< Ezekieli 33 >

1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
And the word of the LORD came unto me, saying:
2 “Mwanadamu, sema hivi kwa watu wako; waambie, 'Nitakapoleta upanga juu ya nchi, kisha watu wa hiyo nchi wakamchukua mtu mmoja kutoka mingoni mwao na kumfanya awe mlinzi wao.
'Son of man, speak to the children of thy people, and say unto them: When I bring the sword upon a land, if the people of the land take a man from among them, and set him for their watchman;
3 Atazamapo kwa upanga kama unakuja juu ya nchi, na apige tarumbeta kuwaonya watu!
if, when he seeth the sword come upon the land, he blow the horn, and warn the people;
4 Kama watu wakisikia sauti ya tarumbeta lakini bila kusikia, na kama upanga ukija na kuwaua, kisha damu ya kila mmoja iko juu ya kichwa chake mwenyewe.
then whosoever heareth the sound of the horn, and taketh not warning, if the sword come, and take him away, his blood shall be upon his own head;
5 Kama mtu akisikia sauti ya tarumbeta na hakusikiliza, damu yake iko juu yake; lakini kama akisikia, ataokoa maisha yake mwenyewe.
he heard the sound of the horn, and took not warning, his blood shall be upon him; whereas if he had taken warning, he would have delivered his soul.
6 Bali, kama mlinzi akiona upanga unakuja, lakini kama asipopiga tarumbeta, pamoja na matokeo kwamba watu hawajaonywa, na kama upanga ukija na kuchukua uhai wa mtu yeyote, kisha yule mtu akafa kwenye dhambi yake mwenyewe, lakini nitaitaka damu yake kutoka mlinzi.'
But if the watchman see the sword come, and blow not the horn, and the people be not warned, and the sword do come, and take any person from among them, he is taken away in his iniquity, but his blood will I require at the watchman's hand.
7 Sasa wewe mwenyewe, mwanadamu! Nimekufanya kuwa mlinzi kwa ajili ya nyumba ya Israeli; utasikia maneno kutoka kinywani mwangu na uwaonye badala yangu.
So thou, son of man, I have set thee a watchman unto the house of Israel; therefore, when thou shalt hear the word at My mouth, warn them from Me.
8 Kama nikimwambia mtu mwovu, 'Mwovu, hakika utakufa!' lakini kama hutangazi hivi ili kwa ajili ya kumuonya mtu mwovu kuhusu hii njia, kisha huyo mtu mwovu atakufa katika dhambi yake, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako!
When I say unto the wicked: O wicked man, thou shalt surely die, and thou dost not speak to warn the wicked from his way; that wicked man shall die in his iniquity, but his blood will I require at thy hand.
9 Lakini wewe, kama ukimwonya mwovu kuhusu hii njia, hivyo basi anaweza kurudi kutoka hiyo, na kama kama asipogeuka kutoka njia yake, kisha atakufa katika dhambi yake, lakini wewe mwenyewe utakuwa umeokoa maisha yako.
Nevertheless, if thou warn the wicked of his way to turn from it, and he turn not from his way; he shall die in his iniquity, but thou hast delivered thy soul.
10 Basi wewe, mwanadamu, sema kwa nyumba ya Israeli, 'Mnasema hivi, Makosa yetu na dhambi zetu zi juu yetu, na tunadhoofika kwa ajili yao! Je! tutaishije?”'
Therefore, O thou son of man, say unto the house of Israel: Thus ye speak, saying: Our transgressions and our sins are upon us, and we pine away in them; how then can we live?
11 Waambie, 'Kama niishivyo-asema Bwana Yahwe-sifurahii kifo cha mwovu, kwa kuwa kama mwovu akitubu kutoka njia yake, kisha ataishi! Tubu! Tubu kutoka njia zako mbaya! Kwa nini mnataka kufa, nyumba ya Israeli?'
Say unto them: As I live, saith the Lord GOD, I have no pleasure in the death of the wicked, but that the wicked turn from his way and live; turn ye, turn ye from your evil ways; for why will ye die, O house of Israel?
12 Hivyo basi wewe, mwanadamu, waambe watu wako, 'Haki ya mwenye haki haitamwokoa kama akikosa! Uovu wa mtu mwovu hautamfanya kuangamia kama akitubu dhambi zake! Kwa kuwa mtu mwenye haki hataweza kuishi kwa sababu ya haki yake kama akikosa.
And thou, son of man, say unto the children of thy people: The righteousness of the righteous shall not deliver him in the day of his transgression; and as for the wickedness of the wicked, he shall not stumble thereby in the day that he turneth from his wickedness; neither shall he that is righteous be able to live thereby in the day that he sinneth.
13 Kama nikisema kwa mwenye haki, “Hakika ataisha!” na kama akiamini katika haki yake na kisha akafanya udhalimu, sitokumbuka haki yake yoyote. Atakufa kwa ajili ya uovu alioufanya.
When I say to the righteous, that he shall surely live; if he trust to his righteousness, and commit iniquity, none of his righteous deeds shall be remembered; but for his iniquity that he hath committed, for it shall he die.
14 Hivyo kama nikisema kwa mwovu, “Utakufa hakika,” lakini kama akitubu kutoka kwenye dhambi zake na kufanya yaliyo halali na haki-
Again, when I say unto the wicked: Thou shalt surely die; if he turn from his sin, and do that which is lawful and right;
15 kama akirudisha dhamana ambayo aliyomnyang'anya, au kama akirudisha alichokipoteza, na kama akitembea katika amri zitoazo uhai na bila kufanya dhambi-kisha ataishi hakika. Hatakufa.
if the wicked restore the pledge, give back that which he had taken by robbery, walk in the statutes of life, committing no iniquity; he shall surely live, he shall not die.
