< Wagalatia 3 >

1 Wagalatia wajinga, ni jicho gani ovu lililowaharibu? Je Yesu Kristo hakuoneshwa kama msulubiwa mbele ya macho yenu?
Galates insensés, qui vous a ensorcelés pour que vous n'obéissiez pas à la vérité, et sous les yeux desquels Jésus-Christ a été ouvertement présenté au milieu de vous comme crucifié?
2 Mimi nataka tu kufahamu hili kutoka kwenu. Je mlimpokea Roho kwa matendo ya sheria au kwa kuamini kile mlichosikia?
Je veux apprendre ceci de vous: Avez-vous reçu l'Esprit par les œuvres de la loi, ou par l'audition de la foi?
3 Je, ninyi ni wajinga kiasi hiki? Je mlianza katika Roho ili mmalize katika mwili?
Êtes-vous si insensés? Après avoir commencé dans l'Esprit, êtes-vous maintenant achevés dans la chair?
4 Je mliteseka kwa mambo mengi bure, kama kweli yalikuwa ya bure?
Avez-vous souffert tant de choses en vain, si c'est en vain?
5 Je yeye atoaye Roho kwenu na kutenda matendo ya nguvu kati yenu hufanya kwa matendo ya sheria au kwa kusikia pamoja na imani?
Celui donc qui vous fournit l'Esprit et qui fait des miracles au milieu de vous, le fait-il par les œuvres de la loi, ou par l'audition de la foi?
6 Abraham “Alimwamini Mungu akahesabiwa kuwa mwenye haki”.
De même, Abraham « crut à Dieu, et cela lui fut compté pour justice ».
7 Kwa namna ile ile eleweni kwamba, wale ambao wanaamini ni watoto wa Abrahamu.
Sachez donc que ceux qui ont la foi sont enfants d'Abraham.
8 Andiko lilitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa mataifa kwa njia ya imani. Injili ilihubiriwa kwanza kwa Abrahamu: “katika wewe mataifa yote yatabarikiwa”.
L'Écriture, prévoyant que Dieu justifierait les païens par la foi, a annoncé d'avance la Bonne Nouvelle à Abraham, en disant: « En toi toutes les nations seront bénies. »
9 Ili baadaye wale ambao wana imani wabarikiwe pamoja na Abrahamu, ambaye alikuwa na imani.
Ainsi donc, ceux qui ont la foi sont bénis avec le fidèle Abraham.
10 Wale ambao wanategemea matendo ya sheria wako chini ya laana. Kwa kuwa imeandikwa, “Amelaaniwa kila mtu ambaye hashikamani na mambo yote yaliyoandikwa katika kitabu cha sheria, kuyatenda yote.”
Car tous ceux qui pratiquent les œuvres de la loi sont sous la malédiction. Car il est écrit: « Maudit est quiconque ne met pas en pratique tout ce qui est écrit dans le livre de la loi. »
11 Sasa ni wazi kwamba Mungu hamhesabii haki hata mmoja kwa sheria, kwa kuwa “Mwenye haki ataishi kwa imani”.
Or, il est évident que nul n'est justifié devant Dieu par la loi, car il est écrit: « Le juste vivra par la foi. »
12 Sheria haitokani na imani, lakini badala yake “Ambaye hufanya mambo haya katika sheria, ataishi kwa sheria.”
La loi n'est pas de la foi, mais: « L'homme qui les met en pratique vivra par elles. »
13 Kristo alitukomboa sisi kutoka katika laana ya sheria wakati alipofanyika laana kwa ajili yetu. Kwa kuwa imeandikwa, “Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti.”
Le Christ nous a rachetés de la malédiction de la loi, étant devenu malédiction pour nous. Car il est écrit: « Maudit est quiconque est pendu à un arbre »,
14 Lengo lilikuwa kwamba, baraka ambazo zilikuwa kwa Ibrahimu zingekuja kwa watu wa mataifa katika Kristo Yesu, ili kwamba tuweze kupokea ahadi ya Roho kupitia imani.
afin que la bénédiction d'Abraham vienne sur les païens par Jésus-Christ, pour que nous recevions par la foi la promesse de l'Esprit.
15 Ndugu, ninazungumza kwa namna ya kibinadamu. Hata wakati ambapo agano la kibinadamu limekwisha kuwekwa imara, hakuna awezaye kupuuza au kuongezea.
Frères, en termes humains, bien qu'il ne s'agisse que d'une alliance d'homme, quand elle a été confirmée, personne ne l'annule ni n'y ajoute.
