< Mwanzo 13 >

1 Kwa hiyo Abram akaondoka akatoka Misri na akaenda Negebu, Yeye, mke wake, na vyote alivyokuwa navyo. Lutu pia akaenda pamoja naye.
And Abram went up out of Egypt, he and his wife, and all that he had, and Lot with him, into the wilderness.
2 Na sasa Abram alikuwa tajiri wa mifugo, fedha na dhahabu.
And Abram was very rich in cattle, and silver, and gold.
3 Aliendelea na safari yake kutoka Negebu hadi Betheli, mahali ambapo hema yake ilikuwa tangu mwanzo, kati ya Betheli na mji wa Ai.
And he went [to the place] whence he came, into the wilderness as far as Baethel, as far as the place where his tent was before, between Baethel and Aggai,
4 Akaenda mahali ambapo madhabahu ilikuwa imejengwa mwanzoni. Hapa akaliitia jina la Yahwe.
to the place of the altar, which he built there at first, and Abram there called on the name of the Lord.
5 aliyekuwa anasafiri na Abram, alikuwa pia na ngo'mbe, makundi ya mifugo, na mahema.
And Lot who went out with Abram had sheep, and oxen, and tents.
6 Nchi haikuwatosha wote kukaa pamoja karibu kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana, kiasi kwamba hawakuweza kukaa pamoja.
And the land was not large enough for them to live together, because their possessions were great; and the land was not large enough for them to live together.
7 Pia, kulikuwa na ugomvi kati ya wachunga wanyama wa Abram na wachunga wanyama wa Lutu. Wakanaani pamoja na Waperizi walikuwa wakiishi katika nchi ile wakati huo.
And there was a strife between the herdmen of Abram's cattle, and the herdmen of Lot's cattle, and the Chananites and the Pherezites then inhabited the land.
8 Kwa hiyo Abram akamwambia Lutu, “Pasiwe na ugomvi kati yako na mimi, na kati ya wachunga wanyama wako na wachunga wanyama wangu; licha ya hayo sisi ni familia.
And Abram said to Lot, Let there not be a strife between me and you, and between my herdmen and your herdmen, for we are brethren.
9 Je nchi hii yote haiko mbele yako? Nenda na ujitenge na mi. Ikiwa utakwenda kushoto, mimi nitakwenda kulia. au ikiwa utakwenda kulia, mimi nitakwenda kushoto.”
Behold! is not the whole land before you? Separate yourself from me; if you [go] to the left, I will go to the right, and if you go to the right, I will go to the left.
10 Kwa hiyo Lutu akatazama, na akaona kuwa nchi yote tambarare ya Yorodani ilikuwa na maji kila mahali hadi Zoari, kama vile bustani ya Yahwe, na kama nchi ya Misri. Hii ilikuwa ni kabla Yahwe hajaiangamiza Sodoma na Gomora.
And Lot having lifted up his eyes, observed all the country round about Jordan, that it was all watered, before God overthrew Sodom and Gomorrha, as the garden of the Lord, and as the land of Egypt, until you come to Zogora.
11 Kwa hiyo Lutu akajichagulia yeye mwenyewe nchi tambarare ya Yorodani na akasafiri mashariki, na ndugu hawa wakatengana wao kwa wao.
And Lot chose for himself all the country round Jordan, and Lot went from the east, and they were separated each from his brother. And Abram lived in the land of Chanaan.
12 Abram akaishi katika nchi ya Kanaani, na Lutu akaishi katika miji ya tambarare. Akatandaza hema zake hadi Sodoma.
And Lot lived in a city of the neighbouring people, and pitched his tent in Sodom.
13 Na sasa watu wa Sodoma walikuwa waovu na wenye dhambi nyingi dhidi ya Yahwe.
But the men of Sodom were evil, and exceedingly sinful before God.
14 Yahwe akamwambia Abram baada ya Lutu kuondoka kwake, “Angalia kuanzia mahali ulipo simama hadi kaskazini, kusini, mashariki, na magharibi.
And God said to Abram after Lot was separated from him, Look up with your eyes, and behold from the place where you now are northward and southward, and eastward and seaward;
15 Nchi yote hii uionayo, nitakupatia wewe pamoja na uzao wako milele.
for all the land which you see, I will give it to you and to your seed for ever.
16 Nitawafanya uzao wako kuwa wengi kama mavumbi ya nchi, kiasi kwamba kama kuna mtu anaweza kuhesabu mavumbi ya nchi, ndipo na uzao wako pia utahesabika.
And I will make your seed like the dust of the earth; if any one is able to number the dust of the earth, then shall your seed be numbered.
17 Inuka, tembea katika urefu na upana wa nchi hii, kwa kuwa nitakupatia.”
Arise and traverse the land, both in the length of it and in the breadth; for to you will I give it, and to your seed for ever.
18 Kwa hiyo Abram akachukua hema yake, akaja na kukaa katika mwaloni wa Mamre, ambao uko Hebroni, na pale akajenga Madhabahu ya Yahwe.
And Abram having removed his tent, came and lived by the oak of Mambre, which was in Chebrom, and he there built an altar to the Lord.

< Mwanzo 13 >