< Ezekieli 40 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa kuhamishwa kwetu mwanzoni mwa mwaka siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya mji kuchukuliwa-katika siku hiyo hiyo, mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu na alinichukua huko.
La vingt-cinquième année de notre déportation, au commencement de l'année, le dixième jour du mois, quatorze ans après la ruine de la ville, en ce jour-là, la main de l'Éternel se fit sentir à moi, et m'y transporta.
2 Katika maono ya Mungu akanileta hata nchi ya Israeli. Akanileta kupumzika juu ya kila mlima mrefu sana; upande wa kusini kulikuwa na monekano kana kwamba majengo ya mji.
Ce fut en vision divine qu'il me transporta au pays d'Israël, et me plaça sur une montagne très élevée, de laquelle [on voyait] comme une ville construite au midi.
3 Kisha akanileta huko. Tazama, kulikuwa na mtu! Mwonekano wake ulikuwa kama mwonekano wa shaba. Alikuwa na uzi wa kitani na mwanzi wa kupimia mkononi mwake, na alisimama katika lango la mji.
Il m'y transporta, et voici, il s'y trouvait un homme dont l'aspect était comme l'aspect de l'airain, et il avait en sa main un cordeau de lin et une perche à mesurer, et il se tenait à la porte.
4 Huyo mtu akanambia, “Mwanadamu, tazama kwa macho yako na sikiliza kwa masikio yako, na elekeza moyo wako juu ya yote ninayokufunulia, kwa kuwa ulinileta hapa ili niweze kukufunulia haya wewe. Toa taarifa ya kila kitu utakachokiona kwa nyumba ya Israeli.
Et l'homme me dit: Fils de l'homme, considère de tes yeux, et écoute de tes oreilles, et observe attentivement tout ce que je vais te montrer; car c'est pour qu'on te le montre, que tu as été transporté ici. Rapporte tout ce que tu verras à la maison d'Israël.
5 Kulikuwa ukuta uliokuwa umezunguka eneo la hekalu. Urefu wa kipimo cha mwanzi katika mkono wa mtu ulikuwa dhiraa sita urefu, kila urefu wa dhiraa ulikuwa dhiraa moja na kipimo cha kiganja cha mkono urefu. Aliupima ukuta; ulikuwa kipimo cha mwanzi mmoja na ufito mmoja urefu.
Et voici, un mur régnait extérieurement autour de la maison, tout à l'entour. Or l'homme tenait en sa main une perche de six coudées, dont chacune était d'une coudée et une palme. Et il mesura la largeur de cette construction; elle était d'une perche, et la hauteur d'une perche.
6 Kisha akaenda hata kwenye lango la hekalu lililokuwa limeelekea mashariki. Akapanda ngazi na kuipima kizingiti cha lango-mwanzi mmoja upana.
Puis il vint à la porte qui donne à l'orient, et en monta les degrés et mesura le seuil de la porte; il avait une perche en largeur; c'était là l'un des seuils; sa largeur était d'une perche;
7 Vyumba vya ulinzi vilikuwa kila mwanzi mmoja urefu na mwanzi mmoja upana; kulikuwa na dhiraa tano katika kila vyumba viwili, na kizingiti cha lango la hekalu karibu na tawa la hekalu kilikuwa mwanzi mmoja urefu.
et chaque appartement avait une perche en longueur, et une perche en largeur; et entre les appartements il y avait cinq coudées; et le seuil intérieur de la porte à côté du vestibule de la porte avait une perche.
8 Akapima tawa la lango; ulikuwa mwanzi mmoja urefu.
Et il mesura le vestibule de la porte intérieurement; il avait une perche.
9 Akapima tawa la lango. Ilikuwa mwanzi mmoja kwenda chini. Mihimili ilikuwa dhiraa mbili upana. Hili lilikuwa tawa la lango kuelekea hekalu.
Et il mesura le vestibule de la porte; il avait huit coudées, et ses piliers deux coudées; c'était le vestibule de la porte en dedans.
10 Kulikuwa na vyumba vitatu vya ulinzi pande zote za lango la mashariki, na yote yalikuwa na kipimo kile kile, na kuta zilizokuwa zimezigawanya zilikuwa na kipimo kile kile.
Quant aux appartements de la porte qui donnait à l'orient, il y en avait trois d'un côté et trois de l'autre: ils étaient tous trois de la même dimension, et les piliers de l'un et de l'autre côté avaient la même dimension.
11 Kisha yule mtu akapima upana wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi; na akapima urefu wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi na tatu.
