< Ezra 10 >

1 Wakati Ezra akiomba na kutubu, akalia na kujirusha chini mbele ya nyumba ya Mungu, kusanyiko kubwa la wanaume Israel, wanawake na watoto wakakusanyika kwake, kwa kuwa watu walikuwa wakilia sana.
Now while Ezra prayed, and made confession, weeping and casting himself down before the house of God, there was gathered together unto him out of Israel a very great congregation of men and women and children: for the people wept very sore.
2 Shekania mtoto wa Yehieli, mwana wa Elamu akamwambia Ezra, “Tumekuwa sio waaminifu kwa Mungu na tumeoa wanawake wa kigeni kutoka nchi nyingine. Lakini pamoja na hilo, bado kuna tumaini kwa Israel.
And Shecaniah the son of Jehiel, one of the sons of Elam, answered and said unto Ezra, We have trespassed against our God, and have married strange women of the peoples of the land: yet now there is hope for Israel concerning this thing.
3 sasa natuweke agano pamoja na Mungu wetu kuwaondoa wanawake wote na watoto wao kulingana na maelekezo ya Bwana, na maelekezo ya wale wanaotetemeka kutokana na amri za Mungu wetu. na hii ifanyike kutokana na sheria.
Now therefore let us make a covenant with our God to put away all the wives, and such as are born of them, according to the counsel of my lord, and of those that tremble at the commandment of our God; and let it be done according to the law.
4 Simama, jambo hili linakuhusu wewe, na sisis tuko pamoja na wewe, Uwe imara na kufanya hili.
Arise; for the matter belongeth unto thee, and we are with thee: be of good courage, and do it.
5 Hivyo Ezra akasimama na kufanya makuhani na walawi na waisrael wote wakaahidi kufanya kwa njia hiyo. Hivyo wote wakatoa kiapo.
Then arose Ezra, and made the chiefs of the priests, the Levites, and all Israel, to swear that they would do according to this word. So they sware.
6 Ndipo Ezra akainuka kutoka mbele ya nyumba ya Mungu na kwenda kwenye chumba ya Yehohanani mtoto wa Eliashibu, Yeye hakula mkate au kunywa maji. Tangu alipokuwa akiomboleza kuhusiana na wale wenye imani haba waliokuwa uhamishoni.
Then Ezra rose up from before the house of God, and went into the chamber of Jehohanan the son of Eliashib: and [when] he came thither, he did eat no bread, nor drink water: for he mourned because of the trespass of them of the captivity.
7 Hivyo wakatuma neno katika Yuda na Yerusalem kwa watu wote waliorudi kutoka utumwani kukusanyika Yerusalem.
And they made proclamation throughout Judah and Jerusalem unto all the children of the captivity, that they should gather themselves together unto Jerusalem;
8 Yeyote ambaye hakuja katika siku tatu kutokana na maelekezo kutoka kwa wakuu na viongozi atachukuliwa mali zote na atatengwa na kusanyiko kuu la watu ambao walikuja kutoka uhamisho.
and that whosoever came not within three days, according to the counsel of the princes and the elders, all his substance should be forfeited, and himself separated from the congregation of the captivity.
9 Hivyo watu wote wa Yuda na Benjamini wakakusanyika Yerusalem kwa siku tatu. Ilikuwa ni mwezi wa tisa na siku ya ishirini ya mwezi. watu wote wakasimama mbele ya nyumba ya Mungu na wakatetemeka kwa sababu ya neno na mvua.
Then all the men of Judah and Benjamin gathered themselves together unto Jerusalem within the three days; it was the ninth month, on the twentieth [day] of the month: and all the people sat in the broad place before the house of God, trembling because of this matter, and for the great rain.
10 Ezra kuhani akasimama na kusema, “Ninyi wenyewe mmefanya uasi, ninyi mmeishi na wanawake wa kigeni na kuongeza makosa ya Israel.
And Ezra the priest stood up, and said unto them, Ye have trespassed, and have married strange women, to increase the guilt of Israel.
