Esau, babu wa Waedomu katika nchi ya mlima Seiri.
These are the generations of Esau the father of the Edomites in the hill country of Seir:
10 Haya yalikuwa majina ya wana wa Esau: Elifazi mwana wa Ada, mkewe Esau; Reueli mwana wa Basemathi, mkewe Esau.
these are the names of Esau's sons: Eliphaz, the son of Adah, the wife of Esau; and Reuel, the son of Basemath, the wife of Esau.
11 Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Zefo, Gatamu, na Kenazi.
The sons of Eliphaz were Teman, Omar, Zepho, and Gatam, and Kenaz.
12 Timna, suria wa Elifazi, mwana wa Esau, akamzaa Amaleki. Hawa walikuwa wajukuu wa Ada, mkewe Esau.
Timna was the secondary wife to Eliphaz, Esau's son; and she bore to Eliphaz Amalek. These are the sons of Adah, Esau's wife.
13 Hawa walikuwa wana wa Reueli: Nahathi, Zera, Shama, na Miza. Hawa walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
These are the sons of Reuel: Nahath, and Zerah, Shammah, and Mizzah. These were the sons of Basemath, Esau's wife.
14 Hawa walikuwa wana wa Oholibama, mkewe Esau, aliyekuwa binti Ana na mjukuu wa Zibeoni. Alimzalia Esau Yeushi, Yalamu, na Kora.
These were the sons of Oholibamah, the daughter of Anah, the daughter of Zibeon, Esau's wife: she bore to Esau Jeush, and Jalam, and Korah.
15 Hizi zilikuwa koo kati ya vizazi vya Esau: uzao wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau: Temani, Omari, Zefo, Kenazi, Kora,
These are the chiefs of the sons of Esau: the sons of Eliphaz the firstborn of Esau: chief Teman, chief Omar, chief Zepho, chief Kenaz,
16 Gatamu, na Amaleki. Hivi vilikuwa vizazi vya koo kutoka kwa Elifazi katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Ada.
chief Korah, chief Gatam, chief Amalek: these are the chiefs who came of Eliphaz in the land of Edom; these are the sons of Adah.
17 Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli, mwana wa Esau: Nahathi, Zera, Shama, Miza. Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
These are the sons of Reuel, Esau's son: chief Nahath, chief Zerah, chief Shammah, chief Mizzah: these are the chiefs of Reuel in the land of Edom; these are the sons of Basemath, Esau's wife.
18 Hizi zilikuwa koo za Oholibama, mkewe Esau: Yeushi, Yalamu, Kora. Hizi ni koo zilizotoka kwa Oholibama mkewe Esau, binti Ana.
These are the sons of Oholibamah, Esau's wife: chief Jeush, chief Jalam, chief Korah: these are the chiefs who came of Oholibamah the daughter of Anah, Esau's wife.
19 Hawa walikuwa wana wa Esau na koo zao.
These are the sons of Esau (also known as Edom), and these are their chiefs.
20 Hawa walikuwa wana wa Seiri Mhori, wenyeji wa nchi hiyo: Lotani, Shobali, Zibeoni, Ana,
These are the sons of Seir the Horite, the inhabitants of the land: Lotan, and Shobal, and Zibeon, and Anah,
21 Dishoni, Ezeri, na Dishani. Hizi zilikuwa koo the Wahori, wenyeji wa Seiri katika nchi ya Edomu.
and Dishon, and Ezer, and Dishan. These are the chiefs of the Horites, the sons of Seir in the land of Edom.
22 Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemani, na Timna alikuwa dada wa Lotani.
The sons of Lotan were Hori and Hemam. Lotan's sister was Timna.
23 Hawa walikuwa wana wa Shobali: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo, na Onamu.
These are the sons of Shobal: Alvan, and Manahath, and Ebal, Shepho, and Onam.
24 Hawa walikuwa wana wa Zibeoni: Aia na Ana. Huyu ndiye Ana aliyeona chemichemi za moto nyikani, alipokuwa akichunga punda wa Zibeoni babaye.
