< Mwanzo 2 >

1 Kisha mbingu na nchi zilimalizika, na viumbe hai vyote vilivyo jaza mbingu na nchi.
And the heaven and the earth were finished, and all the host of them.
2 Siku ya saba Mungu alifikia mwisho wa kazi yake ambayo aliifanya, na kwa hiyo alipumzika siku ya saba kutoka kwenye kazi yake yote.
And on the seventh day God finished His work which He had made; and He rested on the seventh day from all His work which He had made.
3 Mungu akaibarikia siku ya saba na akaitakasa, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kwenye kazi yake yote ambayo aliifanya katika uumbaji.
And God blessed the seventh day, and hallowed it; because that in it He rested from all His work which God in creating had made.
4 Haya yalikuwa ni matukio yahusuyo mbingu na nchi, wakati vilipoumbwa, katika siku ambayo Yahwe Mungu aliumba nchi na mbingu.
These are the generations of the heaven and of the earth when they were created, in the day that the LORD God made earth and heaven.
5 Hapakuwa na msitu wa shambani uliokuwa katika nchi, na hapakuwa na mmea wa shambani uliokuwa umechipuka, kwa kuwa Yahwe Mungu alikuwa hajasababisha mvua kunyesha juu ya nchi, na hapakuwa na mtu wa kulima ardhi.
No shrub of the field was yet in the earth, and no herb of the field had yet sprung up; for the LORD God had not caused it to rain upon the earth, and there was not a man to till the ground;
6 Lakini ukungu uliinuka juu kutoka kwenye nchi na kuutia maji uso wote wa ardhi.
but there went up a mist from the earth, and watered the whole face of the ground.
7 Yahwe Mungu aliumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi, na akampulizia puani pumzi ya uhai, na mtu akawa kiumbe hai.
Then the LORD God formed man of the dust of the ground, and breathed into his nostrils the breath of life; and man became a living soul.
8 Yahwe Mungu aliotesha bustani upande wa mashariki, katika Edeni, na pale akamuweka mtu ambaye alimuumba.
And the LORD God planted a garden eastward, in Eden; and there He put the man whom He had formed.
9 Kutoka ardhini Yahwe Mungu alifanya kila mti uote ambao unapendeza na ni mzuri kwa chakula. Hii ni pamoja na mti wa uzima ambao ulikuwa katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
And out of the ground made the LORD God to grow every tree that is pleasant to the sight, and good for food; the tree of life also in the midst of the garden, and the tree of the knowledge of good and evil.
10 Mto ukatoka nje ya Edeni kuitia maji bustani. Na kutoka pale ukagawanyika na kuwa mito minne.
And a river went out of Eden to water the garden; and from thence it was parted, and became four heads.
11 Jina la ule wa kwanza ni Pishoni. Huu ni ule ambao unatiririka kupitia nchi yote ya Havila, ambapo kuna dhahabu.
The name of the first is Pishon; that is it which compasseth the whole land of Havilah, where there is gold;
12 Dhahabu ya inchi ile ni nzuri. pia kuna bedola na jiwe shohamu.
and the gold of that land is good; there is bdellium and the onyx stone.
13 Jina la mto wa pili ni Gihoni. Huu unatiririka kupitia nchi yote ya kushi.
And the name of the second river is Gihon; the same is it that compasseth the whole land of Cush.
14 Jina la mto wa tatu ni Hidekeli, ambao unatiririka mashariki mwa Ashuru. Mto wa nne ni Frati.
And the name of the third river is Tigris; that is it which goeth toward the east of Asshur. And the fourth river is the Euphrates.
15 Yahwe Mungu alimtwaa mtu na kumweka ndani ya bustani ya Edeni kuilima na kuitunza.
And the LORD God took the man, and put him into the garden of Eden to dress it and to keep it.
16 Yahwe Mungu alimuagiza mtu akisema, “kutoka kwenye kila mti bustanini waweza kula kwa uhuru.
And the LORD God commanded the man, saying: 'Of every tree of the garden thou mayest freely eat;
17 Lakini kutoka kwenye mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa kuwa siku utakayo kula kutoka katika mti huo, utakufa hakika.”
but of the tree of the knowledge of good and evil, thou shalt not eat of it; for in the day that thou eatest thereof thou shalt surely die.'
18 Kisha Yahwe Mungu akasema, “siyo jambo jema kwamba mtu huyu lazima awe pekeyake. Nitamfanyia msaidizi anaye mfaa.”
And the LORD God said: 'It is not good that the man should be alone; I will make him a help meet for him.'
19 Kutoka ardhini Yahwe Mungu akafanya kila mnyama wa kondeni na kila ndege wa angani. Kisha akawaleta kwa mtu huyu aone angewapatia majina gani. Jina ambalo mtu huyu alimwita kila kiumbe hai, hili ndilo lilikuwa jina lake.
And out of the ground the LORD God formed every beast of the field, and every fowl of the air; and brought them unto the man to see what he would call them; and whatsoever the man would call every living creature, that was to be the name thereof.
20 Mtu huyu akawapatia majina wanyama wote, ndege wote wa angani, na kila mnyama wa mwitu. Lakini kwa mtu mwenyewe hapakuwa na msaidizi wa kumfaa yeye.
And the man gave names to all cattle, and to the fowl of the air, and to every beast of the field; but for Adam there was not found a help meet for him.
21 Yahwe Mungu akaleta usingizi mzito kwa mtu huyu, kwa hiyo mtu huyu akalala. Yahwe Mungu akatwaa moja ya mbavu za mtu huyu na akapafunika pale alipo chukua ubavu.
And the LORD God caused a deep sleep to fall upon the man, and he slept; and He took one of his ribs, and closed up the place with flesh instead thereof.
22 Kwa ubavu ambao Yahwe Mungu alichukua toka kwa mtu huyu, akafanya mwanamke na akamleta kwa mtu huyu.
And the rib, which the LORD God had taken from the man, made He a woman, and brought her unto the man.
23 Mwanaume akasema, “kwa sasa, huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu. ataitwa 'mwanamke,' kwa sababu ametwaliwa katika mwanaume.
And the man said: 'This is now bone of my bones, and flesh of my flesh; she shall be called Woman, because she was taken out of Man.'
24 Kwa hiyo mwanaume atawaacha baba yake na mama yake, ataungamanika na mke wake, na watakuwa mwili mmoja.
Therefore shall a man leave his father and his mother, and shall cleave unto his wife, and they shall be one flesh.
25 Wote wawili walikuwa uchi, mwanaume na mke wake, lakini hawakuona aibu.
And they were both naked, the man and his wife, and were not ashamed.

< Mwanzo 2 >