< Ezekieli 39 >

1 “Kisha wewe, mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! ni kinyume nawe, Gogu, mkuu wa Mesheki na Tubali.
And you O son of humankind prophesy on Gog and you will say thus he says [the] Lord Yahweh here I [am] against you O Gog [the] prince of [the] head of Meshech and Tubal.
2 Nitakugeuza na kukuongoza; nitakupandisha juu kutoka mbali kaskazini na kukuleta hata milima ya Israeli.
And I will turn around you and I will lead on you and I will bring up you from [the] remotest parts of [the] north and I will bring you on [the] mountains of Israel.
3 Kisha nitaufunga upinde wako utoke katika mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale kuanguka kutoka kwenye mkono wako wa kuume.
And I will strike bow your from [the] hand of left your and arrows your from [the] hand of right your I will make fall.
4 Utaanguka juu ya milima ya Israeli-wewe na jeshi lako late na maaskari walio pamoja nawe. Nitawapatia ndege mbua na wanyama pori wa mashambani kwa ajili ya chakula.
On [the] mountains of Israel you will fall you and all troops your and peoples which [are] with you to bird[s] of prey of bird[s] every wing and [the] animal[s] of the field I will give you for food.
5 Utaanguka juu ya uso wa shamba, kwa kuwa mimi mwenyewe nimesema hivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
On [the] surface of the field you will fall for I I have spoken [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
6 Kisha nitapeleka moto juu ya Magogu na kwa wale waishio salama juu ya pwani, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.
And I will send fire on Magog and on [the] inhabitants of the islands to security and they will know that I [am] Yahweh.
7 Kwa kuwa nitalifanya jina langu takatifu lijulikane kati ya watu wangu Israeli, na sitaruhusu tena jina langu takatifu litukanwe; mataifa watajua kwamba mimi ni Yahwe, Mtakatifu katika Israeli.
And [the] name of holiness my I will make known in among people my Israel and not I will let be profaned [the] name of holiness my again and they will know the nations that I Yahweh [am] holy in Israel.
8 Tazama! Siku inakuja, na itachukua nafasi-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
There! [it is] coming and it will occur [the] utterance of [the] Lord Yahweh it [is] the day which I have spoken.
9 Hao wakaao katika miji ya Israeli watatoka nje na watatumia silaha kuwasha moto na kutengeneza moto na kuwachoma-ngao ndogo, ngao kubwa, pinde, mishale, rungu, na mikuki; watatengeneza mioto pamoja nao kwa muda wa siku saba.
And they will go out [the] inhabitants of - [the] cities of Israel and they will kindle and they will kindle a fire with weapon and shield and body shield with bow and with arrows and with staff of hand and with spear and they will kindle with them fire seven years.
10 Hawatakusanya kuni kutoka mashambani wala kukata miti kutoka kwenye misitu, kwa kuwa watazichoma hizo silaha; watawateka nyara wale watakaotaka kuwateka nyara-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
And not they will carry wood from the field and not they will cut [it] from the forests for with the weapon they will kindle fire and they will plunder [those who] plundered them and they will take as spoil [those who] took as spoil them [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
11 Kisha itakuwa katika hiyo siku ambayo nitaifanya sehemu huko kwa ajili ya Gogu-kaburi la Israeli, bonde kwa ajili ya wale wanaosafiri hata mashariki ya bahari. Litawazuia wale wanaotegemea kupita. Huko watamzika Gogu pamoja na kundi lake lote. Watapaita bonde la Hamon-Gogu.
And it will be on the day that I will give to Gog - a place there a burial site in Israel [the] valley of those [who] pass through [the] east of the sea and [will] block [the] way of it those [who] pass through and people will bury there Gog and all (multitude his *Qk) and they will call [it] [the] valley of Hamon-Gog.
12 Kwa muda wa siku saba nyumba ya Israeli itawazika ili kuitakasa nchi.
And they will bury them [the] house of Israel so as to cleanse the land seven months.
13 Kwa kuwa watu wa nchi watawazika; itakuwa siku ya kukumbukwa kwao wakati nitakapotukuzwa-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
And they will bury [them] all [the] people of the land and it will become for them a name [the] day of my glorifying myself [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
14 Kisha watawateua watu kuendelea kwenda kwenye nchi, kuwatafuta wale waliokuwa wakisafiri, lakini waliokufa na miili yao kubaki juu ya uso wa nchi, ili kwamba waweze kuwazika, kwa ajili ya kusafisha nchi. Katika siku ya mwisho ya mwezi wa saba wataanza kutafuta.
And people of continuity they will set apart [who] pass in the land [who] bury those [who] pass through those [who] remain on [the] surface of the land to cleanse it from [the] end of seven months they will make a search.
15 Kama hawa watu wapitao kwenye nchi, watakapoona mfupa wowote wa binadamu, wataweka alama kwa huo, hadi wachimba kaburi watakapokuja na kuizika katika bonde la Hamoni Gogu.