Puis il mesura la largeur de l'ouverture de la porte; elle était de dix coudées; la longueur de la voie de la porte était de treize coudées;
12 Akaupima ukuta uliokuwa mpaka mbele ya vyumba-dhiraa moja urefu. Vyumba vilipimwa dhiraa sita kila upande.
et il y avait devant les appartements un bord d'une coudée, et un bord d'une coudée de l'autre côté; et chaque appartement avait six coudées d'un côté et six coudées de l'autre.
13 Kisha akapima lango la njia kutoka kwenye paa ya chumba kimoja kuelekea chumba kingine-dhiraa ishirini na tano, kutoka lango la kuingia chumba cha kwanza kuelekea kile cha pili.
Puis il mesura toute la porte depuis le toit d'un appartement jusqu'au toit de l'autre, c'était une largeur de vingt-cinq coudées entre les deux ouvertures opposées;
14 Kisha akapima ukuta uliokuwa umeenda kati ya vyumba vya ulinzi-dhiraa sitini urefu; alipima kwa mbali na tawa la lango.
et il trouva pour les piliers soixante coudées; et près des piliers il y avait une cour, la porte étant tout autour;
15 Lango la kuingia kutoka lango la mbele kuelekea lango jingine la tawa la mwisho lilikuwa dhiraa hamsini.
et depuis le devant de la porte d'entrée jusqu'au devant du vestibule de la porte intérieure il y avait cinquante coudées.
16 Kulikuwa na madirisha yaliyokuwa yamefungwa kuelekea vyumba na kuelekea nguzo zake kati ya malango kuzunguka kote; na vivyo hivyo kwa mabaraza. Kulikuwa na madirisha pande zote za ndani, na kila mhimili ulikuwa umepambwa kwa mitende.
Et il y avait aux appartements des fenêtres fermées, et à leurs piliers en dedans de la porte tout autour; et de même au vestibule il y avait des fenêtres tout autour intérieurement, et sur les piliers étaient [sculptés] des palmiers.
17 Kisha huyo mtu akanileta hata ua wa nje mwa hekalu. Tazama, kulikuwa na vyumba, na kulikuwa na kibamba katika ua, pamoja na vyumba thelathini baada ya kibamba.
Alors il m'introduisit dans le parvis extérieur; et voici, il y avait des chambres, et un pavé fait dans le parvis tout autour; il y avait trente chambres sur le pavé.
18 Kibamba kilienda juu hata upande wa malango, na upana wake ulikuwa sawsawa na urefu wa malango. Hiki kilikuwa kibamba cha chini.
Or le pavé était à côté des portes, parallèle à la longueur des portes, c'était le pavé inférieur.
19 Kisha huyo mtu akapima umbali kutoka mebele ya lango la chini hata mbele ya lango la ndani; ilikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki, na sawasawa na upande wa kaskazini.
Et il mesura extérieurement la largeur, depuis le devant de la porte inférieure jusqu'au devant du parvis intérieur; c'étaient cent coudées à l'orient et au nord.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango lililokuwa upande wa kaskazini mwa ua wa nje.
Il mesura aussi en longueur et en largeur la porte qui donnait au nord, dans le parvis extérieur,
21 Kulikuwa na vyumba vitatu pande zote za lango, na lango na matawa yake yalipimwa sawa na lango kubwa-dhiraa hamsini upana wote na dhiraa ishirini na tano upana.
et ses appartements dont il y avait trois d'un côté et trois de l'autre. Et ses piliers et ses vestibules avaient la dimension de la première porte; sa longueur cinquante coudées, et sa largeur vingt-cinq coudées:
22 Madirisha yake, tawa, vyumba, na mitende yake vilikabiliana na lango ambalo linaloelekea mashariki. Ngazi saba kuupandia juu hata kwenye tawa lake.
et ses fenêtres, et son vestibule, et ses palmiers avaient les mêmes dimensions qu'à la porte de l'orient; et on y montait par sept degrés, et son vestibule était en dedans.
23 Kulikuwa na lango kwenye ua wa ndani mbele kuelekea mashariki; huyo mtu alipima kutoka lango moja hadi lango jingine-dhiraa mia moja umbali.
Et il y avait une porte au parvis intérieur, vis-à-vis de la porte du nord et de l'orient; et il mesura d'une porte à l'autre porte cent coudées.
24 Kisha huyo mtu akanileta hata kwenye lango la kuingia la kusini, na kuta zake na tawa vilipimwa sawa kama malango mengine ya nje.