16 Sasa ahadi zilisemwa kwa Ibrahim na kwa kizazi chake. Haisemi, “kwa vizazi,” kumaanisha wengi, bali badala yake kwa mmoja pekee, “kwa kizazi chako,” ambaye ni Kristo.
Or les promesses ont été faites à Abraham et à sa descendance. Il ne dit pas: « A une descendance", comme à plusieurs, mais comme à un seul: « A ta descendance », qui est le Christ.
17 Sasa nasema hivi, sheria ambayo ilikuja miaka 430 baadaye, haiondoi agano la nyuma lililowekwa na Mungu.
Or je dis ceci: Une alliance confirmée d'avance par Dieu en Christ, la loi, qui est venue quatre cent trente ans après, ne l'annule pas, au point de rendre la promesse sans effet.
18 Kwa kuwa kama urithi ungelikuja kwa njia ya sheria, usingekuwa tena umekuja kwa njia ya ahadi. Lakini Mungu aliutoa bure kwa Ibrahimu kwa njia ya ahadi.
Car si l'héritage vient de la loi, il ne vient plus de la promesse; mais Dieu l'a accordé à Abraham par promesse.
19 Kwa nini sasa sheria ilitolewa? Iliongezwa kwa sababu ya makosa, mpaka mzao wa Ibrahimu aje kwa wale ambao kwao alikuwa ameahidiwa. Sheria iliwekwa katika shinikizo kupitia malaika kwa mkono wa mpatanishi.
Alors pourquoi la loi existe-t-elle? Elle a été ajoutée à cause des transgressions, jusqu'à ce que vienne la descendance à laquelle la promesse a été faite. Elle a été ordonnée par des anges, par la main d'un médiateur.
20 Sasa mpatanishi humaanisha zaidi ya mtu mmoja, bali Mungu ni mmoja peke yake.
Or, il n'y a pas de médiateur entre les uns et les autres, mais Dieu est unique.
21 Kwa hiyo je sheria iko kinyume na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa kuwa kama sheria iliyokuwa imetolewa ilikuwa na uwezo wa kuleta uzima, haki ingepatikana kwa sheria.
La loi est-elle donc contre les promesses de Dieu? Certainement pas! Car s'il avait été donné une loi qui pût faire vivre, très certainement la justice aurait été de la loi.
22 Lakini badala yake, andiko limefunga mambo yote chini ya dhambi. Mungu alifanya hivi ili kwamba ahadi yake ya kutuokoa sisi kwa imani katika Yesu Kristo iweze kupatikana kwa wale wanao amini.
Mais l'Écriture a emprisonné toutes choses sous le péché, afin que la promesse par la foi en Jésus-Christ soit accordée à ceux qui croient.
23 Lakini kabla ya imani katika Kristo haijaja, tulikuwa tumefungwa na kuwa chini ya sheria hadi uje ufunuo wa imani.
Mais avant que la foi ne vienne, nous étions gardés sous la loi, enfermés pour la foi qui devait être révélée ensuite.
24 Kwa hiyo sheria ilifanyika kiongozi wetu hadi Kristo alipokuja, ili kwamba tuhesabiwe haki kwa imani.
De sorte que la loi est devenue notre précepteur pour nous amener au Christ, afin que nous soyons justifiés par la foi.
25 Sasa kwa kuwa imani imekuja, hatuko tena chini ya mwangalizi.
Mais maintenant que la foi est venue, nous ne sommes plus sous un tuteur.
26 Kwa kuwa ninyi nyote ni watoto wa Mungu kupitia imani katika Kristo Yesu.
Car vous êtes tous enfants de Dieu, par la foi en Jésus-Christ.
27 Wote ambao mlibatizwa katika Kristo mmejivika Kristo.
Car tous ceux d'entre vous qui ont été baptisés dans le Christ ont revêtu le Christ.
28 Hakuna Myahudi wala Myunani, mtumwa wala huru, mwanaume wala mwanamke, kwa kuwa ninyi nyote ni mmoja katika Kristo Yesu.
Il n'y a plus ni Juif ni Grec, il n'y a plus ni esclave ni homme libre, il n'y a plus ni homme ni femme, car vous êtes tous un en Jésus-Christ.
29 Kama ninyi ni wa Kristo, basi ni uzao wa Ibrahimu, warithi kwa mujibu wa ahadi.
Si vous appartenez au Christ, vous êtes donc la postérité d'Abraham et les héritiers selon la promesse.

< Wagalatia 3 >