< Mwanzo 2 >

1 Kisha mbingu na nchi zilimalizika, na viumbe hai vyote vilivyo jaza mbingu na nchi.
Tak ukończone zostały niebiosa i ziemia oraz wszystkie ich zastępy.
2 Siku ya saba Mungu alifikia mwisho wa kazi yake ambayo aliifanya, na kwa hiyo alipumzika siku ya saba kutoka kwenye kazi yake yote.
W siódmym dniu Bóg ukończył swe dzieło, które uczynił; i odpoczął siódmego dnia od wszelkiego swego dzieła, które stworzył.
3 Mungu akaibarikia siku ya saba na akaitakasa, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kwenye kazi yake yote ambayo aliifanya katika uumbaji.
I Bóg błogosławił siódmy dzień, i poświęcił go, bo w nim odpoczął od wszelkiego swego dzieła, które Bóg stworzył i uczynił.
4 Haya yalikuwa ni matukio yahusuyo mbingu na nchi, wakati vilipoumbwa, katika siku ambayo Yahwe Mungu aliumba nchi na mbingu.
Takie [są] dzieje stworzenia niebios i ziemi w dniu, w którym PAN Bóg uczynił ziemię i niebiosa;
5 Hapakuwa na msitu wa shambani uliokuwa katika nchi, na hapakuwa na mmea wa shambani uliokuwa umechipuka, kwa kuwa Yahwe Mungu alikuwa hajasababisha mvua kunyesha juu ya nchi, na hapakuwa na mtu wa kulima ardhi.
Wszelkie krzewy polne, zanim były na ziemi, i wszelkie rośliny polne, nim wzeszły. Bo PAN Bóg [jeszcze] nie spuścił deszczu na ziemię i nie było człowieka, który by uprawiał ziemię.
6 Lakini ukungu uliinuka juu kutoka kwenye nchi na kuutia maji uso wote wa ardhi.
Ale z ziemi wychodziła para, która nawilżała całą powierzchnię ziemi.
7 Yahwe Mungu aliumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi, na akampulizia puani pumzi ya uhai, na mtu akawa kiumbe hai.
Wtedy PAN Bóg ukształtował człowieka z prochu ziemi i tchnął w jego nozdrza tchnienie życia. I człowiek stał się żywą duszą.
8 Yahwe Mungu aliotesha bustani upande wa mashariki, katika Edeni, na pale akamuweka mtu ambaye alimuumba.
PAN Bóg zasadził też ogród w Edenie, na wschodzie, i umieścił tam człowieka, którego ukształtował.
9 Kutoka ardhini Yahwe Mungu alifanya kila mti uote ambao unapendeza na ni mzuri kwa chakula. Hii ni pamoja na mti wa uzima ambao ulikuwa katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
I wywiódł PAN Bóg z ziemi wszelkie drzewa miłe dla oka i których [owoce] były dobre do jedzenia oraz drzewo życia pośrodku ogrodu i drzewo poznania dobra i zła.
10 Mto ukatoka nje ya Edeni kuitia maji bustani. Na kutoka pale ukagawanyika na kuwa mito minne.
A z Edenu wypływała rzeka, aby nawadniać ogród; i stamtąd dzieliła się na cztery główne [rzeki].
11 Jina la ule wa kwanza ni Pishoni. Huu ni ule ambao unatiririka kupitia nchi yote ya Havila, ambapo kuna dhahabu.
Nazwa pierwszej – Piszon; to ta, która okrąża całą ziemię Chawila, gdzie [znajduje się] złoto.
12 Dhahabu ya inchi ile ni nzuri. pia kuna bedola na jiwe shohamu.
A złoto tej ziemi [jest] wyborne. Tam też jest bdellium i kamień onyksowy.
13 Jina la mto wa pili ni Gihoni. Huu unatiririka kupitia nchi yote ya kushi.
Nazwa drugiej rzeki – Gichon; ta okrąża całą ziemię Kusz.
