< Mwanzo 19 >

1 Malaika wawili wakaja Sodoma jioni, wakati ambao Lutu alikuwa amekaa langoni mwa Sodoma. Lutu akawaona, akainuka kuwalaki, na akainama uso wake chini ardhini.
And they came [the] two the angels Sodom towards in the evening and Lot [was] sitting in [the] gate of Sodom and he saw [them] Lot and he arose to meet them and he bowed down face [the] ground towards.
2 Akasema, Tafadhari Bwana zangu, nawasihi mgeuke mwende kwenye nyumba ya mtumishi wenu, mlale pale usiku na muoshe miguu yenu. Kisha muamke asubuhi na mapema muondoke.” Nao wakasema, “Hapana, usiku tutalala mjini.”
And he said here! please O lords my turn aside please to [the] house of servant your and stay [the] night and wash feet your and you will rise early (and you will go *Lb) to way your and they said In-deed in the open place we will stay [the] night.
3 Lakini akawasihi sana, mwishowe wakaondoka pamoja nae, na wakaingia katika nyumba yake. Akaandaa chakula na kuoka mkate usiotiwa chachu, wakala.
And he urged them exceedingly and they turned aside to him and they went into house his and he prepared for them a feast and unleavened bread he baked and they ate.
4 Lakini kabla hawaja lala, wanaume wa mji, wa Sodoma, vijana kwa wazee wakaizunguka nyumba, wanaume wote kutoka kila kona ya mji.
Before they lay down and [the] men of the city [the] men of Sodom they surrounded the house from young man and unto old [man] all the people from [the] end.
5 Wakamwita Lutu, na kumwambia, “Wale wanaume walioingia kwako usiku wakowapi? watoe hapa nje waje kwetu, ili tuweze kulala nao.”
And they called to Lot and they said to him where? [are] the men who they came to you this night bring them to us so let us know them.
6 Lutu akatoka nje na akafunga mlango.
And he went out to them Lot the entrance towards and the door he closed behind him.
7 Akasema, “Nawasihi, ndugu zangu, msitende uovu.
And he said may not please O brothers my you do evil.
8 Tazama, nina mabinti wawili ambao hawajawahi kulala na mwanaume yeyote. Nawaomba tafadhari niwalete kwenu, na muwafanyie lolote muonalo kuwa jema machoni penu. Msitende lolote kwa wanaume hawa, kwa kuwa wamekuja chini ya kivuli cha dari yangu.”
Here! please [belong] to me two daughters who not they have known a man let me bring out please them to you and do to them according to the good in eyes your only to the men these may not you do anything for since they have come in [the] shadow of roof my.
9 Wakasema, “Ondoka hapa!” Wakasema pia, huyu alikuja kukaa hapa kama mgeni, na sasa amekuwa mwamuzi! Sasa tutakushugulilia vibaya wewe kuliko wao.” Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, na wakakaribia kuvunja mlango.
And they said - approach beyond and they said the one he came to sojourn and he has judged continuously now we will do harm to you more than them and they urged the man Lot exceedingly and they approached to break down the door.
10 Lakini wale wanaume wakamkamata Lutu na kumweka ndani na wakafunga mlango.
And they stretched out the men hand their and they brought Lot to them the house towards and the door they closed.
11 Kisha wale wageni wa Lutu wakawapiga kwa upofu wale wanaume waliokuwa nje ya nyumba, vijana na wazee kwa pamoja, kiasi kwamba wakachoka wakati wakiutafuta mlango.
And the men who [were] [the] entrance of the house they struck with sudden blindness from small and unto great and they became weary to find the entrance.
12 Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je una mtu mwingine yeyote hapa? wakwe zako, wanao na mabinti zako, na yeyote mwingine katika huu mji, ukawatoe hapa.
And they said the men to Lot yet who? [belongs] to you here a son-in-law and sons your and daughters your and all who [belong] to you in the city bring out from the place.
