< Mwanzo 35 >

1 Mungu akamwambia Yakobo, “Inuka, panda kwenda Betheli, na ukae pale. Unijengee madhabahu pale, niliyekutokea pale ulipomkimbia Esau kaka yako.”
God said to Jacob [Supplanter], “Arise, go up to Beth-el [House of God], and live there. Make there an altar to God, who appeared to you when you fled from the face of Esau [Hairy] your brother.”
2 Kisha Yakobo akawambia nyumba yake na wote aliokuwa nao, “Wekeni mbali miungu yote ya kigeni iliyo kati yenu, jitakaseni wenyewe, na kubadili mavazi yenu.
Then Jacob [Supplanter] said to his household, and to all who were with him, “Put away the foreign deities that are among you, purify yourselves, change your garments.
3 Kisha tuondoke na kwenda Betheli. Nitajenga pale madhabahu kwa Mungu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, naye amekuwa pamoja nami kila nilikokwenda.
Let us arise, and go up to Beth-el [House of God]. I will make there an altar to God, who answered me in the day of my distress, and was with me on the way which I went.”
4 Hivyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni iliyokuwa mikononi mwao, na heleni zilizokuwa katika masikio yao. Yakobo akazifukia chini ya mwaloni uliokuwa karibu na Shekemu.
They gave to Jacob [Supplanter] all the foreign deities which were in their hands, and the rings which were in their ears; and Jacob [Supplanter] hid them under the oak which was by Shechem.
5 Kwa kadili walivyo safiri, Mungu akaifanya miji yote iliyokuwa karibu nao kuhofu, hivyo watu hao hawakuwafuatia wana wa Yakobo.
They traveled, and a terror of God was on the cities that were around them, and they didn’t pursue the sons of Jacob [Supplanter].
6 Hivyo Yakobo akafika Luzu(ndiyo Betheli), ulioko katika nchi ya Kanaani, yeye na watu wote aliokuwa nao.
So Jacob [Supplanter] came to Luz (that is, Beth-el [House of God]), which is in the land of Canaan [Humbled], he and all the people who were with him.
7 Alijenge madhabahu na kuliita eneo hilo El Betheli, kwa sababu Mungu alikuwa amejifunua kwake, alipokuwa akimkimbia ndugu yake.
He built an altar there, and called the place El Beit-El [God of House of God]; because there God was revealed to him, when he fled from the face of his brother.
8 Debora, mlezi wa Rebeka, akafa. Akazikwa chini kutoka Betheli chini ya mwaloni, hivyo ikaitwa Aloni Bakuthi.
Deborah, Rebekah [Securely bound]’s nurse, died, and she was buried below Beth-el [House of God] under the oak; and its name was called Allon Bacuth.
9 Yakobo alipokuja kutoka Padani Aramu, Mungu akamtokea tena na kumbariki.
God appeared to Jacob [Supplanter] again, when he came from Paddan Aram [Elevated], and blessed him.
10 Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini jina lako halitakuwa Yakobo tena. Jina lako litakuwa Israeli.” Hivyo Mungu akamwita jina lake Israeli.
God said to him, “Your name is Jacob [Supplanter]. Your name shall not be Jacob [Supplanter] any more, but your name will be Israel [God prevails].” He named him Israel [God prevails].
11 Mungu akamwambia, “Mimi ni Mungu Mwenyezi, Uwe mwenye kuzaa na kuongezeka. Taifa na wingi wa mataifa watakujia, na wafalme watatoka miongoni mwa uzao wako.
God said to him, “I am El Shaddai [God Almighty]. Be fruitful and multiply. A nation and a company of nations will be from you, and kings will come out of your body.
12 Nchi ambayo nilimpa Ibrahimu na Isaka, nitakupa wewe. Nami nitaupa pia uzao wako baada yako nchi hii.”
The land which I gave to Abraham [Father of a multitude] and Isaac [Laughter], I will give it to you, and to your offspring after you will I give the land.”
13 Mungu akapanda kutoka mahali alipoongea naye.
God went up from him in the place where he spoke with him.
14 Yakobo akaweka nguzo katika eneo ambalo Mungu alikuwa ameongea naye, nguzo ya jiwe. Akamimina juu yake sadaka ya kinywaji na akamimina mafuta juu yake.
