< Mwanzo 18 >

1 Yahwe alimtokea Abraham katika Mialoni ya Mamre, alipokua ameketi mlangoni pa hema wakati wa jua.
and to see: see to(wards) him LORD in/on/with terebinth Mamre and he/she/it to dwell entrance [the] tent like/as heat [the] day
2 Akatazama juu na, tazama, akaona wanaume watatu wamesimama mbele yake. Alipo waona, alikimbia kupitia mlango wa hema kuwalaki na kuinama chini hadi ardhini.
and to lift: look eye his and to see: see and behold three human to stand upon him and to see: see and to run: run to/for to encounter: meet them from entrance [the] tent and to bow land: soil [to]
3 Akasema, “Bwana, kama nimepata upendelea machoni pako, nakuomba usinipite na kuniacha mtumishi wako.
and to say lord my if please to find favor in/on/with eye: seeing your not please to pass from upon servant/slave your
4 Naomba maji kidogo yaletwe, mnawe miguu yenu, na mjipumzishe chini ya mti.
to take: bring please little water and to wash: wash foot your and to lean underneath: under [the] tree
5 Nami acha nilete chakula kidogo, ili kwamba mjiburudishe wenyewe. Ndipo baadae mwaweza kwenda zenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.” Nao wakasema, “Fanya kama ulivyo sema.”
and to take: bring morsel food: bread and to support heart your (after *LS) to pass for as that: since as as to pass upon servant/slave your and to say so to make: do like/as as which to speak: speak
6 Kisha Abraham akaenda upesi hemani kwa Sara, na akasema, “Harakisha, chukua vipimo vitatu vya unga safi, uukande, na fanya mkate.”
and to hasten Abraham [the] tent [to] to(wards) Sarah and to say to hasten three seah flour fine flour to knead and to make bun
7 Kisha Abraham akakimbia kundini, akachukua ndama wa ng'ombe aliye laini na mzuri, na akampatia mtumishi na kwa haraka akamwandaa.
and to(wards) [the] cattle to run: run Abraham and to take: take son: young animal cattle tender and pleasant and to give: give to(wards) [the] youth and to hasten to/for to make [obj] him
8 Akatwaa siagi na maziwa na ndama aliye kwisha andaliwa, na akaweka chakula mbele yao, naye akasimama karibu nao chini ya mti wakati wanakula.
and to take: take curd and milk and son: young animal [the] cattle which to make and to give: put to/for face: before their and he/she/it to stand: stand upon them underneath: under [the] tree and to eat
9 Wakamwambia, “Mke wako Sara yuko wapi?” akajibu. “pale hemani.”
and to say to(wards) him where? Sarah woman: wife your and to say behold in/on/with tent
10 akasema, “Hakika nitarejea kwako majira ya machipuko, na tazama Sara mkeo atakuwa na mtoto wa kiume.” Sara alikuwa akisikiliza mlangoni pa hema iliyokuwa nyuma yake.
and to say to return: return to return: return to(wards) you like/as time alive and behold son: child to/for Sarah woman: wife your and Sarah to hear: hear entrance [the] tent and he/she/it after him
11 Abraham na Sara walikuwa wazee, umri wao ulikuwa umeendelea sana, na Sara alikuwa amepita umri ambao mwanamke anaweza kuzaa watoto.
and Abraham and Sarah old to come (in): advanced in/on/with day: year to cease to/for to be to/for Sarah way like/as woman
12 Kwa hiyo Sara akajicheka mwenyewe, akijisemesha mwenyewe, “baada ya kuwa nimechakaa na bwana wangu ni mzee, je ni tapata furaha hii?”
and to laugh Sarah in/on/with entrails: among her to/for to say after to become old I to be to/for me delight and lord my be old
13 Yahwe akamwambia Abraham, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, Je ni kweli nitazaa mtoto, nikiwa mzee'?
and to say LORD to(wards) Abraham to/for what? this to laugh Sarah to/for to say also truly to beget and I be old
14 Je kuna jambo lolote gumu sana kwa Yahwe? Itakuwa katika wakati nilioweka mimi majira ya machipuko, nitarejea kwako. Majira haya mwakani Sara atakuwa na mtoto wa kiume.”
to wonder from LORD word: thing to/for meeting: time appointed to return: return to(wards) you like/as time alive and to/for Sarah son: child
15 Kisha Sara akakataa na kusema, “sikucheka,” kwa kuwa aliogopa. Yahwe akasema, “hapana ulicheka.”
and to deceive Sarah to/for to say not to laugh for to fear and to say not for to laugh
16 Kisha wale wanaume walisimama kuondoka na wakatazama chini kuelekea Sodoma. Abraham akafuatana nao kuona njia yao.
and to arise: rise from there [the] human and to look upon face: surface Sodom and Abraham to go: went with them to/for to send: depart them
17 Lakini Yahwe akasema, Je ni mfiche Abraham kile ninacho kusudia kufanya,
and LORD to say to cover I from Abraham which I to make: do
18 Ikiwa kwa hakika Abraham atakuwa mkuu na taifa lenye nguvu, na katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa?