13 Kwa kuwa tunakaribia kuiangamiza sehemu hii, kwa sababu mashitaka dhidi yake mbele ya Yahwe yamezidi kiasi kwamba ametutuma kuuangamiza.”
For [are] about to destroy we the place this for it is great outcry their with [the] face of Yahweh and he has sent us Yahweh to destroy it.
14 Lutu akatoka na akazungumza na wakwe zake, wanaume ambao walikuwa wamewaposa binti zake, akawambia, “Ondokeni upesi mahali hapa, kwa kuwa Yahwe anakaribia kuuangamiza mji.” Lakini kwa wakwe zake alionekana kuwa anawatania.
And he went out Lot and he spoke - to sons-in-law his - [who were] about to take daughters his and he said arise go out from the place this for [is] about to destroy Yahweh the city and he was like [one who] jests in [the] eyes of sons-in-law his.
15 Alfajiri, malaika wakamsihi Lutu, wakisema, ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili ambao wako hapa, ili kwamba usipotelee katika adhabu ya mji huu.”
And when the dawn it came up and they urged the angels Lot saying arise take wife your and [the] two daughters your who are found lest you should be swept away in [the] punishment of the city.
16 Lakini akakawia-kawia. Kwa hiyo watu wale wakamshika mkono wake, na mkono wa mkewe, na mikono ya binti zake wawili, kwa sababu Yahwe alimhurumia. Wakawatoa nje, na kuwaweka nje ya mji.
And he delayed - and they took hold the men on hand his and on [the] hand of wife his and on [the] hand of [the] two daughters his in [the] mercy of Yahweh towards him and they brought out him and they placed him from [the] outside of the city.
17 Wakisha kuwatoa nje mmoja wa wale watu akasema, “jiponye nafsi yako! usitazame nyuma, au usikae mahali popote kwenye hili bonde. Toroka uende milimani ili kwamba usije ukatoweshwa mbali.”
And it was when brought out they them the outside towards and he said escape on life your may not you look behind you and may not you stop in all the valley the hill country towards escape lest you should be swept away.
18 Lutu akawambia, “Hapana, tafadhali bwana zangu!
And he said Lot to them may not [it be] please O Lord.
19 Mtumishi wenu amepata kibali machoni pako, na umenionesha wema ulio mkuu kwa kuokoa maisha yangu, lakini sitaweza kutorokea milimani, kwa sababu mabaya yataniwahi na nitakufa.
Here! please he has found servant your favor in eyes your and you have made great loyalty your which you have done with me by preserving alive life my and I not I am able to escape the hill country towards lest it should cling to me the calamity and I will die.
20 Tazama, ule mji pale uko karibu nijisalimishe pale, na ni mdogo. Tafadhari niacheni nikimbilie pale ( Je Siyo mdogo ule?), na maisha yangu yataokolewa.”
Here! please the city this [is] near to flee there towards and it [is] a small place let me escape please there towards ¿ not a small place [is] it so it may live life my.
21 Akamwambia, “Sawa, nimekubali ombi hili pia, kwamba sitaangamiza mji ambaoumeutaja.
And he said to him here! I lift up face your also to the matter this to not to overthrow I the city which you have spoken.
22 Harakisha! toroka uende pale, kwa kuwa sitafanya chochote mpaka ufike pale.” kwa hiyo mji ule ukaitwa Soari.
Hurry escape there towards for not I will be able to do anything until going you there towards there-fore someone called [the] name of the city Zoar.
23 Jua lilikuwa limekwisha chomoza juu ya nchi wakati Lutu alipofika Soari.
The sun it came out over the earth and Lot he went Zoar towards.
24 Kisha Yahwe akanyesha juu ya Sodoma na Gomora kiberiti na moto toka kwa Yahwe mbinguni.
And Yahweh he caused to rain on Sodom and on Gomorrah sulfur and fire from with Yahweh from the heavens.
