< Mwanzo 29 >

1 Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika katika nchi ya watu wa mashariki.
Тогава Яков тръгна и отиде в земята на източните жители.
2 Hata alipotazama, akaona kisima kondeni, na, tazama, makundi matatu ya kondoo yalikuwa yamelala kando yake. Kwani kutoka katika hicho wangeyanywesha makundi, na jiwe juu ya mdomo wa kisima lilikuwa kubwa.
И погледна, и, ето, кладенец на полето, и там три стада овци, които почиваха при него, защото от оня кладенец напояваха стадата; и върху отвора на кладенеца имаше голям камък.
3 Wakati makundi yote yangekusanyika pale, wachungaji wangevingirisha jiwe kutoka katika mdomo wa kisima na kuwanywesha kondoo, na kisha kurudisha jiwe juu ya mdomo wa kisima, mahali pake.
И когато се събираха там всичките стада, отваляха камъка от отвора на кладенеца, та напояваха стадата; после пак туряха камъка на мястото му над отвора на кладенеца.
4 Yakobo akawambia, “Ndugu zangu, ninyi mnatokea wapi?” nao wakasema, “Tunatoka Harani.”
И Яков каза на овчарите: Братя, от где сте? А те рекоха: От Харан сме.
5 Akawambia, “Mnamfahamu Labani mwana wa Nahori?” Wakasema, “Tunamfahamu.”
И рече им: Познавате ли Лавана, Нахоровия син? Отговориха: Познаваме.
6 Akawambia, “Je hajambo?” Wakasema, “Hajambo, na, tazama pale, Raheli binti yake anakuja na kondoo.”
И рече им: Здрав ли е? А те рекоха: Здрав е; и ето дъщеря му Рахил иде с те.
7 Yakobo akasema, “Tazama, ni mchana. Siyo wakati wa kukusanya kondoo pamoja. Mnapaswa kuwanywesha kondoo na kisha mkaenda na kuwaacha wachunge.”
А той каза: Вижте, още е много рано, не е време да се прибира добитъкът; напойте те и идете да ги пасете.
8 Wakamwambia, “Hatuwezi kuwanywesha mpaka makundi yote yakusanyike pamoja. Ndipo wanaume watakapovingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na ndipo tutakapowanywesha kondoo.”
А те рекоха: Не можем догде не се съберат всичките стада и не отвалят камъка от отвора на кладенеца; тогава напояваме овците.
9 Wakati bado Yakobo anaongea nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa babaye, kwani alikuwa akiwachunga.
Докато им говореше още, дойде Рахил с бащините си, защото тя ги пасеше.
10 Yakobo alipomwona Raheli, binti wa Labani, kaka wa mamaye, na kondoo wa Labani, kaka wa mama yake, Yakobo akaja juu, akalivingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na akawanywesha kondoo wa Labani, kaka wa mama yake.
А като видя Яков Рахил, дъщерята на вуйка си Лавана, и овците на вуйка си Лавана, Яков се приближи, та отвали камъка от отвора на кладенеца; и напои стадото на вуйка си Лавана.
11 Yakobo akambusu Raheli na akalia kwa sauti.
И Яков целуна Рахил и заплака с висок глас.
12 Yakobo akamwambia Raheli kwamba alikuwa ni ndugu wa baba yake, na kwamba alikuwa mwana wa Rebeka. Kisha yeye akakimbia kumwambia baba yake.
И Яков каза на Рахил, че е брат на баща й и, че е син на Ревека; а тя се завтече, та извести на баща си.
13 Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo mwana wa dada yake, akaenda kukutana naye, akamkumbatia, akambusu, na kumleta nyumbani kwake. Yakobo akamwambia Labani mambo haya yote.
А Лаван, като чу за своя сестриник Яков, завтече се да го посрещне; и прегърна го, целуна го и го заведе у дома си. Тогава Яков разказа на Лавана всичко.
14 Labani akamwambia, “Kwa hakika wewe ni mfupa wangu na nyama yangu.” Kisha Yakobo akakaa naye kama mwezi mmoja.
И Лаван му рече: Наистина, ти си моя кост и моя плът. И Яков живя при него един месец.
15 Kisha Labani akamwambia Yakobo, “Je unitumikie bure kwa kuwa wewe ni ndugu yangu? Niambie, ujira wako utakuwaje?
След това Лаван рече на Якова: Нима, като си ми брат, ти ще ми работиш безплатно? Кажи ми, каква да ти бъде заплатата?
16 Basi Labani alikuwa na binti wawili. Jina la mkubwa lilikuwa ni Lea, na jina la mdogo lilikuwa Raheli.
А Лаван имаше две дъщери: името на по-старата беше Лия, а името на по-младата - Рахил.