11 Lakini sasa mpeni sifa Yahwe, Mungu wa watangulizi wenu, na mfanye mapenzi yake, mjitenge na watu wa nchi na wanawake wa kigeni.
Now therefore make confession unto the LORD, the God of your fathers, and do his pleasure: and separate yourselves from the peoples of the land, and from the strange women.
12 Kusanyiko lote likajibu kwa sauti. “Tutatenda kama ulivyosema,
Then all the congregation answered and said with a loud voice, as thou hast said concerning us, so must we do.
13 haijalishi, kuna watu wengi na ni kipindi cha mvua. Hatuna nguvu ya kusimama nje na hii si siku moja au mbili za kufanya kazi, kwa kuwa tumekosea katika jambo hili.
But the people are many, and it is a time of much rain, and we are not able to stand without, neither is this a work of one day or two: for we have greatly transgressed in this matter.
14 Hivyo wakuu wetu wawakilishe kusanyiko lote, iwe kwamba wote walioruhusu wanawake wa kigeni kuishi katika miji yetu waje katika muda uliopangwa na viongozi wa mji na waamuzi wa mji hadi hapo hasira ya Mungu itakapoondoka kutoka kwetu.
Let now our princes be appointed for all the congregation, and let all them that are in our cities which have married strange women come at appointed times, and with them the elders of every city, and the judges thereof, until the fierce wrath of our God be turned from us, until this matter be despatched.
15 Yonathan mtoto Asaheli na Yazeya mwana wa Tikwa wakapinga hili, Meshulamu na Shabethai mlawi wakawaunga mkono wao.
Only Jonathan the son of Asahel and Jahzeiah the son of Tikvah stood up against this [matter]: and Meshullam and Shabbethai the Levite helped them.
16 Hivyo watu waliotoka uhamishoni wakafanya hivi, Ezra kuhani akachagua wanaume, viongozi watamgulizi wa ukoo na nyumba, wao wote kwa majina na wakaliangalia suala hili siku ya kwanza ya mwezi wa kumi.
And the children of the captivity did so. And Ezra the priest, [with] certain heads of fathers’ [houses], after their fathers’ houses, and all of them by their names, were separated; and they sat down in the first day of the tenth month to examine the matter.
17 Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakawa wamemaliza kuchunguza wale wanaume walioishi na wanawake wa kigeni.
And they made an end with all the men that had married strange women by the first day of the first month.
18 Miongoni mwa wana wa kikuhani kuna wale walioishi na wanawake wa kigeni. Miongoni mwa wana wa Yoshua mtoto wa Yosadaki na kaka zake ambao walikuwa Maasela, Eliazeri, na Yaribu na Gedalia.
And among the sons of the priests there were found that had married strange women: [namely], of the sons of Jeshua, the son of Jozadak, and his brethren, Maaseiah, and Eliezer, and Jarib, and Gedaliah.
19 Hivyo wakaamua kuwaondoa wake zao. kwa kuwa walikuwa na makosa, wakatoa sadaka ya kondoo kwenye mifugo kwa ajili ya makosa yao.
And they gave their hand that they would put away their wives; and being guilty, [they offered] a ram of the flock for their guilt.
20 Miongoni mwa wana wa Imeri, Hanani, na Zebadia.
And of the sons of Immer; Hanani and Zebadiah.
21 Miongoni mwa wana wa Harimu, Maaseya, na Eliya na Shemaya, na Yehieli na Uzia.
And of the sons of Harim; Maaseiah, and Elijah, and Shemaiah, and Jehiel, and Uzziah.
22 Miongoni mwa wana wa Pashuri, Elasa
And of the sons of Pashhur; Elioenai, Maaseiah, Ishmael, Nethanel, Jozabad, and Elasah.
23 Miongoni mwa walawi: Yozabadi na Shimei na Kelaya (ndiye Kelita) na Pethaia, na Yuda na Eliezeri. Miongoni mwa waimbaji Eliashibu na. Miongoni mwa walinzi Shalumu, Telemu na Uri.