25 Akaharibu miji ile, na bonde lote, na vyote vilivyomo katika miji, na mimea iliyo chipua juu ya ardhi.
And he overthrew the cities these and all the valley and all [the] inhabitants of the cities and [the] growth of the ground.
26 Lakini mke wa Lutu aliye kuwa nyuma yake, akatazama nyuma, na akawa nguzo ya chumvi.
And she looked wife his from behind him and she was a pillar of salt.
27 Abraham akaamuka asubuhi na mapema akaenda mahali alipokuwa amesimama mbele ya Yahwe.
And he rose early Abraham in the morning to the place where he had stood there with [the] face of Yahweh.
28 Akatazama chini kuelekea Sodoma na Gomora na kuelekea katika nchi yote bondeni. Akaona na tazama, moshi ulikuwauki ukienda juu kutoka chini kama moshi wa tanuru.
And he looked down on [the] face of Sodom and Gomorrah and on all [the] face of [the] land of the valley and he saw and there! it went up [the] smoke of the land like [the] smoke of furnace.
29 Wakati Mungu alipoharibu miji ya bondeni, Mungu akamkumbuka Abraham. Akamtoa Lutu kutoka katika maangamizi alipoangamiza miji ambayo katika hiyo Lutu aliishi.
And it was when destroyed God [the] cities of the valley and he remembered God Abraham and he sent out Lot from [the] middle of the overthrow when overthrew the cities which he had dwelt in them Lot.
30 Lakini Lutu akapanda juu kutoka Soari na kwenda kuishi katika milima akiwa pamoja na binti zake wawili, kwa sababu aliogopa kuishi Soari. Kwa hiyo akaishi pangoni, yeye na binti zake wawili.
And he went up Lot from Zoar and he dwelt in the hill country and [the] two daughters his [were] with him for he was afraid to dwell in Zoar and he dwelt in the cave he and [the] two daughters his.
31 Yule wa kwanza akamwambia yule mdogo, “Baba yetu ni mzee, na hakuna mwanaume mahali popote wa kulala na sisi kulingana na desturi ya dunia yote.
And she said the firstborn to the young father our he is old and [is] a man there not in the land to go on us according to [the] way of all the earth.
32 Njoo na tumnyweshe baba yetu mvinyo na tulale naye ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”
Come! let us make drink father our wine and let us lie with him so we may preserve alive from father of our spring.
33 Kwa hiyo wakamnywesha baba yako mvinyo usiku ule. Kisha yule wa kwanza akaingia na akalala na baba yake; Baba yake hakujua ni wakati gani alikuja kulala, wala wakati alipo amka.
And they made drink father their wine in the night that and she came the firstborn and she lay with father her and not he knew when lay down she and when arose she.
34 Siku iliyo fuata yule wa kwanza akamwambia mdogowake, “Sikiliza, usiku wa jana nililala na baba yangu. Na tumnyweshe mvinyo usiku wa leo pia, na uingie ukalale naye. Ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”
And it was from [the] next day and she said the firstborn to the young here! I lay with last night father my let us make drink him wine also this night and go lie with him so we may preserve alive from father of our spring.
35 Kwa hiyo wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule pia, na yule mdogo akaenda na akalala naye. Baba yake hakujua ni wakati gani alilala, wala wakati alipoamka.
And they made drink also in the night that father their wine and she arose the young and she lay with him and not he knew when lay down she and when arose she.
36 Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao.
And they conceived [the] two [the] daughters of Lot from father their.
37 Wa kwanza akazaa mwana wa kiume, na akamwita jina lake Moabu. Akawa ndiye baba wa wamoabu hata leo.
And she bore the firstborn a son and she called name his Moab he [is] [the] ancestor of Moab until this day.
38 Nayule mdogo naye akazaa mwana wa kiume, na akamwita Benami. Huyu ndiye baba wa watu wa Waamoni hata leo.
And the young also she she bore a son and she called name his Ben-Ammi he [is] [the] ancestor of [the] people of Ammon until this day.

< Mwanzo 19 >