Ensuite il me conduisit au midi; et voici, il y avait une porte au midi: et il mesura ses piliers et ses vestibules; c'étaient les mêmes dimensions;
25 Kulikuwa na madirisha yaliyofungwa katika lango la njia na tawa lake kama lile lango. Lango la kusini na tawa lake vilipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
et elle avait, ainsi que son vestibule, des fenêtres de tous côtés, pareilles aux autres fenêtres; la longueur était de cinquante coudées, et la largeur de vingt-cinq coudées;
26 Kulikuwa na ngazi saba hadi kwenye lango na matawa yake, na kulikuwa na mitende iliyochongoka juu ya kuta pande zote.
et sept marches formaient son escalier, et son vestibule était en dedans; il y avait aussi des palmiers, un d'un côté et un de l'autre, à ses piliers.
27 Kulikuwa na lango la ua wa ndani upande wa kusini, na yule mtu akapima kutoka hilo lango hata lango la kuingia upande wa kusini-dhiraa mia moja umbali.
Et le parvis intérieur avait une porte du côté du midi. Et il mesura d'une porte à l'autre porte au côté du midi cent coudées.
28 Kishi huyo mtu akanileta hata ua wa ndani karibu na lango lake la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo vile vile kama malango mengine.
Ensuite il m'introduisit dans le parvis intérieur par la porte du midi; et il trouva à la porte du midi les mêmes dimensions,
29 Vyumba vyake, kuta, na matao vilipimwa sawa kama malango mengine; kulikuwa na madirisha kuzunguka matao yote. Lango la ndani na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
et à ses appartements et à ses piliers et à ses vestibules les mêmes dimensions. Elle avait, ainsi que son vestibule, des fenêtres tout autour; la longueur était de cinquante coudées et la largeur de vingt-cinq coudées.
30 Pia kulikuwa na matao pande zote za kuta za ndani; haya yalikuwa dhiraa ishirini na tano urefu na dhiraa tano upana.
(Et il y avait tout autour un vestibule de vingt-cinq coudées en longueur et de cinq de largeur.)
31 Hili tawa lilielekea ua wa nje pamoja na mitende iliyochongwa juu ya kuta zake na ngazi nane kuupandia.
Or son vestibule était du côté du parvis extérieur, et ses piliers avaient des palmiers, et huit marches formaient son escalier.
32 Kisha yule mtu akanileta hata kwenye ua wa ndani karibu na njia ya kaskazini na kulipima lango, ambalo lilikuwa na vipimo sawa kama malango mengine.
Alors il m'introduisit dans le parvis intérieur du côté de l'orient, et il trouva à cette porte les mêmes dimensions,
33 Vyumba vyake, kuta, na matawa yalikuwa na kipima sawa kama cha malango, na kulikuwa na madirisha pande zote. Laango la ndani na matawa yake yalikuwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
et à ses appartements et à ses piliers et à ses vestibules les mêmes dimensions; et elle avait, ainsi que son vestibule, des fenêtres tout autour; la longueur était de cinquante coudées, et la largeur de vingt-cinq coudées.
34 Matawa yake yalielekea nje ya ua; ilikuwa na mitende pande zote za hiyo na ngazi nane za kuupandia.
Or son vestibule était du côté du parvis extérieur, et il y avait des palmiers sur ses piliers d'un côté et de l'autre, et huit marches formaient son escalier.
35 Kisha huyo mtu akanileta hata lango la kaskazini na kulipima; likapimwa vivyo hivyo kama malango mengine.
Puis il m'introduisit dans la porte du nord, et il trouva les mêmes dimensions,
36 Vyumba vyake, kuta, na ukumbi vilipimwa sawa na malango mengine, na kulikuwa na madirisha pande zote. Njia ya lango na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na upana dhiraa ishirini na tano.
à ses appartements, à ses piliers et à ses vestibules, et elle avait des fenêtres de tous côtés; la longueur était de cinquante coudées, et la largeur de vingt-cinq coudées.
37 Tatawa lake lilielekea ua wa nje; ilikuwa na mitende pande zote za huo na ngazi nane kuupandia.
Or son vestibule était du côté du parvis extérieur, et il y avait des palmiers à ses piliers d'un côté et de l'autre, et huit marches formaient son escalier.
38 Kulikuwa na chumba pamoja na mlango karibu na kila lango la ndani. Hapa ndipo ambako walipooshea sadaka za kutekezwa.
Or il y avait une chambre avec sa porte entre les piliers aux portes; c'est là qu'on devait laver les holocaustes.
