< Mwanzo 15 >

1 Baada ya mabo haya neno la Yahwe likamjia Abram katika maono, likisema, “Usiogope, Abram! mimi ni ngao yako na thawabu yako kubwa sana.”
After these things hath the word of Jehovah been unto Abram in a vision, saying, 'Fear not, Abram, I [am] a shield to thee, thy reward [is] exceeding great.'
2 Abram akasema, “Bwana Yahwe, utanipatia nini, kwa kuwa naenda bila mtoto, na mrithi wa nyumba yangu ni Eliezeri wa Dameski?”
And Abram saith, 'Lord Jehovah, what dost Thou give to me, and I am going childless? and an acquired son in my house is Demmesek Eliezer.'
3 Abram akasema, “Kwakuwa hujanipatia uzao, tazama, mwangalizi wa nyumba yangu ndiye mrithi wangu.”
And Abram saith, 'Lo, to me Thou hast not given seed, and lo, a domestic doth heir me.'
4 Kisha, tazama, neno la Yahwe likaja kwake, kusema, “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako; isipokuwa atakaye toka katika mwili wako ndiye atakuwa mrithi wako.”
And lo, the word of Jehovah [is] unto him, saying, 'This [one] doth not heir thee; but he who cometh out from thy bowels, he doth heir thee;'
5 Kisha akamtoa nje, na akasema, Tazama mbinguni, na uzihesabu nyota, ikiwa unaweza kuzihesabu.” Kisha akamwambia, hivyo ndivyo uzao wako utakavyokuwa.
and He bringeth him out without, and saith, 'Look attentively, I pray thee, towards the heavens, and count the stars, if thou art able to count them;' and He saith to him, 'Thus is thy seed.'
6 Akamwamini Yahwe, na akamuhesabia jambo hili kuwa mwenye haki.
And he hath believed in Jehovah, and He reckoneth it to him — righteousness.
7 Akamwambia, Mimi ni Yahwe, niliye kutoa katika Uru ya Wakaldayo, na kukupatia nchi hii kuirithi.”
And He saith unto him, 'I [am] Jehovah who brought thee out from Ur of the Chaldees, to give to thee this land to possess it;'
8 Akasema, “Bwana Yahwe, nitajua je kuwa nitairithi?”
and he saith, 'Lord Jehovah, whereby do I know that I possess it?'
9 Kisha akamwambia, “Nipatie ndama wa umri wa miaka mitatu, mbuzi mke wa umri wa miaka mitatu, na kondoo mume wa umri wa miaka mitatu, na njiwa na mwana njiwa.”
And He saith unto him, 'Take for Me a heifer of three years, and a she-goat of three years, and a ram of three years, and a turtle-dove, and a young bird;'
10 Akamletea hivi vyote, akavipasua katika sehemu mbili, akaweka kila kipande kuelekea mwenzake, ila ndege hakuawapasua.
and he taketh to him all these, and separateth them in the midst, and putteth each piece over against its fellow, but the bird he hath not divided;
11 Wakati ndege walipokuja juu ya mizoga, Abram akawafukuza.
and the ravenous birds come down upon the carcases, and Abram causeth them to turn back.
12 Kisha wakati jua lilipokuwa likizama, Abram akalala usingizi mzito na tazama, hofu ya giza kuu ikamfunika.
And the sun is about to go in, and deep sleep hath fallen upon Abram, and lo, a terror of great darkness is falling upon him;
13 Kisha Yahwe akamwambia Abram, “Ujuwe kwa hakika kwamba uzao wako watakuwa wageni katika nchi ambayo si ya kwao, na watatumikishwa na kuteswa kwa miaka mia nne.
and He saith to Abram, 'knowing — know that thy seed is a sojourner in a land not theirs, and they have served them, and they have afflicted them four hundred years,
14 Nitahukumu taifa ambalo watalitumikia, na baadye watatoka wakiwa na mali nyingi.
and the nation also whom they serve I judge, and after this they go out with great substance;
15 Lakini utakwenda kwa baba zako kwa amani, na utazikwa katika uzee mwema.
and thou — thou comest in unto thy fathers in peace; thou art buried in a good old age;
16 Katika kizazi cha nne watakuja tena hapa, kwa sababu uovu wa Waamori haujafikia mwisho wake.”
and the fourth generation doth turn back hither, for the iniquity of the Amorite is not yet complete.'
17 Jua lilipokuwa limezama na kuwa giza, tazama, chungu cha moshi wenye moto na miali ya mwanga ilipita kati ya vile vipande.
And it cometh to pass — the sun hath gone in, and thick darkness hath been — and lo, a furnace of smoke, and a lamp of fire, which hath passed over between those pieces.
18 Siku hiyo Yahwe akafanya agano na Abram, akisema, “Ninatoa nchi hii kwa uzao wako, kutoka mto wa Misri hadi kwenye mto mkuu, Frati -
In that day hath Jehovah made with Abram a covenant, saying, 'To thy seed I have given this land, from the river of Egypt unto the great river, the river Phrat,
19 Mkeni, Mkenizi, na Mkadmoni,
with the Kenite, and the Kenizzite, and the Kadmonite,
20 Mhiti, Mperizi, Mrefai,
and the Hittite, and the Perizzite, and the Rephaim,
21 Mwamori, Mkanaani, Mgirgashi, na Myebusi.
and the Amorite, and the Canaanite, and the Girgashite, and the Jebusite.'

< Mwanzo 15 >