< Mwanzo 10 >

1 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu, ambao ni, Shemu, Hamu, na Yafethi. Wana wa kiume walizaliwa kwao baada ya gharika.
And these [are] [the] accounts of [the] sons of Noah Shem Ham and Japheth and they were born to them sons after the flood.
2 Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Masheki, na Tirasi.
[the] sons of Japheth [were] Gomer and Magog and Madai and Javan and Tubal and Meshech and Tiras.
3 Na wana wa Gomeri walikuwa Ashikenazi, Rifathi na Togama.
And [the] sons of Gomer [were] Ashkenaz and Riphath and Togarmah.
4 Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Dodanimu.
And [the] sons of Javan [were] Elishah and Tarshish Kittim and Dodanim.
5 Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na kwenda kwenye ardhi zao, kila mtu na lugha yake, kufuatana na koo zao, kwa mataifa yao.
From these they separated [the] coastlands of the nations in own lands their each to own language its to clans their in nations their.
6 Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu, Putu, na Kanaani.
And [the] sons of Ham [were] Cush and Mizraim and Put and Canaan.
7 Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama, na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.
And [the] sons of Cush [were] Seba and Havilah and Sabtah and Raamah and Sabteca and [the] sons of Raamah [were] Sheba and Dedan.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikuwa hodari wa kwanza juu ya nchi.
And Cush he fathered Nimrod he he began to be a mighty [man] on the earth.
9 Alikuwa mwindaji mkuu mbele ya Yahwe. Hii ndiyo sababu hunenwa, “Kama Nimrod mwindaji mkuu mbele za Yahwe.”
He he was a mighty [man] of hunting before Yahweh there-fore it is said like Nimrod a mighty [man] of hunting before Yahweh.
10 Miji ya kwanza ya ufalme wake ilikuwa Babeli, Ereku, Akadi na Kalne, katika ichi ya Shinari.
And it was [the] beginning of kingdom his Babel and Erech and Akkad and Calneh in [the] land of Shinar.
11 Kutoka katika nchi ile alikwenda Ashuru na akajenga Ninawi, Rehoboth- iri na Kala,
From the land that he went forth Assyria and he built Nineveh and Rehoboth-Ir and Calah.
12 na Raseni ambao ulikuwa kati ya Ninawi na Kala. Ulikuwa mji mkubwa.
And Resen between Nineveh and between Calah that [is] the city great.
13 Misraimu akazaa Waludi, Waanami, Walehabi, na Wanaftuhi,
And Mizraim he fathered [the] Ludites and [the] Anamites and [the] Lehabites and [the] Naphtuhites.
14 Wapathrusi na Wakasluhi ( ambao kwao Wafilisti walitokea), na Wakaftori.
And [the] Pathrusites and [the] Casluhites where they came out from there [the] Philistines and [the] Caphtorites.
15 Kanaani akamzaa Sidono, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
And Canaan he fathered Sidon firstborn his and Heth.
16 pia na Myebusi, na Mwamori, Mgirgashi,
And the Jebusite[s] and the Amorite[s] and the Girgashite[s].
17 Mhivi, Mwarki, Msini,
And the Hivite[s] and the Arkite[s] and the Sinite[s].
18 Mwarvadi, Msemari, na Mhamathi. Baadaye koo za wakanaani zikasambaa.
And the Arvadite[s] and the Zemarite[s] and the Hamathite[s] and after they were scattered [the] clans of the Canaanite[s].
19 Mpaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza, na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha.
And it was [the] border of the Canaanite[s] from Sidon going you Gerar towards to Gaza going you Sodom towards and Gomorrah and Admah and Zeboiim to Lasha.
20 Hawa walikuwa wana wa Ham, kwa koo zao, kwa lugha zao, katika ardhi zao na katika mataifa yao.
These [were] [the] sons of Ham to clans their to languages their in lands their in nations their.
21 Pia walizaliwa wana kwa Shemu, ndugu yake mkubwa wa Yafethi. Shemu pia alikuwa baba yao na watu wote wa Eberi.
And to Shem was born also he [the] father of all [the] sons of Eber [the] brother of Japheth old.
22 Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Alfaksadi, Ludi, na Aramu.
[the] sons of Shem [were] Elam and Asshur and Arphaxad and Lud and Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa ni Usi, Huli, Getheri, na Mashi.
And [the] sons of Aram [were] Uz and Hul and Gether and Mash.
24 Arfaksadi akamzaa Sela, na Sela akamzaa Eber.
And Arphaxad he fathered Shelah and Shelah he fathered Eber.
25 Eberi akazaa wana wawili wa kiume. Jina la mmoja aliitwa Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika. Jina la ndugu yake aliitwa Yoktani.
And to Eber was born two sons [the] name of the one [was] Peleg for in days his was divided the earth and [the] name of brother his [was] Joktan.
26 Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
And Joktan he fathered Almodad and Sheleph and Hazarmaveth and Jerah.
27 Hadoram, Uzali, Dikla,
And Hadoram and Uzal and Diklah.
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
And Obal and Abimael and Sheba.
29 Ofiri, Havila, na Yobabi. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
And Ophir and Havilah and Jobab all these [were] [the] sons of Joktan.
30 Mpaka wao ulikuwa unaanzia Mesha, hadi Sefari, mlima wa mashariki.
And it was dwelling place their from Mesha going you Sephar towards [the] hill country of the east.
31 Hawa walikuwa wana wa Shemu, kulingana na koo zao na lugha zao, katika ardhi zao kulingana na mataifa yao.
These [were] [the] sons of Shem to clans their to languages their in lands their to nations their.
32 Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.
These [were] [the] clans of [the] sons of Noah to descendants their in nations their and from these they separated the nations on the earth after the flood.

< Mwanzo 10 >