39 Kulikuwa na meza mbili kila upande wa kila ukumbi, ambako sadaka ya kuteketezwa ilipochinjiwa, na pia sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
Et dans le vestibule de la porte se trouvaient deux tables d'un côté, et deux tables de l'autre, pour y égorger l'holocauste et les victimes pour le péché et pour le délit.
40 Karibu na ukuta wa ua, kuelekea juu kwenye lango kuelekea kaskazini, kulikuwa na meza mbili. Pia kwa upande mwingine kulikuwa na meza mbili kwenye lango la ukumbi.
De plus, au côté extérieur, près de l'escalier qui montait à l'ouverture de la porte du nord, il y avait deux tables, et à l'autre côté qui appartenait au vestibule de la porte, il y avait deux tables:
41 Kulikuwa na meza nne pande zote karibu na lango; wakachinja wanyama juu ya meza nane.
quatre tables de ci et quatre tables de là, à côté de la porte; en tout huit tables, où l'on devait égorger les victimes.
42 Kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, dhiraa moja na nusu urefu, dhiraa moja na nusu upana, na kimo dhiraa moja. Juu yake waliweka vyombo pamoja ambavyo walivichinjia sadaka za kuteketezwa kwa ajili ya sadaka.
Il y avait aussi quatre tables à l'escalier, de pierre de taille, longues d'une coudée et demie, et larges d'une coudée et demie, et hautes d'une coudée: on y devait déposer les instruments avec lesquels on égorge les holocaustes et les autres victimes;
43 Kulabu mbili ujazo wa kiganja urefu uliokuwa umeunganishwa katika ua pande zote, na nyama ya matoleo ilikuwa imewekwa juu ya meza.
et des crochets larges d'une palme étaient fixés au dedans de la maison de toutes parts; et les tables devaient recevoir la chair des sacrifices.
44 Karibu na lango la ndani, katika ua wa ndani, kulikuwa na vyumba vya waimbaji. Moja ya hivi vyumba kilikuwa upande wa kaskazini, na kingine kusini.
Et en dehors de la porte intérieure il y avait des chambres pour les chantres dans le parvis intérieur, elles étaient à côté de la porte du nord, ayant leur façade au midi, et une autre à côté de la porte de l'orient, ayant sa façade au nord.
45 Kisha yule mtu akanambia, “Hiki chumba kinachoelekea kusini ni kwa ajili ya makuhani walio zamu katika hekalu.
Alors il me dit: « Cette chambre dont la façade est au midi, est pour les prêtres chargés du service de la maison,
46 Chumba kilichoelekea kaskazini kilikuwa kwa ajili ya makuhani waliokuwa zamu kwenye madhabahu. Hawa ni wana wa Sadoki ambaye huja humkaribia Yahwe kumtumikia; ambao ni miongoni mwa wana wa Lawi.”
et la chambre dont la façade est au nord, est pour les prêtres chargés du service de l'autel. Ce sont les enfants de Tsadok qui entre les enfants de Lévi auront accès auprès de l'Éternel pour le servir. »
47 Kisha akaupima ule ua-dhiraa mia moja urefu na dhiraa mia moja upana mraba, pamoja na madhabahu mbele ya nyumba.
– Alors il mesura le parvis qui avait en longueur cent coudées et en largeur cent coudées, en carré. Or l'autel était devant la maison.
48 Kisha yule mtu akanileta hata kwenye varanda ya nyumba na kupima mwimo wa milango yake-ilikuwa dhiraa tano unene upande huu. Njia ya kuingilia yenyewe ilikuwa dhiraa kumi na nne, na kuta pande zote za huo zilikuwa dhraa tatu upana.
Alors il me conduisit au vestibule de la maison, et il mesura les piliers de ce vestibule: il y avait cinq coudées d'un côté et cinq coudées de l'autre. Et la largeur de la porte était de trois coudées d'un côté et trois coudées de l'autre;
49 Urefu wa ukumbi ulikuwa dhiraa ishirini, na upana wake ulikuwa dhiraa kumi na moja. Kulikuwa na ngazi zilizokuwa zimepanda juu na nguzo zilizokuwa zimesimama pande zote za huo.
la longueur du vestibule était de vingt coudées, et la largeur de onze coudées, et on y montait par des degrés; et il y avait des colonnes près des piliers, l'une d'un côté, l'autre de l'autre.

< Ezekieli 40 >