< Ezekieli 43 >

1 Yule mtu kisha akanileta hata kwenye lango lililokuwa linaelekea mashariki.
The man then brought me to the gate that opened to the east.
2 Tazama! Utukufu wa Mungu wa Israeli ukaja kutoka mashariki; sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi, na nchi iling'aa kwa utukufu wake.
Behold! The glory of the God of Israel came from the east; his voice was like the sound of many waters, and the earth shone with his glory.
3 Yalikuwa yanalingana na sura ya ono nililolona, kulingana na ono nililokuwa nimeliona wakati alipokuja kuuteketeza mji, na maono yalikuwa kama maono ambayo niliyokuwa nimeyaona Keberi Kanali nikaanguka kifudi fudi.
It was according to the appearance of the vision that I saw, according to the vision that I saw when he had come to destroy the city, and the visions were like the vision that I saw at the Kebar Canal—and I fell to my face.
4 Hivyo utukufu wa Yahwe ukaja kwenye nyumba ya karibu na njia ya lango lililokuwa wazi kwa upande wa magharibi.
So the glory of Yahweh came to the house by way of the gate that opened to the east.
5 Kisha Roho akanichukua na kunileta kwenye ua wa ndanni. Tazama! Utukufu wa Yahwe ulikuwa umeijaza nyumba.
Then the Spirit lifted me up and brought me into the inner court. Behold! The glory of Yahweh was filling the house.
6 Mtu alisimama karibu na mimi, na nikamsikia mtu mwingine akizungumza na mimi kutoka kwenye nyumba.
The man was standing beside me, and I heard someone else speaking to me from the house.
7 Akanambia, “Mwanadamu, hapa ndipo mahali pangu pa enzi na mahali kwa ajili ya ya miguu yangu, ambapo nitaishi kati ya watu wa Israeli milele. Nyumba ya Israeli haitalikufuru tena jina langu takatifu-wao au wafalme wao katika mahali patakatifu pao.
He said to me, “Son of man, this is the place of my throne and the place for the soles of my feet, where I will live in the midst of the people of Israel forever. The house of Israel will no longer profane my holy name—they or their kings—with their faithlessness or with the corpses of their kings at their high places.
8 Hawatalikufuru tena jina langu takatifu kwa kuweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu, na nguzo yao ya lango karibu na nguzo yangu ya lango, bila kitu lakini ukuta kati yangu na wao. Wamelikufuru jina langu kwa matendo yao machafu, hivyo nimewala kwa hasira yangu.
They will no longer profane my holy name by putting their threshold next to my threshold, and their gateposts next to my gateposts, with nothing but a wall between me and them. They profaned my holy name with their disgusting actions, so I consumed them with my anger.
9 Sasa waache waondoe udanganyifu wao na maiti za wafalme wao kutoka kwangu, na nitaishi katikati yao milele.
Now let them remove their faithlessness and the corpses of their kings from before me, and I will live in their midst forever.
10 Mwanadamu, wewe mwenyewe utaiambia nyumba ya Israeli kuhusu nyumba hii hivyo watajiskia aibu ya uovu wao. Wanaweza kutafakari kuhusu haya maelezo.
Son of man, you yourself must tell the house of Israel about this house so they will be ashamed of their iniquities. They should think about this description.
11 Kwa kuwa wameaibika kwa yote waliyoyafanya, kisha waonyeshe mchoro wa nyumba, maelezo yake, matokeo yake, maingio yake, na mchoro wake, sheria zake zote na kanuni. Kisha andika hivi chini mbele ya macho yao ili waweze kutunza michoro yote na kanuni zake zote, hivyo kama wazitiivo.
For if they are ashamed of all that they have done, then reveal to them the design of the house, its details, its exits, its entrances, and all its designs, all its decrees and rules. Then write this down before their eyes so they will keep to all its design and all its rules, so as to obey them.
12 Hii ndiyo sheria kwa ajili ya nyumba: Kutoka kwenye kilele cha mlima hata mpaka wote unaoizunguka, patakuwa patakatifu sana. Tazama! Hii ndiyo sheria kwa ajili ya nyumba.
This is the regulation for the house: From the peak of the hill to all the surrounding border around it, it will be most holy. Behold! This is the regulation for the house.
13 Hivi vitakuwa vipimo vya madhabahu katika dhiraa-hiyo dhiraa kuwa dhiraa ya kawaida na urefu wa kiganja. Hivyo mfereji ulio uzunguka madhabahu utakuwa dhiraa moja chini, na upana wake pia utakuwa dhiraa moja. Mpaka wa karibu uizungukayo machinjio shubiri moja. Hii itakuwa kitako cha madhabahu.
These will be the measurements of the altar in cubits—that cubit being a regular cubit and a handbreadth in length. So the gutter around the altar will be a cubit deep, and its width will also be a cubit. The border around its surrounding edge will be one span. This will be the base of the altar.