16 Dhambi alizozifanya hazitakumbukwa kwa ajili yake. Ametenda halali na haki, na hivyo, ataishi hakika!
None of his sins that he hath committed shall be remembered against him; he hath done that which is lawful and right; he shall surely live.
17 Lakini watu wako husema, “Njia ya Bwana haiko sawa!” lakini ni njia zako ndizo haziko sawa!
Yet the children of thy people say: The way of the Lord is not equal; but as for them, their way is not equal.
18 Wakati mtu mwenye haki ageukapo kutoka kwenye haki na kufanya dhambi, kisha atakufa katika hiyo!
When the righteous turneth from his righteousness, and committeth iniquity, he shall even die thereby.
19 Wakati mtu mbaya ageukapo kutoka kwenye ubaya wake na kufanya iliyo halali na haki, ataishi kwa sababu ya hayo mambo!
And when the wicked turneth from his wickedness, and doeth that which is lawful and right, he shall live thereby.
20 Lakini ninyi watu husema, “Njia ya Bwana haiko sawa!” Nitawahukumu kila mmoja wenu kulingana na njia yake, nyumba ya Israeli!”'
Yet ye say: The way of the Lord is not equal. O house of Israel, I will judge you every one after his ways.'
21 Ikawa katika mwaka wa kumi na mbili, siku ya tano ya mwezi wa kumi ya uhamisho wetu, mtu mmoja akatoroka kutoka Yerusalemuna kusema, “Mji umetekwa!”
And it came to pass in the twelfth year of our captivity, in the tenth month, in the fifth day of the month, that one that had escaped out of Jerusalem came unto me, saying: 'The city is smitten.'
22 Mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu jioni kabla yule mtoro hajaja, na mdomo wangu ulikuwa wazi mda huo alikuja kwangu wakati wa mapambazuko. Hivyo mdomo wangu ulikuwa wazi; sikuwa bubu tena!
Now the hand of the LORD had been upon me in the evening, before he that was escaped came; and He had opened my mouth against his coming to me in the morning; and my mouth was opened, and I was no more dumb.
23 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
Then the word of the LORD came unto me, saying:
24 “Mwanadamu, wale waishio mahali palipoharibika katika nchi ya Israeli huongea na kusema, 'Ibrahimu alikuwa mtu pekee, na alirithi nchi, lakini sisi tukowengi! Tumepewa nchi kama wamiliki.”
'Son of man, they that inhabit those waste places in the land of Israel speak, saying: Abraham was one, and he inherited the land; but we are many; the land is given us for inheritance.
25 Kwa hiyo waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Mnakula damu, na mmeziinulia macho yenu sanamu, kisha mnazimwagia damu za watu. Je! mna uhakika wa kuimiliki hii nchi?
Wherefore say unto them: Thus saith the Lord GOD. Ye eat with the blood, and lift up your eyes unto your idols, and shed blood; and shall ye possess the land?
26 Mnategemea upanga wenu na mmetenda mambo maovu; kila mtu amemnajisi mke wa jirani yake. Je! kweli mtaimiliki nchi?'
Ye stand upon your sword, ye work abomination, and ye defile every one his neighbour's wife; and shall ye possess the land?
27 Utawaambia hivi, 'Bwana Yahwe asema hivi: Kama niishivyo, hakika wale walio katika uharibifu wataanguka kwa upanga, na nitawapatia wale walio katika mashamba viumbe hai kama chakula, na wale walio katika ngome na mapango watakufa kwa tauni.
Thus shalt thou say unto them: Thus saith the Lord GOD: As I live, surely they that are in the waste places shall fall by the sword, and him that is in the open field will I give to the beasts to be devoured, and they that are in the strongholds and in the caves shall die of the pestilence.
28 Kisha nitairudisha nchi kwenye ukiwa na tishio, na kiburi cha uwezo wake kitakoma, kwa kuwa milima ya Israeli itakuwa jangwa, na hakutakuwa na mtu yeyote atakayewapitia.'
And I will make the land most desolate, and the pride of her power shall cease; and the mountains of Israel shall be desolate, so that none shall pass through.
29 Hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapoifanya nchi ukiwa na tishio kwa sababu ya machukizo yote waliyoyafanya.
Then shall they know that I am the LORD, when I have made the land most desolate, because of all their abominations which they have committed.
30 Hivyo basi wewe, mwanadamu-watu wako wanasema mambo yako karibu na kuta na malango ya nyumba, na kila mmoja anaambizana na mwenzake-kila mtu na ndugu yake, 'Twende na tukasikilize neno la nabii lililotoka kwa Yahwe!
And as for thee, son of man, the children of thy people that talk of thee by the walls and in the doors of the houses, and speak one to another, every one to his brother, saying: Come, I pray you, and hear what is the word that cometh forth from the LORD;
31 Hivyo watu wangu watakuja kwako, kama wafanyavyo mara nyingi, na nitaketi mbele yako na kusikiliza maneno yako, lakini mioyo yao inafuata udhalimu kwa faida yao.
and come unto thee as the people cometh, and sit before thee as My people, and hear thy words, but do them not — for with their mouth they show much love, but their heart goeth after their covetousness;
32 Kwa kuwa umekuwa kama wimbo mzuri kwao, sauti nzuri awezaye kucheza kinanda vizuri, hivyo watasikia maneno yako, lakini hakuna atakaye yatii.
and, lo, thou art unto them as a love song of one that hath a pleasant voice, and can play well on an instrument; so they hear thy words, but they do them not —
33 Hivyo wakati haya yote yatakapotokea-tazama! itatokea! -watajua yakwamba nabii alikuwa miongoni mwao.”
when this cometh to pass — behold, it cometh — then shall they know that a prophet hath been among them.'

< Ezekieli 33 >