And of the Levites; Jozabad, and Shimei, and Kelaiah (the same is Kelita), Pethahiah, Judah, and Eliezer.
24 Miongoni mwa Israel waliobaki -
And of the singers; Eliashib; and of the porters; Shallum, and Telem, and Uri.
25 Miongoni mwa wana wa Paroshi, Ramia na Izia na Malkiya na Miyamini na Eliazari na Malkiya na Benaya
And of Israel: of the sons of Parosh; Ramiah, and Izziah, and Malchijah, and Mijamin, and Eleazar, and Malchijah, and Benaiah.
26 Miongoni mwa wana wa Elamu Mataniana Zekaria, na yeehieli, na Abdi na Yeremothi na Eliya.
And of the sons of Elam; Mattaniah, Zechariah, and Jehiel, and Abdi, and Jeremoth, and Elijah.
27 Miongoni mwa wana wa Zatu: Elionai, na Eliashibu, na Matania na Yeremothi na Zabadi na Aziza.
And of the sons of Zattu; Elioenai, Eliashib, Mattaniah, and Jeremoth, and Zabad, and Aziza.
28 Miongoni mwa wana wa Bebai Yehohanani, na Hanania na Zakai na Athlai.
And of the sons of Bebai; Jehohanan, Hananiah, Zabbai, Athlai.
29 Miongoni mwa wana wa bani: Meshulami na Maluki, na Adaya na Yashubu na Sheali na Yeremothi.
And of the sons of Bani; Meshullam, Malluch, and Adaiah, Jashub, and Sheal, Jeremoth.
30 Miongoni mwa wana wa Pahath-Moabu, Adna, na kelali, na Benaya na Maaseya, na Matania, na Besaleli na Binti na Manase.
And of the sons of Pahath-moab; Adna, and Chelal, Benaiah, Maaseiah, Mattaniah, Bezalel, and Binnui, and Manasseh.
31 Na miongoni mwa wana wa Harimu: Eliezeri na Ishiya, na Malkiya na Shemaya na Shimeoni, na
And [of] the sons of Harim; Eliezer, Isshijah, Malchijah, Shemaiah, Shimeon;
32 Benyamini na Maluki na Shemaria
Benjamin, Malluch, Shemariah.
33 Miongoni mwa wana Hashumu: Matenai, na Matatana Zabadi, na Elifereti na Yeremai, na Manase, na Shimei.
Of the sons of Hashum; Mattenai, Mattattah, Zabad, Eliphelet, Jeremai, Manasseh, Shimei.
34 Miongoni mwa wana wa Bani: Maadai, na Amramu na Aueli, na
Of the sons of Bani; Maadai, Amram, and Uel;
35 Benaya, na Bedeya na Keluhi, na
Benaiah, Bedeiah, Cheluhi;
36 wania, na Meremothi, Eliashibu,
Vaniah, Meremoth, Eliashib;
37 Matania, na Matenai. na
Mattaniah, Mattenai, and Jaasu;
38 Yaasi. Miongoni mwa wana wa Binui: Shimei,
and Bani, and Binnui, Shimei;
39 Sheremia, na Nathani, na Adaya, na
and Shelemiah, and Nathan, and Adaiah;
40 Maknadebai, na Shashai, na Sharai
Machnadebai, Shashai, Sharai;
41 Azareri, na Sheremia, na Shemaria, na
Azarel, and Shelemiah, Shemariah;
42 Shalumu, na Amaria, na Yusufu.
Shallum, Amariah, Joseph.
43 Miongoni wa wana wa Nebo: Yeieli, na Mathiana zabadi, na Zebina, na Ido, na Yoeli na Benaya.
Of the sons of Nebo; Jeiel, Mattithiah, Zabad, Zebina, Iddo, and Joel, Benaiah.
44 Hawa wote walikuwa wameoa wanawake wa kigeni na walikuwa wamezaa watoto baadhi yao.
All these had taken strange wives: and some of them had wives by whom they had children.

< Ezra 10 >