< Ezekieli 8 >

1 Hivyo ikawa kuhusu katika mwaka wa sita na mwezi wa sita, katika siku ya tano ya mwezi, nilipokuwa nimeketi kwenye nyumba yangu na wazee wa Yuda waliketi mbele yangu, kwamba mkono wa Bwana Yahwe ukanijaza juu yangu huko.
Now in the sixth year, in the sixth month, on the fifth day of the month, when I was in my house and the responsible men of Judah were seated before me, the hand of the Lord came on me there.
2 Hivyo nikaona, na tazama, kulikuwa na mfano kama mwonekano wa mwanadamu. Kutoka kwenye mwonekano wake wa nyonga kwenda chini kulikuwa na moto. Na kutoka kwenye nyonga kwenda juu kulikuwa na mwonekano wa kitu kinachong'aa, kama mng'ao wa chuma.
And looking, I saw a form like fire; from the middle of his body and down there was fire: and up from the middle of his body a sort of shining, like electrum.
3 Kisha akanyoosha kutoka kwenye mkono na kunichukua kwa nywele za kichwa changu; Roho akaniacha juu kati ya dunia na mbingu, na katika maono kutoka kwa Mungu, akaniletea hata Yerusalemu, kwenye mlango wa kuingia ndani ya lango la kaskazini, ambako sanamu ile iletayo wivu mkubwa ilipokuwa imesiamama.
And he put out the form of a hand and took me by the hair of my head; and the wind, lifting me up between the earth and the heaven, took me in the visions of God to Jerusalem, to the way into the inner door facing to the north; where was the seat of the image of envy.
4 Kisha tazama, utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa huko, kulingana na ono nililokuwa nimeliona kwenye uwanda.
And I saw the glory of the Lord there, as in the vision which I saw in the valley.
5 Kisha akanambia, “Mwanadamu, inua juu macho yako kwenda upande wa kaskazini.” Hivyo nikainua macho yangu kuelekea kaskazini, na kwenye lango la kaskazini kulekea kwenye madhabahu, huko kwenye lango la kuingilia, kulikuwa na sanamu ya wivu.
Then he said to me, Son of man, now let your eyes be lifted up in the direction of the north; and on looking in the direction of the north, to the north of the doorway of the altar, I saw this image of envy by the way in.
6 Hivyo akanambia, “Mwanadamu, unaona wanayoyafanya? Haya ni machukizo makubwa ambayo nyumba ya Israeli wanayoyafanya hapa kunifanya niende mbali kutoka patakatifu pangu. Lakini utageuka na kuona machukizo makubwa zaidi.”
And he said to me, Son of man, do you see what they are doing? even the very disgusting things which the children of Israel are doing here, causing me to go far away from my holy place? but you will see other most disgusting things.
7 Kisha akanileta hata kwenye mlango wa uzio, na nikatazama, kulikuwa na shimo kwenye ukuta.”
And he took me to the door of the open place; and looking, I saw a hole in the wall.
8 Akanambia, “Mwanadamu, chimba kwenye huu ukuta.” Basi nikachimba kwenye huo ukuta, na kulikuwa na mlango.
And he said to me, Son of man, make a hole in the wall: and after making a hole in the wall I saw a door.
9 Kisha akanambia, “Nenda na ukaone machukizo ya uovu ambayo wanayoyafanya hapa.”
And he said to me, Go in and see the evil and disgusting things which they are doing here.
10 Basi nilipokuwa nikienda ndani na nikaona, na tazama! Kulikuwa na kila umbo la vitu vikitembea polepole na mnyama achukizaye sana! Kila sanamu wa nyumba ya Israeli ilikuwa imechongwa kwenye ukuta pande zote.
So I went in and saw; and there every sort of living thing which goes flat on the earth, and unclean beasts, and all the images of the children of Israel, were pictured round about on the wall.
11 Wazee sabini wa wa nyumba ya Israeli walikuwa huko, na Yaazania mwana wa Shafani alikuwa amesimama katikati yao. Walikuwa wamesimama mbele ya picha, na kila mtu alikuwa na chetezo kwenye mkono wake ili kwamba harufu ya ubani ingeweza kupanda juu.
And before them seventy of the responsible men of the children of Israel had taken their places, every man with a vessel for burning perfumes in his hand, and in the middle of them was Jaazaniah, the son of Shaphan; and a cloud of smoke went up from the burning perfume.
12 Akanambia, “mwanadamu, unaona kile ambacho wazee wa nyumba ya Israeli wanachokifanya kwenye giza? Kila mmoja hufanya hivi kwenye chumba cha sanamu yake, kwa kuwa husema, 'Yahwe hatuone! Yahwe ameitelekeza hii nchi.”'
And he said to me, Son of man, have you seen what the responsible men of the children of Israel do in the dark, every man in his room of pictured images? for they say, The Lord does not see us; the Lord has gone away from the land.
13 Kisha akanambia, “Geuka tena na tazama machukizo makubwa ambayo wanayoyafanya.”
Then he said to me, You will see even more disgusting things which they do.
14 Tena akanileta kwenye lango la kuingia la nyumba ya Yahwe lililokuwa upande waa kaskazini, na tazama! Wanawake walikuwa wameketi huko wakimlilia Tamuzi.
Then he took me to the door of the way into the Lord's house looking to the north; and there women were seated weeping for Tammuz.
15 Hivyo akanambia, “Umeiona hii, mwanadamu? Geuka tena na uone machukizo makubwana zaidi kuliko hayo.”
Then he said to me, Have you seen this, O son of man? you will see even more disgusting things than these.
16 Akanileta hata kwenye uzio wa ndani wa nyumba ya Yahwe, na tazama! huko kwenye lango la kuingia kwenye madhabahu, kulikuwa na takribani watu ishirini na tano waliokuwa wamelipa mgongo hekalu la Yahwe na nyuso zao kuelekea mashariki, na walikuwa wakiabudu jua.
And he took me into the inner square of the Lord's house, and at the door of the Temple of the Lord, between the covered way and the altar, there were about twenty-five men with their backs turned to the Temple of the Lord and their faces turned to the east; and they were worshipping the sun, turning to the east.
17 Akanambia, “Unaona hii, mwanadamu? Je ni kitu kidigo kwa ajili ya nyumba ya Yuda kufanya haya machukizo wanayoyafanya? Kwa kuwa wameijaza nchi kwa uovu na wamerudi tena ili kuniletea hasira, kuweka tawi kwenye pua zao.
Then he said to me, Have you seen this, O son of man? is it a small thing to the children of Judah that they do the disgusting things which they are doing here? for they have made the land full of violent behaviour, making me angry again and again: and see, they put the branch to my nose.
18 Hivyo nitatenda miongoni mwao pia; jicho langu halitakuwa na huruma, sitaacha kuwaharibu. hata watalia kwenye masikio yangu kwa sauti kubwa, sitawasikia.”
For this reason I will let loose my wrath: my eye will not have mercy, and I will have no pity.

< Ezekieli 8 >