< Mwanzo 35 >

1 Mungu akamwambia Yakobo, “Inuka, panda kwenda Betheli, na ukae pale. Unijengee madhabahu pale, niliyekutokea pale ulipomkimbia Esau kaka yako.”
And God said unto Jacob: 'Arise, go up to Beth-el, and dwell there; and make there an altar unto God, who appeared unto thee when thou didst flee from the face of Esau thy brother.'
2 Kisha Yakobo akawambia nyumba yake na wote aliokuwa nao, “Wekeni mbali miungu yote ya kigeni iliyo kati yenu, jitakaseni wenyewe, na kubadili mavazi yenu.
Then Jacob said unto his household, and to all that were with him: 'Put away the strange gods that are among you, and purify yourselves, and change your garments;
3 Kisha tuondoke na kwenda Betheli. Nitajenga pale madhabahu kwa Mungu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, naye amekuwa pamoja nami kila nilikokwenda.
and let us arise, and go up to Beth-el; and I will make there an altar unto God, who answered me in the day of my distress, and was with me in the way which I went.'
4 Hivyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni iliyokuwa mikononi mwao, na heleni zilizokuwa katika masikio yao. Yakobo akazifukia chini ya mwaloni uliokuwa karibu na Shekemu.
And they gave unto Jacob all the foreign gods which were in their hand, and the rings which were in their ears; and Jacob hid them under the terebinth which was by Shechem.
5 Kwa kadili walivyo safiri, Mungu akaifanya miji yote iliyokuwa karibu nao kuhofu, hivyo watu hao hawakuwafuatia wana wa Yakobo.
And they journeyed; and a terror of God was upon the cities that were round about them, and they did not pursue after the sons of Jacob.
6 Hivyo Yakobo akafika Luzu(ndiyo Betheli), ulioko katika nchi ya Kanaani, yeye na watu wote aliokuwa nao.
So Jacob came to Luz, which is in the land of Canaan — the same is Beth-el — he and all the people that were with him.
7 Alijenge madhabahu na kuliita eneo hilo El Betheli, kwa sababu Mungu alikuwa amejifunua kwake, alipokuwa akimkimbia ndugu yake.
And he built there an altar, and called the place El-beth-el, because there God was revealed unto him, when he fled from the face of his brother.
8 Debora, mlezi wa Rebeka, akafa. Akazikwa chini kutoka Betheli chini ya mwaloni, hivyo ikaitwa Aloni Bakuthi.
And Deborah Rebekah's nurse died, and she was buried below Beth-el under the oak; and the name of it was called Allon-bacuth.
9 Yakobo alipokuja kutoka Padani Aramu, Mungu akamtokea tena na kumbariki.
And God appeared unto Jacob again, when he came from Paddan-aram, and blessed him.
10 Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini jina lako halitakuwa Yakobo tena. Jina lako litakuwa Israeli.” Hivyo Mungu akamwita jina lake Israeli.
And God said unto him: 'Thy name is Jacob: thy name shall not be called any more Jacob, but Israel shall be thy name'; and He called his name Israel.
11 Mungu akamwambia, “Mimi ni Mungu Mwenyezi, Uwe mwenye kuzaa na kuongezeka. Taifa na wingi wa mataifa watakujia, na wafalme watatoka miongoni mwa uzao wako.
And God said unto him: 'I am God Almighty. Be fruitful and multiply; a nation and a company of nations shall be of thee, and kings shall come out of thy loins;
12 Nchi ambayo nilimpa Ibrahimu na Isaka, nitakupa wewe. Nami nitaupa pia uzao wako baada yako nchi hii.”
and the land which I gave unto Abraham and Isaac, to thee I will give it, and to thy seed after thee will I give the land.'
13 Mungu akapanda kutoka mahali alipoongea naye.
And God went up from him in the place where He spoke with him.
