< Mwanzo 19 >

1 Malaika wawili wakaja Sodoma jioni, wakati ambao Lutu alikuwa amekaa langoni mwa Sodoma. Lutu akawaona, akainuka kuwalaki, na akainama uso wake chini ardhini.
The two angels came to Sodom at evening. Lot sat in the gate of Sodom. Lot saw them, and rose up to meet them. He bowed himself with his face to the earth,
2 Akasema, Tafadhari Bwana zangu, nawasihi mgeuke mwende kwenye nyumba ya mtumishi wenu, mlale pale usiku na muoshe miguu yenu. Kisha muamke asubuhi na mapema muondoke.” Nao wakasema, “Hapana, usiku tutalala mjini.”
and he said, "See now, my lords, please turn aside into your servant's house, and stay all night, and wash your feet, then you may rise up early, and go on your way." They said, "No, but we will stay in the street all night."
3 Lakini akawasihi sana, mwishowe wakaondoka pamoja nae, na wakaingia katika nyumba yake. Akaandaa chakula na kuoka mkate usiotiwa chachu, wakala.
But he urged them so strongly that they came in with him, and entered into his house. He made them a feast, and baked unleavened bread, and they ate.
4 Lakini kabla hawaja lala, wanaume wa mji, wa Sodoma, vijana kwa wazee wakaizunguka nyumba, wanaume wote kutoka kila kona ya mji.
But before they could lie down to sleep, the men of the city, the men of Sodom, surrounded the house, both young and old, all the people from every quarter.
5 Wakamwita Lutu, na kumwambia, “Wale wanaume walioingia kwako usiku wakowapi? watoe hapa nje waje kwetu, ili tuweze kulala nao.”
They called to Lot, and said to him, "Where are the men who came in to you this night? Bring them out to us, that we may have sex with them."
6 Lutu akatoka nje na akafunga mlango.
Lot went out to them at the entrance, and shut the door behind him.
7 Akasema, “Nawasihi, ndugu zangu, msitende uovu.
He said, "Please, my brothers, do not act so wickedly.
8 Tazama, nina mabinti wawili ambao hawajawahi kulala na mwanaume yeyote. Nawaomba tafadhari niwalete kwenu, na muwafanyie lolote muonalo kuwa jema machoni penu. Msitende lolote kwa wanaume hawa, kwa kuwa wamekuja chini ya kivuli cha dari yangu.”
Look, I have two virgin daughters. Please let me bring them out to you, and you may do to them what seems good to you. Only do not do anything to these men, because they have come under the protection of my roof."
9 Wakasema, “Ondoka hapa!” Wakasema pia, huyu alikuja kukaa hapa kama mgeni, na sasa amekuwa mwamuzi! Sasa tutakushugulilia vibaya wewe kuliko wao.” Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, na wakakaribia kuvunja mlango.
They said, "Stand back." They said, "This one fellow came in to live as a foreigner, and he appoints himself a judge. Now will we deal worse with you, than with them." They pressed hard on the man Lot, and drew near to break the door.
10 Lakini wale wanaume wakamkamata Lutu na kumweka ndani na wakafunga mlango.
But the men reached out their hands and pulled Lot into the house to them, and shut the door.
11 Kisha wale wageni wa Lutu wakawapiga kwa upofu wale wanaume waliokuwa nje ya nyumba, vijana na wazee kwa pamoja, kiasi kwamba wakachoka wakati wakiutafuta mlango.
They struck the men who were at the door of the house with blindness, both small and great, so that they were unable to find the door.
12 Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je una mtu mwingine yeyote hapa? wakwe zako, wanao na mabinti zako, na yeyote mwingine katika huu mji, ukawatoe hapa.
The men said to Lot, "Do you have anybody else here? Sons-in-law, your sons, your daughters, and whoever you have in the city, bring them out of the place:
13 Kwa kuwa tunakaribia kuiangamiza sehemu hii, kwa sababu mashitaka dhidi yake mbele ya Yahwe yamezidi kiasi kwamba ametutuma kuuangamiza.”
for we will destroy this place, because the outcry against them has grown great before God that he has sent us to destroy it."
14 Lutu akatoka na akazungumza na wakwe zake, wanaume ambao walikuwa wamewaposa binti zake, akawambia, “Ondokeni upesi mahali hapa, kwa kuwa Yahwe anakaribia kuuangamiza mji.” Lakini kwa wakwe zake alionekana kuwa anawatania.
Lot went out, and spoke to his sons-in-law, who were pledged to marry his daughters, and said, "Get up. Get out of this place, for God will destroy the city." But he seemed to his sons-in-law to be joking.
15 Alfajiri, malaika wakamsihi Lutu, wakisema, ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili ambao wako hapa, ili kwamba usipotelee katika adhabu ya mji huu.”
When the morning came, then the angels hurried Lot along, saying, "Get up. Take your wife, and your two daughters who are here, and get out, lest you be swept away in the punishment of the city."
16 Lakini akakawia-kawia. Kwa hiyo watu wale wakamshika mkono wake, na mkono wa mkewe, na mikono ya binti zake wawili, kwa sababu Yahwe alimhurumia. Wakawatoa nje, na kuwaweka nje ya mji.
But he hesitated, so the men grabbed his hand, his wife's hand, and his two daughters' hands, God being merciful to him; and they took him out, and set him outside of the city.
17 Wakisha kuwatoa nje mmoja wa wale watu akasema, “jiponye nafsi yako! usitazame nyuma, au usikae mahali popote kwenye hili bonde. Toroka uende milimani ili kwamba usije ukatoweshwa mbali.”