and Abraham to be to be to/for nation great: large and mighty and to bless in/on/with him all nation [the] land: country/planet
19 Kwa kuwa nimemchagua ili awaelekeze wanawe na nyumba yake baada yake waishike njia ya Yahwe, watende utakatifu na haki, ili kwamba Yahwe ampatie Abraham yale aliyo yasema kwake.”
for to know him because which to command [obj] son: child his and [obj] house: household his after him and to keep: obey way: conduct LORD to/for to make: do righteousness and justice because to come (in): bring LORD upon Abraham [obj] which to speak: promise upon him
20 Kisha Yahwe akasema, “Kwa sababu kilio cha Sodoma na Gomora ni kikuu, na kwa kuwa dhambi yao ni kubwa,
and to say LORD outcry Sodom and Gomorrah for to multiply and sin their for to honor: heavy much
21 sasa nitashuka pale na kuona kilio kilicho nifikia dhidi yake, ikiwa kweli wamefanya au hawakufanya, nitajua.”
to go down please and to see: see like/as cry her [the] to come (in): come to(wards) me to make: do consumption and if not to know
22 Kwa hiyo wale wanaume wakageuka toka pale, na kuelekea Sodoma, lakini Abraham akabaki amesimama mbele ya Yahwe.
and to turn from there [the] human and to go: went Sodom [to] (and Abraham *LS) still he to stand: stand to/for face: before (LORD *LS)
23 Kisha Abraham alikaribia na kusema, “Je utawafutilia mbali watakatifu pamoja na waovu?
and to approach: approach Abraham and to say also to snatch righteous with wicked
24 Huenda wakawepo wenye haki hamsini katika mji. Je utawakatilia mbali na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?
perhaps there fifty righteous in/on/with midst [the] city also to snatch and not to lift: bear to/for place because fifty [the] righteous which in/on/with entrails: among her
25 Hasha usifanye hivyo, kuwauwa watakatifu pamoja na waovu, ili kwamba watakatifu watendewe sawa na waovu. Hasha! Je muhukumu wa ulimwengu wote hatatenda haki?”
forbid to/for you from to make: do like/as Chronicles [the] this to/for to die righteous with wicked and to be like/as righteous like/as wicked forbid to/for you to judge all [the] land: country/planet not to make: do justice
26 Yahwe akasema, “Katika Sodoma nikipata watakatifu hamsini kwenye mji, nita uacha mji wote kwa ajili ya hao.”
and to say LORD if to find in/on/with Sodom fifty righteous in/on/with midst [the] city and to lift: bear to/for all [the] place in/on/with for the sake of them
27 Abraham akajibu na kusema, “Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu, hata kama mimi ni mavumbi na majivu!
and to answer Abraham and to say behold please be willing to/for to speak: speak to(wards) Lord and I dust and ashes
28 Itakuwaje ikiwa kuna watano pungufu katika idadi ya hao watakatifu hamsini? Je utaangamiza mji wote kwa upungufu wa hao watano?” Akasema, “Sitaangamiza, ikiwa nitapata watu arobaini na watano pale.”
perhaps to lack [emph?] fifty [the] righteous five to ruin in/on/with five [obj] all [the] city and to say not to ruin if to find there forty and five
29 Akaongea naye tena, na kusema, “Itakuwaje ikiwa arobaini watapatikana pale?” Akajibu, “Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini.”
and to add: again still to/for to speak: speak to(wards) him and to say perhaps to find [emph?] there forty and to say not to make: do in/on/with for the sake of [the] forty
30 Akasema, Tafadhali usikasirike, Bwana, nikiongea. Pengine thelathini watapatikana pale.” Akajibu, 'Sitafanya, ikiwa nitapata thelathini pale.”
and to say not please to be incensed to/for Lord and to speak: speak perhaps to find [emph?] there thirty and to say not to make: do if to find there thirty
31 Akasema, Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu! Pengine ishirini watapatikana pale.” Akajibu, “Sitaharibu kwa ajili ya hao ishirini.”
and to say behold please be willing to/for to speak: speak to(wards) Lord perhaps to find [emph?] there twenty and to say not to ruin in/on/with for the sake of [the] twenty
32 Akasema, “Tafadhali usikasirike, Bwana, na nitasema jambo hili kwa mara ya mwisho. Huenda kumi wakaonekana kule.” Na akasema, sitaangamiza kwa ajili ya hao kumi.”
and to say not please to be incensed to/for Lord and to speak: speak surely [the] beat perhaps to find [emph?] there ten and to say not to ruin in/on/with for the sake of [the] ten
33 Yahwe akaendelea na njia yake mara tu baada ya kumaliza kuongea na Abraham, na Abraham akarudi nyumbani.
and to go: journey LORD like/as as which to end: finish to/for to speak: speak to(wards) Abraham and Abraham to return: return to/for place his

< Mwanzo 18 >