And they will pass those [who] pass in the land and they will see a bone of a human and he will build beside it a marker until they have buried it those [who] bury to [the] valley of Hamon-Gog.
16 Kutakuwa na mji huko unaitwa Hamona. Wataitakasa nchi kwa njia hii.
And also [the] name of a city [is] Hamonah and they will cleanse the land.
17 Kwako wewe, mwanadamu, Bwana Yahwe asema hivi: Waambie ndege wote wenye mabawa na wanyama wote wa porini katika mashamba, 'Kusanyikeni pamoja na mje. Kusanyikeni kutoka pande zote kwenda kwenye dhabihu yote ambayo mimi mwenyewe ninayoifanya kwa ajili yako, dhabihu kubwa juu ya milima ya Israeli, ili kwamba mle nyama na kunywa damu.
And you O son of humankind thus he says - [the] Lord Yahweh say to bird[s] of every wing and to every - animal of the field assemble and come gather yourselves from round about to sacrifice my which I [am] sacrificing for you a sacrifice great on [the] mountains of Israel and you will eat flesh and you will drink blood.
18 Mtakula nyama ya walio hodari na kunywa damu ya wakuu wa dunia; watakuwa kondoo waume, wana kondoo, mbuzi, na ng'ombe, wote walikuwa wanene katika Basheni.
[the] flesh of Warriors you will eat and [the] blood of [the] princes of the land you will drink rams lambs and goats bulls fatlings of Bashan all of them.
19 Kisha mtakula mafuta hata kuridhika kwenu; mtakunywa damu hadi kulewa; hii itakuwa dhabihu nitakayoichinja kwa ajili yenu.
And you will eat fat to satiety and you will drink blood to drunkenness from sacrifice my which I have sacrificed for you.
20 Mtatosheka kwenye meza yangu pamoja na farasi, magari ya farasi, shujaa, na kila mtu wa vita-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
And you will be satisfied at table my horse and charioteer warrior and every man of war [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
21 Nitauweka utukufu wangu kati ya mataifa, na mataifa yote yataona hukumu yangu ninayoionyesha na mkono wangu nimeuweka juu yao.
And I will set glory my among the nations and they will see all the nations judgment my which I have done and hand my which I have put on them.
22 Nyumba ya Israeli itajua yakwamba mimi ni Yahwe Mungu wao kutoka hiyo siku na kuendelea.
And they will know [the] house of Israel that I [am] Yahweh God their from the day that and onwards.
23 Mataifa yatajua kwamba nyumba ya Israeli wameenda uhamishoni kwa sababu ya udhalimu wao kwa kunisaliti, hivyo naficha uso wangu kwao na kuwaweka kwenye mkono wa maadui zao ili kwamba wote waanguke kwa upanga.
And they will know the nations that for iniquity their they went into exile [the] house of Israel on that they had acted unfaithfully against me and I hid face my from them and I gave them in [the] hand of opponents their and they fell by the sword all of them.
24 Nimewafanyia kutokana na uchafu wao na dhambi zao, nitakapokuwa nimeuficha uso wangu kwao.
According to uncleanness their and according to transgressions their I have dealt them and I hid face my from them.
25 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Sasa nitawarudisha watu wa Yakobo, na kuwa na huruma juu ya nyumba yote ya Israeli, wakati nitakapoona wivu kwa ajili ya jina langu.
Therefore thus he says [the] Lord Yahweh now I will turn back ([the] captivity of *Qk) Jacob and I will have compassion on all [the] house of Israel and I will be zealous for [the] name of holiness my.
26 Kisha watabeba aibu yao na uhaini mkubwa walio nihaini. Watayasahau haya yote watakapopumzika katika nchi yao katika usalama, wala hakuna mtu atakaye waogofya.
And they will bear disgrace their and all unfaithfulness their which they acted unfaithfully against me when dwell they on own land their to security and there not [will be one who] disturbs [them].
27 Wakati nitakapokuwa nimewarudisha kutoka kwa watu na kuwakusanya kutoka kwenye nchi za maadui zao, nitajionyesha mimi mwenyewe kuwa mtakatifu kwenye uso wa mataifa mengi.
When bring back I them from the peoples and I will gather them from [the] lands of enemies their and I will show myself holy by them to [the] eyes of the nations many.
28 Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe Mungu wao, kwa kuwa nimewapeleka utumwani kati ya mataifa, lakini kisha nitawakusanya kuwarudisha hata nchi yao. Sitamuacha hata mmoja wao kati ya mataifa.
And they will know that I [am] Yahweh God their because sent into exile I them to the nations and I will gather them to own land their and not I will leave behind again any of them there.
29 Sitawaficha uso wangu kwao wakati nitakapomwaga Roho wangu katika nyumba ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
And not I will hide again face my from them [I] who I have poured out spirit my on [the] house of Israel [the] utterance of [the] Lord Yahweh.

< Ezekieli 39 >