It came to pass, when they had taken them out, that he said, "Escape for your life. Do not look behind you, and do not stay anywhere in the plain. Escape to the mountains, or you will be swept away."
18 Lutu akawambia, “Hapana, tafadhali bwana zangu!
Lot said to them, "Oh, not so, my lord.
19 Mtumishi wenu amepata kibali machoni pako, na umenionesha wema ulio mkuu kwa kuokoa maisha yangu, lakini sitaweza kutorokea milimani, kwa sababu mabaya yataniwahi na nitakufa.
See now, your servant has found favor in your sight, and you have magnified your loving kindness, which you have shown to me in saving my life. I can't escape to the mountain, lest the disaster overtake me, and I die.
20 Tazama, ule mji pale uko karibu nijisalimishe pale, na ni mdogo. Tafadhari niacheni nikimbilie pale ( Je Siyo mdogo ule?), na maisha yangu yataokolewa.”
See now, this city is near to flee to, and it is a little one. Let me escape there--isn't it a little one?--and my life will be saved."
21 Akamwambia, “Sawa, nimekubali ombi hili pia, kwamba sitaangamiza mji ambaoumeutaja.
He said to him, "Look, I have granted your request concerning this thing also, that I will not overthrow the city of which you have spoken.
22 Harakisha! toroka uende pale, kwa kuwa sitafanya chochote mpaka ufike pale.” kwa hiyo mji ule ukaitwa Soari.
Hurry, escape there, for I can't do anything until you get there." Therefore the name of the city was called Zoar.
23 Jua lilikuwa limekwisha chomoza juu ya nchi wakati Lutu alipofika Soari.
The sun had risen on the earth when Lot came to Zoar.
24 Kisha Yahwe akanyesha juu ya Sodoma na Gomora kiberiti na moto toka kwa Yahwe mbinguni.
Then the LORD rained on Sodom and on Gomorrah sulfur and fire from the sky.
25 Akaharibu miji ile, na bonde lote, na vyote vilivyomo katika miji, na mimea iliyo chipua juu ya ardhi.
He overthrew those cities, and all the plain, and all the inhabitants of the cities, and that which grew on the ground.
26 Lakini mke wa Lutu aliye kuwa nyuma yake, akatazama nyuma, na akawa nguzo ya chumvi.
But his wife looked back from behind him, and she became a pillar of salt.
27 Abraham akaamuka asubuhi na mapema akaenda mahali alipokuwa amesimama mbele ya Yahwe.
Abraham got up early in the morning to the place where he had stood before God.
28 Akatazama chini kuelekea Sodoma na Gomora na kuelekea katika nchi yote bondeni. Akaona na tazama, moshi ulikuwauki ukienda juu kutoka chini kama moshi wa tanuru.
He looked toward Sodom and Gomorrah, and toward all the land of the plain, and he saw; and look, the smoke was rising from the land like smoke from a furnace.
29 Wakati Mungu alipoharibu miji ya bondeni, Mungu akamkumbuka Abraham. Akamtoa Lutu kutoka katika maangamizi alipoangamiza miji ambayo katika hiyo Lutu aliishi.
It happened, when God destroyed the cities of the plain, that God remembered Abraham, and sent Lot out of the middle of the overthrow, when he overthrew the cities in which Lot lived.
30 Lakini Lutu akapanda juu kutoka Soari na kwenda kuishi katika milima akiwa pamoja na binti zake wawili, kwa sababu aliogopa kuishi Soari. Kwa hiyo akaishi pangoni, yeye na binti zake wawili.
Lot went up out of Zoar, and lived in the mountain, and his two daughters with him; for he was afraid to live in Zoar. He lived in a cave with his two daughters.
31 Yule wa kwanza akamwambia yule mdogo, “Baba yetu ni mzee, na hakuna mwanaume mahali popote wa kulala na sisi kulingana na desturi ya dunia yote.
The firstborn said to the younger, "Our father is old, and there is not a man in the land to sleep with us according to the custom of all the land.
32 Njoo na tumnyweshe baba yetu mvinyo na tulale naye ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”
Come, let's make our father drink wine, and we will sleep with him, that we may preserve our family through our father."
33 Kwa hiyo wakamnywesha baba yako mvinyo usiku ule. Kisha yule wa kwanza akaingia na akalala na baba yake; Baba yake hakujua ni wakati gani alikuja kulala, wala wakati alipo amka.
They made their father drink wine that night: and the firstborn went in, and slept with her father. He did not know when she lay down, nor when she arose.
34 Siku iliyo fuata yule wa kwanza akamwambia mdogowake, “Sikiliza, usiku wa jana nililala na baba yangu. Na tumnyweshe mvinyo usiku wa leo pia, na uingie ukalale naye. Ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”
It came to pass on the next day, that the firstborn said to the younger, "Look, I slept last night with my father. Let us make him drink wine again tonight. You go in, and sleep with him, that we may preserve our family through our father."
35 Kwa hiyo wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule pia, na yule mdogo akaenda na akalala naye. Baba yake hakujua ni wakati gani alilala, wala wakati alipoamka.
They made their father drink wine that night also. The younger went and slept with him. He did not know when she lay down, nor when she got up.
36 Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao.
Thus both of Lot's daughters became pregnant by their father.
37 Wa kwanza akazaa mwana wa kiume, na akamwita jina lake Moabu. Akawa ndiye baba wa wamoabu hata leo.
The firstborn bore a son, and named him Moab. He is the father of the Moabites to this day.
38 Nayule mdogo naye akazaa mwana wa kiume, na akamwita Benami. Huyu ndiye baba wa watu wa Waamoni hata leo.
The younger also bore a son, and called his name Ben Ammi. He is the father of the people of Ammon to this day.

< Mwanzo 19 >