These are the sons of Zibeon: Aiah and Anah. This is the Anah who found the hot springs in the desert as he pastured the donkeys of his father Zibeon.
25 Hawa walikuwa watoto wa Ana: Dishoni na Oholibama, binti Ana.
These are the children of Anah: Dishon, and Oholibamah the daughter of Anah.
26 Hawa walikuwa wana wa Dishoni: Hemdani, Eshbani, Ithrani, na Kerani.
These are the children of Dishon: Hemdan, and Eshban, and Ithran, and Keran.
27 Hawa walikuwa wana wa Ezeri: Bilhani, Zaavani, na Akani.
These are the sons of Ezer: Bilhan, and Zaavan, and Akan.
28 Hawa walikuwa wana wa Dishani: Uzi na Arani.
These are the sons of Dishan: Uz and Aran.
29 Hizi zilikuwa koo za Wahori: Lotani, Shobali, Zibeoni, na Ana,
These are the chiefs of the Horites: chief Lotan, chief Shobal, chief Zibeon, chief Anah,
30 Dishoni, Ezeri, Dishani: hizi zilikuwa koo za Wahori, kulingana na ukoo ulivyoorodheshwa katika nchi ya Seiri.
chief Dishon, chief Ezer, and chief Dishan: these are the chiefs who came of the Horites, according to their chiefs in the land of Seir.
31 Hawa walikuwa wafalme waliomiliki katika nchi ya Edomu kabla ya mfalme yeyote kumilika juu ya Waisraeli:
These are the kings who reigned in the land of Edom, before any king reigned over the children of Israel.
32 Bela mwana wa Beori, alitawala huko Edomu, na jina la mji wake lilikuwa Dinhaba.
Bela the son of Beor reigned in Edom. The name of his city was Dinhabah.
33 Bela alipofariki, kisha Yobabu mwana wa Zera kutoka Bozra, akatawala mahali pake.
When Bela died, and Jobab, the son of Zerah of Bozrah reigned in his place.
34 Yobabu alipofariki, Hushamu aliyekuwa wa nchi ya Watemani, akatawala mahali pake.
And Jobab died, and Husham of the land of the Temanites reigned in his place.
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi aliyewashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu, akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Avithi.
And Husham died, and Hadad the son of Bedad who struck Midian in the field of Moab reigned in his place. The name of his city was Avith.
36 Hadadi alipofariki, kisha Samla wa Masreka akatawala mahali pake.
And Hadad died, and Samlah of Masrekah reigned in his place.
37 Samla alipofariki, kisha Shauli wa Rehobothi kando ya mto alitawala mahali pake.
And Samlah died, and Shaul of Rehoboth-on-the-River reigned in his place.
38 Shauli alipofariki, kisha Baali Hanani mwana wa Akbori akatawala mahali pake.
And Shaul died, and Baal Hanan the son of Achbor reigned in his place.
39 Baali Hanani mwana wa Akbori, alipokufa, kisha Hadari akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Pau. Jina la mkewe lilikuwa Mehetabeli, binti Matredi, mjukuu wa Me Zahabu.
And Baal Hanan the son of Achbor died, and Hadad reigned in his place. The name of his city was Pau. His wife's name was Mehetabel, the daughter of Matred, the daughter of Me-Zahab.
40 Haya ndiyo yalikuwa majina ya wakuu wa koo kutoka uzao wa Esau, kwa kufuata koo zao na maeneo yao, kwa majina yao: Timna, Alva, Yethethi,
These are the names of the chiefs who came from Esau, according to their families, according to their places, and by their names: chief Timna, chief Alvah, chief Jetheth,
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
chief Oholibamah, chief Elah, chief Pinon,
42 Kenazi, Temani, Mbza,
chief Kenaz, chief Teman, chief Mibzar,
43 Magdieli, na Iramu. Hawa walikuwa wakuu wa ukoo wa Edomu, kwa kufuata makao yao katika nchi waliyomiliki. Nao ni Esau, baba wa Waedomu.
chief Magdiel, and chief Iram. These are the chiefs of Edom, according to their settlements in the land they possessed. This is Esau the father of Edom.

< Mwanzo 36 >