14 Jina la mto wa tatu ni Hidekeli, ambao unatiririka mashariki mwa Ashuru. Mto wa nne ni Frati.
Nazwa zaś trzeciej rzeki – Chiddekel; płynie ona na wschód ku Asyrii. A czwarta rzeka to Eufrat.
15 Yahwe Mungu alimtwaa mtu na kumweka ndani ya bustani ya Edeni kuilima na kuitunza.
PAN Bóg wziął więc człowieka i umieścił go w ogrodzie Eden, aby go uprawiał i strzegł.
16 Yahwe Mungu alimuagiza mtu akisema, “kutoka kwenye kila mti bustanini waweza kula kwa uhuru.
I rozkazał PAN Bóg człowiekowi: Możesz jeść do woli z każdego drzewa ogrodu;
17 Lakini kutoka kwenye mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa kuwa siku utakayo kula kutoka katika mti huo, utakufa hakika.”
Ale z drzewa poznania dobra i zła jeść nie będziesz, bo tego dnia, kiedy zjesz z niego, na pewno umrzesz.
18 Kisha Yahwe Mungu akasema, “siyo jambo jema kwamba mtu huyu lazima awe pekeyake. Nitamfanyia msaidizi anaye mfaa.”
PAN Bóg powiedział też: Niedobrze, by człowiek był sam; uczynię mu odpowiednią dla niego pomoc.
19 Kutoka ardhini Yahwe Mungu akafanya kila mnyama wa kondeni na kila ndege wa angani. Kisha akawaleta kwa mtu huyu aone angewapatia majina gani. Jina ambalo mtu huyu alimwita kila kiumbe hai, hili ndilo lilikuwa jina lake.
I ukształtował PAN Bóg z ziemi wszelkie zwierzęta polne i wszelkie ptactwo niebieskie, i przyprowadził [je] do Adama, aby zobaczyć, jak je nazwie; a jak Adam nazwał każdą istotę żywą, [taka] była jej nazwa.
20 Mtu huyu akawapatia majina wanyama wote, ndege wote wa angani, na kila mnyama wa mwitu. Lakini kwa mtu mwenyewe hapakuwa na msaidizi wa kumfaa yeye.
I Adam nadał nazwy wszelkiemu bydłu i ptactwu niebieskiemu, i wszelkim zwierzętom polnym. Dla Adama jednak nie znalazła się pomoc odpowiednia dla niego.
21 Yahwe Mungu akaleta usingizi mzito kwa mtu huyu, kwa hiyo mtu huyu akalala. Yahwe Mungu akatwaa moja ya mbavu za mtu huyu na akapafunika pale alipo chukua ubavu.
Wtedy PAN Bóg zesłał głęboki sen na Adama; a gdy zasnął, wyjął jedno z jego żeber i zapełnił ciałem miejsce po nim.
22 Kwa ubavu ambao Yahwe Mungu alichukua toka kwa mtu huyu, akafanya mwanamke na akamleta kwa mtu huyu.
I z tego żebra, które PAN Bóg wyjął z Adama, utworzył kobietę i przyprowadził ją do Adama.
23 Mwanaume akasema, “kwa sasa, huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu. ataitwa 'mwanamke,' kwa sababu ametwaliwa katika mwanaume.
I Adam powiedział: To [teraz jest] kość z moich kości i ciało z mojego ciała; dlatego będzie nazwana kobietą, bo z mężczyzny została wzięta.
24 Kwa hiyo mwanaume atawaacha baba yake na mama yake, ataungamanika na mke wake, na watakuwa mwili mmoja.
Dlatego opuści mężczyzna swojego ojca i swoją matkę i połączy się ze swoją żoną, i będą jednym ciałem.
25 Wote wawili walikuwa uchi, mwanaume na mke wake, lakini hawakuona aibu.
I oboje, Adam i jego żona, byli nadzy, a nie wstydzili się.

< Mwanzo 2 >