14 Yakobo akaweka nguzo katika eneo ambalo Mungu alikuwa ameongea naye, nguzo ya jiwe. Akamimina juu yake sadaka ya kinywaji na akamimina mafuta juu yake.
And Jacob set up a pillar in the place where He spoke with him, a pillar of stone, and he poured out a drink-offering thereon, and poured oil thereon.
15 Yakobo akaiita sehemu Mungu aliyoongea naye, Betheli
And Jacob called the name of the place where God spoke with him, Beth-el.
16 Wakaendelea na safari kutoka Betheli. Walipokuwa kitambo kabla ya kufika Efrathi, Raheli akashikwa na uchungu.
And they journeyed from Beth-el; and there was still some way to come to Ephrath; and Rachel travailed, and she had hard labour.
17 Akawa na utungu mzito. Alipokuwa katika utungu mzito zaidi, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwani sasa utapata mtoto mwingine wa kiume.”
And it came to pass, when she was in hard labour, that the mid-wife said unto her: 'Fear not; for this also is a son for thee.'
18 Hata alipokaribia kufa, kwa pumzi yake ya mwisho akamwita jina lake Benoni, lakini baba yake akamwita jina lake Benjamini.
And it came to pass, as her soul was in departing — for she died — that she called his name Ben-oni; but his father called him Benjamin.
19 Raheli akafa na kuzikwa katika njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu).
And Rachel died, and was buried in the way to Ephrath — the same is Beth-lehem.
20 Yakobo akaweka nguzo katika kaburi lake. Ndiyo alama ya kaburi la Raheli hata leo.
And Jacob set up a pillar upon her grave; the same is the pillar of Rachel's grave unto this day.
21 Israeli akaendelea na safari na akaweka hema yake kuvuka mnara wa walinzi wa kondoo.
And Israel journeyed, and spread his tent beyond Migdal-eder.
22 Yakobo alipokuwa akiishi katika nchi hiyo, Rubeni akalala na Bilha suria wa baba yake, na Israeli akasikia kuhusu hilo. Basi Yakobo alikuwa na wana kumi na mbili.
And it came to pass, while Israel dwelt in that land, that Reuben went and lay with Bilhah his father's concubine; and Israel heard of it. Now the sons of Jacob were twelve:
23 Wanawe kwa Lea walikuwa Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, na Simoni, Lawi, Yuda, Isakari, na Zabuloni.
the sons of Leah: Reuben, Jacob's first-born, and Simeon, and Levi, and Judah, and Issachar, and Zebulun;
24 Wanawe kwa Raheli walikuwa Yusufu na Benjamini.
the sons of Rachel: Joseph and Benjamin;
25 Wanawe kwa Bilha, mjakazi wa Raheli walikuwa Dani na Naftali.
and the sons of Bilhah, Rachel's handmaid: Dan and Naphtali;
26 Wana wa Zilpa, mjakazi wa Lea, walikuwa Gadi na Asheri. Hawa wote walikuwa wana wa Yakobo waliozaliwa kwake huko Padani Aramu.
and the sons of Zilpah, Leah's handmaid: Gad and Asher. These are the sons of Jacob, that were born to him in Paddan-aram.
27 Yakobo akaja kwa Isaka, baba yake, huko Mamre katika Kiriathi Arba (jina sawa na Hebroni), alipoishi Ibrahimu na Isaka.
And Jacob came unto Isaac his father to Mamre, to Kiriatharba — the same is Hebron — where Abraham and Isaac sojourned.
28 Isaka akaishi miaka mia moja na themanini.
And the days of Isaac were a hundred and fourscore years.
29 Isaka akapumua pumzi yake ya mwisho na akafa, na akakusanywa kwa wahenga wake, na mtu mzee amejaa siku. Esau na Yakobo, wanawe, wakamzika.
And Isaac expired, and died, and was gathered unto his people, old and full of days; and Esau and Jacob his sons buried him.

< Mwanzo 35 >