< Ezra 3 >

1 Ilikuwa miezi saba baaada ya watu wa Israeli kurudi kwenye miji yao, ndipo walipojikusanya pamoja kama mtu mmoja katika Yerusalem.
And the seventh month cometh, and the sons of Israel [are] in the cities, and the people are gathered, as one men, unto Jerusalem.
2 Yeshua mwana wa Yosadaki na kaka yake kuhani, na Zerubabeli mwana wa Sheatieli na kaka yake wakainuka na kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli na kutoa sadaka ya kuteketezwa kama ilivyoagizwa katika sheria ya Musa, Mtu wa Mungu.
And rise doth Jeshua son of Jozadak, and his brethren the priests, and Zerubbabel son of Shealtiel, and his brethren, and they build the altar of the God of Israel, to cause to ascend upon it burnt-offerings, as it is written in the law of Moses, the man of God.
3 Ndipo wakaanzisha madhabahu juu ya msingi, kwa hofu waliokuwa nayo kwa sababu ya watu wa nchi/ Wakatoa sadaka ya kuteketezwa kwa Yahwe asubuhi na jioni.
And they establish the altar on its bases, because of the fear upon them of the peoples of the lands, and he causeth burnt-offerings to ascend upon it to Jehovah, burnt-offerings for the morning and for the evening.
4 Pia vilevile wakaichunguza sikukuu ya vibanda kama ilivyoandikwa na wakatoa sadaka ya kuteketezwa siku kwa siku kama ilivyoagizwa, kila siku kwa siku yake.
And they make the feast of the booths as it is written, and the burnt-offering of the day daily in number according to the ordinance, the matter of a day in its day;
5 Kulikuwa na sadaka ya kila siku ya kuteketezwa na mwezi mara moja na sadaka za siku ya Yahwe za kudumu, pamoja na sadaka zote za hiari.
and after this a continual burnt-offering, and for new moons, and for all appointed seasons of Jehovah that are sanctified; and for every one who is willingly offering a willing-offering to Jehovah.
6 Walianza kutoa sadaka za kuteketezwa za Yahwe siku ya kwanza ya mwezi wa saba, ingawa hekalu lilikuwa halijaanza kujengwa.
From the first day of the seventh month they have begun to cause burnt-offerings to ascend to Jehovah, and the temple of Jehovah hath not been founded,
7 Hivyo wakatoa fedha kwa wahunzi na fundi wa mkono, na wakawapa chakula, vinywaji na mafuta kwa watu wa Sidoni na Tiro, ili kwamba walete miti ya mierezi kupitia baharini kutoka Lebanoni mpaka Yafa, na kama walivyo ruhusiwa na mfalme Koreshi wa Uajemi.
and they give money to hewers and to artificers, and food, and drink, and oil to Zidonians and to Tyrians, to bring in cedar-trees from Lebanon unto the sea of Joppa, according to the permission of Cyrus king of Persia concerning them.
8 Ndipo mwezi wa pili katika mwaka wa pili baadae wakaja kwenye nyumba ya Mungu Yerusalem, Zerubabeli, Yoshua mwana wa Yosadaki, na baadhi ya makuhani na walawi na wale walikuja kutoka uhamishoni kurudi Yerusalem wakaanza kazi. Wakawachagua walawi walikuwa na miaka ishirini na zaidi kusimamia kazi ya nyumba ya Yahwe,
And in the second year of their coming in unto the house of God, to Jerusalem, in the second month, began Zerubbabel son of Shealtiel, and Jeshua son of Jozadak, and the remnant of their brethren the priests and the Levites, and all those coming from the captivity to Jerusalem, and they appoint the Levites from a son of twenty years and upward, to overlook the work of the house of Jehovah.
9 Yoshua akamsimamisha kijana wake na kaka yake, Kadmiel na watoto wake, na kizazi cha yuda kusimamia kufanya kazi katika nyumba ya Mungu. Pamoja na wao kulikuwa na wana wa Henadadi, na uzao wao, na pia jamaa zao walawi.
And Jeshua standeth, [and] his sons, and his brethren, Kadmiel and his sons, sons of Judah together, to overlook those doing the work in the house of God; the sons of Henadad, [and] their sons and their brethren the Levites.
10 Wajenzi wakasimamisha msingi wa Hekalu la Yahwe, Na hii ikawawezesha makuhani kusimama na mavazi yao wakiwa na tarumbeta, na walawi wana wa Asafu, kumtukuza Yahwe kwa matoazi, kama mkono wa mfalme Daudi wa Israel alivyoagiza.
And those building have founded the temple of Jehovah, and they appoint the priests, clothed, with trumpets, and the Levites, sons of Asaph, with cymbals, to praise Jehovah, by means of [the instruments of] David king of Israel.
11 Waliimba kwa kumsifu na kumshukuru Yahwe. “Yeye ni mwema! Agano lake ni kweli kwa Israel ladumu milele.”Watu wote wakapiga kelele kwa sauti kuu za shangwe wakimsifu Yahwe kwa sababu misingi ya Hekalu ilikuwa imekamilika.
And they respond in praising and in giving thanks to Jehovah, for good, for to the age His kindness [is] over Israel, and all the people have shouted — a great shout — in giving praise to Jehovah, because the house of Jehovah hath been founded.
12 Lakini wengi wa Makuhani, walawi, wakuu wa kale, na wazeee wa zamani walioiona nyumba ya kwanza, wakati misingi ilipowekwa wakaishuhudia kwa macho yao, walilia kwa sauti. Lakiniwengi walipiga kelele kwa sauti za shangwe na furaha na sauti za kushangaza.
And many of the priests, and the Levites, and the heads of the fathers, the aged men who had seen the first house — in this house being founded before their eyes — are weeping with a loud voice, and many with a shout, in joy, lifting up the voice;
13 Na matokeo yake, watu hawakuweza kutofautisha sauti za furaha na sauti za shangwe na sauti za watu waliokuwa wanalia, kwa kuwa watu walikuwa wanalia kwa sauti kuu ya shangwe na sauti ilisikika kutoka mbali.
and the people are not discerning the noise of the shout of joy from the noise of the weeping of the people, for the people are shouting — a great shout — and the noise hath been heard unto a distance.

< Ezra 3 >