14 Usawa wa kutoka kwenye mferji hadi kwenye machinijo ya chini ya madhabahu itakuwa dhiraa mbili, na hiyo machinjio yenyewe itakuwa dhiraa moja upana. Kisha kutoka machinjio madogo hadi kwenye machinjio makubwa ya madhabahu, itakuwa dhiraa nne, na machinjio makubwa yatakuwa dhraa moja upana.
From the gutter at the ground level up to the lower ledge of the altar is two cubits, and that ledge itself is one cubit in width. Then from the small ledge up to the large edge of the altar, it is four cubits, and the large edge is a cubit in width.
15 Meko juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa ni dhiraa nne juu, na kuna pembe nne zilizoelekea juu kwenye meku.
The hearth on the altar for the burnt offerings is four cubits high, and there are four horns pointing upward on the hearth.
16 Meku ina dhiraa kumi na moja urefu na dhiraa kumi na mbili upana, za mraba.
The hearth is twelve cubits in length and twelve cubits in width, a square.
17 Mpaka wake ni dhiraa kumi na nne urefu na dhiraa kumi na nne upana pande zake zote nne, na ukingo wake ni nusu dhiraa upana. Mfereji ni dhiraa moja upana kuzuka kote pamoja na ngazi zielekeazo mashariki.”
Its border is fourteen cubits in length and fourteen cubits in width on each of its four sides, and its rim is a half cubit in width. The gutter is a cubit in width all around with its steps facing east.”
18 Kisha akanambia, “Mwanadamu, Bwana Yahwe asema hivi: Hizi ndizo sheria kwa ajili ya madhabahu katika siku watakayoitengeza, kwa ajili kutoa sadaka ya kuteketezwa kwenye hiyo, na kwa jili ya kunyunyiza damu juu yake.
Next he said to me, “Son of man, the Lord Yahweh says this: These are the regulations for the altar on the day they make it, for raising the burnt offering onto it, and for sprinkling blood on it.
19 Utatoa ng'ombe kutoka kwenye kundi kama sadaka ya dhambi kwa ajili ya Walawi makuhani ambao ni uzao wa Zadoki, wale wajao karibu nami kunitumikia-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
You will give a bull from the cattle as a sin offering for the Levitical priests who are the descendants of Zadok, those who come near to me to serve me—this is the Lord Yahweh's declaration.
20 Kisha utachukua baadhi ya damu yake na kuiweka juu pembe nne za madhabahu na pande nne za machinjio na kuuzunguka ukingo; utaitakasa na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
Then you will take some of its blood and place it on the altar's four horns and the four sides of its edge and on the surrounding rim; you will cleanse it and make atonement for it.
21 Kisha chukua ng'ombe kama sadaka ya dhambi na iteketezwe katika eneneo lililotengwa la nje ya patakatifu.
Then take the bull for the sin offering and burn it in the appointed part of the temple area outside of the sanctuary.
22 Kisha katika siku ya pili utatoa mbuzi dume asiyekuwa na dosari kutoka kundini kama sadaka ya dhambi; makuhani wataisafisha madhabahu kama walivyoisafisha kwa ng'ombe.
Then on the second day you will offer a male goat without blemish from the goats as a sin offering; the priests will cleanse the altar just as they cleansed it with the bull.
23 Utakapomaliza kusafisha, toa ng'ombe asiyekuwa na dosari kutoka kwenye mifugo na kondoo dume asiyekuwa na dosari kutoka kundini.
When you finish its cleansing, offer an unblemished bull from the cattle and an unblemished ram from the flock.
24 Watoe mbele ya Yahwe; makuhani watanyunyiza chumvi juu yao na kuwainua juu kama sadaka ya kutekezwa kwa Yahwe.
Offer them before Yahweh; the priests will throw salt onto them and raise them up as a burnt offering to Yahweh.
25 Utaandaa mbuzi dume kama sadaka ya dhambi kila siku kwa mda wa siku saba, na makuhani pia wataandaa ng'ombe asiye na dosari kutoka kwenye kundi na kondoo dume kutoka kwenye kundi.
You must prepare a male goat as a sin offering daily for seven days, and the priests must also prepare an unblemished bull of the cattle and unblemished ram from the flock.
26 Wataipatanisha madhabahu kwa siku saba na kuitakasa, wataitakasa kwa njia hii.
They must atone for the altar for seven days and purify it, and in this way they must consecrate it.
27 Watamaliza hizi siku saba, na katika siku ya nane na kuendelea itakuwa kwamba makuhani wataandaa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani kwenye madhabahu, ndipo nitakapowakubali-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
They must complete these days, and on the eighth day and onward it will come about that the priests will prepare your burnt offerings and your peace offerings on the altar, and I will accept you—this is the Lord Yahweh's declaration.”

< Ezekieli 43 >