< Mwanzo 2 >

1 Kisha mbingu na nchi zilimalizika, na viumbe hai vyote vilivyo jaza mbingu na nchi.
Then the heavens and the earth were finished, and all the living things that filled them.
2 Siku ya saba Mungu alifikia mwisho wa kazi yake ambayo aliifanya, na kwa hiyo alipumzika siku ya saba kutoka kwenye kazi yake yote.
On the seventh day God came to the end of his work which he had done, and so he rested on the seventh day from all his work.
3 Mungu akaibarikia siku ya saba na akaitakasa, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kwenye kazi yake yote ambayo aliifanya katika uumbaji.
God blessed the seventh day and sanctified it, because in it he rested from all his work which he had done in his creation.
4 Haya yalikuwa ni matukio yahusuyo mbingu na nchi, wakati vilipoumbwa, katika siku ambayo Yahwe Mungu aliumba nchi na mbingu.
These were the events concerning the heavens and the earth, when they were created, on the day that Yahweh God made the earth and the heavens.
5 Hapakuwa na msitu wa shambani uliokuwa katika nchi, na hapakuwa na mmea wa shambani uliokuwa umechipuka, kwa kuwa Yahwe Mungu alikuwa hajasababisha mvua kunyesha juu ya nchi, na hapakuwa na mtu wa kulima ardhi.
No bush of the field was yet in the earth, and no plant of the field had yet sprouted, for Yahweh God had not caused it to rain upon the earth, and there was no man to cultivate the ground.
6 Lakini ukungu uliinuka juu kutoka kwenye nchi na kuutia maji uso wote wa ardhi.
But a mist went up from the earth and watered the whole surface of the ground.
7 Yahwe Mungu aliumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi, na akampulizia puani pumzi ya uhai, na mtu akawa kiumbe hai.
Yahweh God formed man from the dust of the ground, and breathed into his nostrils the breath of life, and man became a living being.
8 Yahwe Mungu aliotesha bustani upande wa mashariki, katika Edeni, na pale akamuweka mtu ambaye alimuumba.
Yahweh God planted a garden eastward, in Eden, and there he put the man whom he had formed.
9 Kutoka ardhini Yahwe Mungu alifanya kila mti uote ambao unapendeza na ni mzuri kwa chakula. Hii ni pamoja na mti wa uzima ambao ulikuwa katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
Out of the ground Yahweh God made every tree to grow that is pleasant to the sight and good for food. This included the tree of life that was in the midst of the garden, and the tree of the knowledge of good and evil.
10 Mto ukatoka nje ya Edeni kuitia maji bustani. Na kutoka pale ukagawanyika na kuwa mito minne.
A river went out of Eden to water the garden. From there it divided and became four rivers.
11 Jina la ule wa kwanza ni Pishoni. Huu ni ule ambao unatiririka kupitia nchi yote ya Havila, ambapo kuna dhahabu.
The name of the first is Pishon. It is the one which flows throughout the whole land of Havilah, where there is gold.
12 Dhahabu ya inchi ile ni nzuri. pia kuna bedola na jiwe shohamu.
The gold of that land is good. There are also bdellium and the onyx stone.
13 Jina la mto wa pili ni Gihoni. Huu unatiririka kupitia nchi yote ya kushi.
The name of the second river is Gihon. This one flows throughout the whole land of Cush.
14 Jina la mto wa tatu ni Hidekeli, ambao unatiririka mashariki mwa Ashuru. Mto wa nne ni Frati.
The name of the third river is Tigris, which flows east of Ashur. The fourth river is the Euphrates.
15 Yahwe Mungu alimtwaa mtu na kumweka ndani ya bustani ya Edeni kuilima na kuitunza.
Yahweh God took the man and put him into the garden of Eden to work it and to maintain it.
16 Yahwe Mungu alimuagiza mtu akisema, “kutoka kwenye kila mti bustanini waweza kula kwa uhuru.
Yahweh God commanded the man, saying, “From every tree in the garden you may freely eat.
17 Lakini kutoka kwenye mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa kuwa siku utakayo kula kutoka katika mti huo, utakufa hakika.”
But from the tree of the knowledge of good and evil you may not eat, for on the day that you eat from it, you will surely die.”
18 Kisha Yahwe Mungu akasema, “siyo jambo jema kwamba mtu huyu lazima awe pekeyake. Nitamfanyia msaidizi anaye mfaa.”
Then Yahweh God said, “It is not good that the man should be alone. I will make him a helper suitable for him.”
19 Kutoka ardhini Yahwe Mungu akafanya kila mnyama wa kondeni na kila ndege wa angani. Kisha akawaleta kwa mtu huyu aone angewapatia majina gani. Jina ambalo mtu huyu alimwita kila kiumbe hai, hili ndilo lilikuwa jina lake.
Out of the ground Yahweh God formed every animal of the field and every bird of the sky. Then he brought them to the man to see what he would call them. Whatever the man called each living creature, that was its name.
20 Mtu huyu akawapatia majina wanyama wote, ndege wote wa angani, na kila mnyama wa mwitu. Lakini kwa mtu mwenyewe hapakuwa na msaidizi wa kumfaa yeye.
The man gave names to all the livestock, to all the birds of the sky, and to every beast of the field. But for the man himself there was found no helper suitable for him.
21 Yahwe Mungu akaleta usingizi mzito kwa mtu huyu, kwa hiyo mtu huyu akalala. Yahwe Mungu akatwaa moja ya mbavu za mtu huyu na akapafunika pale alipo chukua ubavu.
Yahweh God caused a deep sleep to fall upon the man, so the man slept. Yahweh God took one of his ribs and closed up the flesh where he took the rib.
22 Kwa ubavu ambao Yahwe Mungu alichukua toka kwa mtu huyu, akafanya mwanamke na akamleta kwa mtu huyu.
With the rib that Yahweh God had taken from the man, he made a woman and brought her to the man.
23 Mwanaume akasema, “kwa sasa, huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu. ataitwa 'mwanamke,' kwa sababu ametwaliwa katika mwanaume.
The man said, “This time, this one is bone of my bones, and flesh of my flesh. She will be called 'woman,' because she was taken out of man.”
24 Kwa hiyo mwanaume atawaacha baba yake na mama yake, ataungamanika na mke wake, na watakuwa mwili mmoja.
Therefore a man will leave his father and his mother, he will be united to his wife, and they will become one flesh.
25 Wote wawili walikuwa uchi, mwanaume na mke wake, lakini hawakuona aibu.
They were both naked, the man and his wife, but were not ashamed.

< Mwanzo 2 >