Jacob [Supplanter] set up a pillar in the place where he spoke with him, a pillar of stone. He poured out a drink offering on it, and poured oil on it.
15 Yakobo akaiita sehemu Mungu aliyoongea naye, Betheli
Jacob [Supplanter] called the name of the place where God spoke with him “Beth-el [House of God]”.
16 Wakaendelea na safari kutoka Betheli. Walipokuwa kitambo kabla ya kufika Efrathi, Raheli akashikwa na uchungu.
They traveled from Beth-el [House of God]. There was still some distance to come to Ephrath, and Rachel [Ewe sheep] travailed. She had hard labor.
17 Akawa na utungu mzito. Alipokuwa katika utungu mzito zaidi, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwani sasa utapata mtoto mwingine wa kiume.”
When she was in hard labor, the midwife said to her, “Don’t be afraid, for now you will have another son.”
18 Hata alipokaribia kufa, kwa pumzi yake ya mwisho akamwita jina lake Benoni, lakini baba yake akamwita jina lake Benjamini.
As her soul was departing (for she died), she named him Benoni, but his father named him Benjamin [Son of right hand, Son of south].
19 Raheli akafa na kuzikwa katika njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu).
Rachel [Ewe sheep] died, and was buried on the way to Ephrath (also called Bethlehem [House of Bread]).
20 Yakobo akaweka nguzo katika kaburi lake. Ndiyo alama ya kaburi la Raheli hata leo.
Jacob [Supplanter] set up a pillar on her grave. The same is the Pillar of Rachel [Ewe sheep]’s grave to this day.
21 Israeli akaendelea na safari na akaweka hema yake kuvuka mnara wa walinzi wa kondoo.
Israel [God prevails] traveled, and spread his tent beyond the tower of Eder.
22 Yakobo alipokuwa akiishi katika nchi hiyo, Rubeni akalala na Bilha suria wa baba yake, na Israeli akasikia kuhusu hilo. Basi Yakobo alikuwa na wana kumi na mbili.
While Israel [God prevails] lived in that land, Reuben [See, a son!] went and lay with Bilhah [Bashful], his father’s concubine, and Israel [God prevails] sh'ma ·heard obeyed· of it. Now the sons of Jacob [Supplanter] were twelve.
23 Wanawe kwa Lea walikuwa Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, na Simoni, Lawi, Yuda, Isakari, na Zabuloni.
The sons of Leah [Weary]: Reuben [See, a son!] (Jacob [Supplanter]’s firstborn), Simeon [Hearing], Levi [United with], Judah [Praised], Issachar [Hire, Reward], and Zebulun [Living together].
24 Wanawe kwa Raheli walikuwa Yusufu na Benjamini.
The sons of Rachel [Ewe sheep]: Joseph [May he add] and Benjamin [Son of right hand, Son of south].
25 Wanawe kwa Bilha, mjakazi wa Raheli walikuwa Dani na Naftali.
The sons of Bilhah [Bashful] (Rachel [Ewe sheep]’s servant): Dan [He judged] and Naphtali [My wrestling].
26 Wana wa Zilpa, mjakazi wa Lea, walikuwa Gadi na Asheri. Hawa wote walikuwa wana wa Yakobo waliozaliwa kwake huko Padani Aramu.
The sons of Zilpah [Frailty] (Leah [Weary]’s servant): Gad [Good fortune] and Asher [Happy]. These are the sons of Jacob [Supplanter], who were born to him in Paddan Aram [Elevated].
27 Yakobo akaja kwa Isaka, baba yake, huko Mamre katika Kiriathi Arba (jina sawa na Hebroni), alipoishi Ibrahimu na Isaka.
Jacob [Supplanter] came to Isaac [Laughter] his father, to Mamre [Bitter, Fatness], to Kiriath Arba (which is Hebron), where Abraham [Father of a multitude] and Isaac [Laughter] lived as foreigners.
28 Isaka akaishi miaka mia moja na themanini.
The days of Isaac [Laughter] were one hundred eighty years.
29 Isaka akapumua pumzi yake ya mwisho na akafa, na akakusanywa kwa wahenga wake, na mtu mzee amejaa siku. Esau na Yakobo, wanawe, wakamzika.
Isaac [Laughter] gave up the spirit, and died, and was gathered to his people, old and full of days. Esau [Hairy] and Jacob [Supplanter], his sons, buried him.

< Mwanzo 35 >