< Ezekieli 42 >

1 Kisha yule mtu akanituma kwenda ua wa nje upande wa kaskazini, akanileta kwenye vyumba mbele ya ua wa nje na ukuta wa nje kaskazini.
Next the man sent me out to the outer courtyard on the north side, and he brought me to rooms in front of the outer courtyard and the northern outer wall.
2 Hivyo vyumba vilikuwa dhiraa mia moja karibu na mbele yake na dhiraa hamsini upana.
Those rooms were one hundred cubits along their front and fifty cubits in width.
3 Baadhi ya hivyo vyumba vilielekea ua wa ndani na vilikuwa na dhiraa ishirini kutoka patakatifu. Kulikuwa na vyumba vitatu vinavyolingana, na kingine juu kilichokuwa kimetazama chini kuelekea kingine vilikuwa vimefunguliwa, vilikuwa na pakutokea. Baadhi ya vyumba vilielekea nje kwenye ua wa nje.
Some of those rooms faced the inner courtyard and were twenty cubits away from the sanctuary. There were three levels of rooms, and the ones above looked down on the ones below and were open to them, having a walkway. Some of the rooms looked out onto the outer courtyard.
4 Njia dhiraa kumi upana dhiraa mia moja urefu kueleikea mbele ya vyumba. Milango ya vyumba ilikuwa mbele kaskazini.
A passage ten cubits in width and one hundred cubits in length ran in front of the rooms. The rooms' doors were toward the north.
5 Lakini kumbi za juu zilikuwa ndogo, kwa ajili ya njia za kutembea zilichukua kutoka kwazo sehemu kubwa kulikuwa walivyofanya kwenye vyumba vya chini na katikati usawa wa jengo.
But the upper halls were smaller, for the walkways took away from them more space than they did in the lowest and middle levels of the building.
6 Kwa kuwa orofa tatu hapakuwa na mihimili, kama zile nyua, ambazo zilikuwa na mihimili. Hivyo usawa wa vyumba vya juu vilikuwa sawa sawa katika kipimo cha kulinganisha na vyumba vya chini na usawa wa katikakati.
For the halls on the third story had no columns, unlike the courtyards, which did have columns. So the highest level's rooms were smaller in size compared to the rooms in the lowest and middle levels.
7 Ukuta wa nje karibu na vyumba mbele ya ua wa nje, ua uliokuwa mbele ya vyumba. Huo ukuta ulikuwa dhiraa hamsini urefu.
The outside wall ran along the rooms toward the outer courtyard, the courtyard that was in front of the rooms. That wall was fifty cubits in length.
8 Urefu wa vyumba vya ua wa nje ulikuwa dhiraa hamsini, na vyumba vilivyokuwa vimeelekea patakatifu vilikuwa dhiraa mia moja urefu.
The length of the rooms of the outer courtyard was fifty cubits, and the rooms facing the sanctuary were one hundred cubits in length.
9 Kulikuwa na mahali pa kuingilia kwenye vyumba vidogo zaidi kutoka upande mashariki, kuingia kutoka ua wa nje.
There was an entrance to the lowest rooms from the east side, coming from the outer courtyard.
10 Karibu na ukuta wa ua wa nje juu ya upande wa mgaribi pa ua wa ndani, mbele ya patakatifu pa ua wa nje, pia kulikuwa na vyumba na njia ya mbele yao.
Along the wall of the outer courtyard on the eastern side of the outer courtyard, in front of the sanctuary's inner courtyard, there were also rooms
11 zilikuwa kama umbo la vyumba kwa upande wa kaskazini. Zilikuwa urefu ule ule na upana na matokeo yale yale na mipangilio na madirisha.
with a walkway in front of them. They were as the appearance of the rooms on the northern side. They had the same length and breadth and the same exits and arrangements and doors.
12 Kwa upande wa kusini kulikuwa na madirisha kwenye vyumba ambavyo vilikuwa kama yale yaliyokuwa upande wa kaskazini. Aya iliyokuwa ndani ilikuwa na mlango kwenye kichwa chake, na njia ilifunguliwa kwenye vyumba tafauti. Upande mashariki kulikuwa na malango wa njia kwenye njia mwishoni.
On the south side were doors into rooms that were just the same as on the north side. A passage on the inside had a door at its head, and the passage opened into the various rooms. On the east side there was a doorway into the passage at one end.
13 Kisha yule mtu akanambia, “Vyumba vya kaskazini na vyumba vya kusini vilivyokuwa mbele ya ua wa nje ni vyumba vitakatifu amabapo makuhani wafanyao kazi karibu sana na Yahwe waweze kula chakula kitakatifu sana. Wataweka vitu vitakatifu sana-sadaka ya chakula, sadaka ya dhambi, na sadaka ya hatia-kwa kuwa hapa ni mahali patakatifu.
Then the man said to me, “The northern rooms and the southern rooms that are in front of the outer courtyard are holy rooms where the priests who work nearest to Yahweh may eat the most holy food. They will put the most holy things there—the food offering, the sin offering, and the guilt offering—for this is a holy place.
14 Wakati makuhani watakapoingia hapo, wasitoke nje ya mahali patakatifu kwa ua wa nje, bila kuweka mavazi karibu mahali wahudumupo, kwa kuwa hapa ni patakatifu. Hivyo watavalia mahali pengine nguo kabla ya kwenda karibu na watu.”
When the priests enter there, they must not go out of the holy place to the outer court, without laying aside the clothes in which they served, since these are holy. So they must dress in other clothes before going near the people.”
15 Yule mtu akamaliza kupima ndani ya nyumba na kisha akanichukua nje ya lango lililokuwa limeelekea magharibi na kuzipima sehemu zote zilizokuwa zimepazunguka hapo.
The man completed measuring the inner house and then took me out to the gate that faced the east and measured all the surrounding area there.
16 Akaupima upande wa mashariki na fimbo ya kupimia-dhiraa mia tano kwa fimbo ya kupimia.
He measured the east side with a measuring stick—five hundred cubits with the measuring stick.
17 akaupima upande wa kaskazini-dhiraa mia tano na fimbo ya kupimia.
He measured the north side—five hundred cubits with the measuring stick.
18 Pia akaupima upande wa kusini dhraa mia tano na fimbo ya kupimia.
He also measured the south side—five hundred cubits with the measuring stick.
19 Pia akageuka na kuupima upande wa magharibi dhiraa mia tano kwa fimbo ya kupimia,
He also turned and measured the west side—five hundred cubits with the measuring stick.
20 Akaipima pande nne. Ilikuwa na ukuta umeizunguka ilikuwa dhiraa mia tano urefu, na dhiraa mia tano upana, kulitenganisha umbo takatifu kutoka ambapo ni pa kawada.
He measured it on four sides. It had a wall around it that was five hundred cubits in length, and five hundred cubits in width, to separate the holy from that which is common.

< Ezekieli 42 >