17 Macho ya Lea yalikuwa dhaifu, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo na mwonekano.
На Лия очите не бяха здрави; а Рахил имаше хубава снага и хубаво лице.
18 Yakobo alimpenda Raheli, hivyo akasema, “Nitakutumikia miaka saba kwa ajili ya Raheli, binti yako mdogo.”
И Яков, понеже обикна Рахил, рече: Ще ти работя седем години за по-малката ти дъщеря, Рахил.
19 Labani akasema, Itakuwa vema kukupa wewe, kuliko kumpa mtu mwingine. Kaa nami.”
И рече Лаван: По-добре да я дам на тебе, отколкото да я дам на друг мъж; живей при мене.
20 Hivyo Yakobo akamtumikia kwa miaka saba kwa ajili ya Raheli; nayo ilionekana kwake kama siku chache tu, kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake.
И тъй, Яков работи за Рахил седем години; но, поради любовта му към нея, те му се видяха като няколко дни.
21 Kisha Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu, kwani siku zangu zimetimia - ili kwamba nimwoe!
След това Яков каза на Лавана: Дай жена ми, защото дойде вече време да вляза при нея.
22 Hivyo Labani akawaalika watu wa mahali hapo na kuandaa sherehe.
И тъй, Лаван събра всичките хора от това място и даде угощение.
23 Wakati wa jioni, Labani akamchukua Lea binti yake mkubwa na kumleta kwa Yakobo, aliyelala naye.
А вечерта взе дъщеря си Лия, та му я доведе; и той влезе при нея.
24 Labani akampa mtumishi wake wakike Zilpa kuwa mjakazi wa Lea.
И Лаван даде слугинята си Зелфа за слугиня на дъщеря си Лия.
25 Ilipofika asubuhi, tazama, kumbe ni Lea! Yakobo akamwambia Labani, “Ni nini hiki ulichonifanyia? Je sikukutumikia kwa ajili ya Raheli? Kwa nini basi umenihadaa?
Но на сутринта, ето, че беше Лия. И Яков рече на Лавана: Що е това, което ми стори ти? Нали за Рахил ти работих? Тогава защо ме излъга?
26 Labani akamwambia, “Siyo utamaduni wetu kumtoa bindi mdogo kabla ya mzaliwa wa kwanza.
А Лаван каза: В нашето място няма обичай да се дава по-младата преди по-старата.
27 Timiza juma la bibi arusi, na tutakupa yule mwingine pia kwa mbadala wa kunitumikia miaka mingine saba.”
Свърши сватбарската седмица с тая; и ще ти дам и оная за работата, която ще ми вършиш още седем години.
28 Yakobo akafanya hivyo, na akatimiza juma la Lea. Kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
И Яков стори така; свърши седмицата с Лия и тогава Лаван му даде дъщеря си Рахил за жена.
29 Lakini pia Labani akampa Raheli binti yake Bilha, kuwa mjakazi wake.
И Лаван даде слугинята си Вала за слугиня на дъщеря си Рахил.
30 Hivyo Yakobo akalala na Raheli, pia, lakini akampenda Raheli zaidi ya Lea. Hivyo Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka saba mingine.
И Яков влезе при Рахил, и обикна Рахил повече от Лия; и работи на Лаван още седем години.
31 Yahwe akaona kwamba Lea hakupendwa, hivyo akalifungua tumbo lake, lakini Raheli hakuwa na mtoto.
А Господ, понеже видя, че Лия не беше обичана, отвори утробата й; а Рахил беше бездетна.
32 Lea akashika mimba na kuzaa mwana, naye akamwita Rubeni. Kwani alisema, “Kwa sababu Yahwe ameliangalia teso langu; bila shaka mme wangu sasa atanipenda.”
И тъй, Лия зачна и роди син, и наименува го Рувим, защото си думаше: Господ погледна на неволята ми; сега мъжът ми ще обикне.
33 Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Kwa sababu Yahwe amesikia kwamba sipendwi, kwa hiyo amenipa mwana mwingine,” na akamwita Simoni.
И пак зачна и роди син; и рече: Понеже чу Господ, че не съм любима, затова ми даде и тоя син; и наименува го Симеон.
34 Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu mme wangu ataungana nami, kwa kuwa nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akaitwa Lawi.
Пак зачна и роди син; и рече: Сега вече мъжът ми ще се привърже към мене, защото му родих три сина; затова го наименува Левий
35 Akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu nitamsifu Yahwe.” Kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; kisha akaacha kuzaa watoto.
И пак зачна и роди син; и рече: Тоя път ще възхваля Господа; затова го наименува Юда. И престана да ражда.

< Mwanzo 29 >