< Ezekieli 8 >

1 Hivyo ikawa kuhusu katika mwaka wa sita na mwezi wa sita, katika siku ya tano ya mwezi, nilipokuwa nimeketi kwenye nyumba yangu na wazee wa Yuda waliketi mbele yangu, kwamba mkono wa Bwana Yahwe ukanijaza juu yangu huko.
And it cometh to pass, in the sixth year, in the sixth [month], in the fifth of the month, I am sitting in my house, and elders of Judah are sitting before me, and fall on me there doth a hand of the Lord Jehovah,
2 Hivyo nikaona, na tazama, kulikuwa na mfano kama mwonekano wa mwanadamu. Kutoka kwenye mwonekano wake wa nyonga kwenda chini kulikuwa na moto. Na kutoka kwenye nyonga kwenda juu kulikuwa na mwonekano wa kitu kinachong'aa, kama mng'ao wa chuma.
and I look, and lo, a likeness as the appearance of fire, from the appearance of His loins and downward — fire, and from His loins and upward, as the appearance of brightness, as the colour of copper.
3 Kisha akanyoosha kutoka kwenye mkono na kunichukua kwa nywele za kichwa changu; Roho akaniacha juu kati ya dunia na mbingu, na katika maono kutoka kwa Mungu, akaniletea hata Yerusalemu, kwenye mlango wa kuingia ndani ya lango la kaskazini, ambako sanamu ile iletayo wivu mkubwa ilipokuwa imesiamama.
And He putteth forth a form of a hand, and taketh me by a lock of my head, and lift me up doth a spirit between the earth and the heavens, and it bringeth me in to Jerusalem in visions of God, unto the opening of the inner gate that is facing the north, where [is] the seat of the figure of jealousy that is making jealous,
4 Kisha tazama, utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa huko, kulingana na ono nililokuwa nimeliona kwenye uwanda.
and lo, there the honour of the God of Israel, as the appearance that I saw in the valley.
5 Kisha akanambia, “Mwanadamu, inua juu macho yako kwenda upande wa kaskazini.” Hivyo nikainua macho yangu kuelekea kaskazini, na kwenye lango la kaskazini kulekea kwenye madhabahu, huko kwenye lango la kuingilia, kulikuwa na sanamu ya wivu.
And He saith unto me, 'Son of man, lift up, I pray thee, thine eyes the way of the north.' And I lift up mine eyes the way of the north, and lo, on the north of the gate of the altar this figure of jealousy, at the entrance.
6 Hivyo akanambia, “Mwanadamu, unaona wanayoyafanya? Haya ni machukizo makubwa ambayo nyumba ya Israeli wanayoyafanya hapa kunifanya niende mbali kutoka patakatifu pangu. Lakini utageuka na kuona machukizo makubwa zaidi.”
And He saith unto me, 'Son of man, art thou seeing what they are doing? the great abominations that the house of Israel are doing here, to keep far off from My sanctuary; and again thou dost turn, thou dost see great abominations.'
7 Kisha akanileta hata kwenye mlango wa uzio, na nikatazama, kulikuwa na shimo kwenye ukuta.”
And He bringeth me in unto an opening of the court, and I look, and lo, a hole in the wall;
8 Akanambia, “Mwanadamu, chimba kwenye huu ukuta.” Basi nikachimba kwenye huo ukuta, na kulikuwa na mlango.
and He saith unto me, 'Son of man, dig, I pray thee, through the wall;' and I dig through the wall, and lo, an opening.
9 Kisha akanambia, “Nenda na ukaone machukizo ya uovu ambayo wanayoyafanya hapa.”
And He saith to me, 'Go in, and see the evil abominations that they are doing here.'
10 Basi nilipokuwa nikienda ndani na nikaona, na tazama! Kulikuwa na kila umbo la vitu vikitembea polepole na mnyama achukizaye sana! Kila sanamu wa nyumba ya Israeli ilikuwa imechongwa kwenye ukuta pande zote.
And I go in, and look, and lo, every form of creeping thing, and detestable beast — and all the Idols of the house of Israel — graved on the wall, all round about,
11 Wazee sabini wa wa nyumba ya Israeli walikuwa huko, na Yaazania mwana wa Shafani alikuwa amesimama katikati yao. Walikuwa wamesimama mbele ya picha, na kila mtu alikuwa na chetezo kwenye mkono wake ili kwamba harufu ya ubani ingeweza kupanda juu.
and seventy men of the elders of the house of Israel — and Jaazaniah son of Shaphan standing in their midst — are standing before them, and each his censer in his hand, and the abundance of the cloud of perfume is going up.
12 Akanambia, “mwanadamu, unaona kile ambacho wazee wa nyumba ya Israeli wanachokifanya kwenye giza? Kila mmoja hufanya hivi kwenye chumba cha sanamu yake, kwa kuwa husema, 'Yahwe hatuone! Yahwe ameitelekeza hii nchi.”'
And He saith unto me, 'Hast thou seen, son of man, that which elders of the house of Israel are doing in darkness, each in the inner chambers of his imagery, for they are saying, Jehovah is not seeing us, Jehovah hath forsaken the land?'
13 Kisha akanambia, “Geuka tena na tazama machukizo makubwa ambayo wanayoyafanya.”
And He saith unto me, 'Again thou dost turn, thou dost see great abominations that they are doing.'
14 Tena akanileta kwenye lango la kuingia la nyumba ya Yahwe lililokuwa upande waa kaskazini, na tazama! Wanawake walikuwa wameketi huko wakimlilia Tamuzi.
And He bringeth me in unto the opening of the gate of the house of Jehovah that [is] at the north, and lo, there the women are sitting weeping for Tammuz.
15 Hivyo akanambia, “Umeiona hii, mwanadamu? Geuka tena na uone machukizo makubwana zaidi kuliko hayo.”
And He saith unto me, 'Hast thou seen, son of man? again thou dost turn, thou dost see greater abominations than these.'
16 Akanileta hata kwenye uzio wa ndani wa nyumba ya Yahwe, na tazama! huko kwenye lango la kuingia kwenye madhabahu, kulikuwa na takribani watu ishirini na tano waliokuwa wamelipa mgongo hekalu la Yahwe na nyuso zao kuelekea mashariki, na walikuwa wakiabudu jua.
And He bringeth me in unto the inner court of the house of Jehovah, and lo, at the opening of the temple of Jehovah, between the porch and the altar, about twenty-five men, their backs toward the temple of Jehovah, and their faces eastward, and they are bowing themselves eastward to the sun.
17 Akanambia, “Unaona hii, mwanadamu? Je ni kitu kidigo kwa ajili ya nyumba ya Yuda kufanya haya machukizo wanayoyafanya? Kwa kuwa wameijaza nchi kwa uovu na wamerudi tena ili kuniletea hasira, kuweka tawi kwenye pua zao.
And He saith unto me, 'Hast thou seen, son of man? hath it been a light thing to the house of Judah to do the abomination that they have done here, that they have filled the land with violence, and turn back to provoke Me to anger? and lo, they are putting forth the branch unto their nose!
18 Hivyo nitatenda miongoni mwao pia; jicho langu halitakuwa na huruma, sitaacha kuwaharibu. hata watalia kwenye masikio yangu kwa sauti kubwa, sitawasikia.”
And I also deal in fury, Mine eye doth not pity, nor do I spare, and they have cried in Mine ears — a loud voice — and I do not hear them.'

< Ezekieli 8 >