< Ezekieli 32 >

1 Kisha ikawa katika mwezi wa kumi na mbili wa mwaka wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
Un divpadsmitā gadā, divpadsmitā mēnesī pirmā mēneša dienā Tā Kunga vārds uz mani notika sacīdams:
2 “Mwanadamu, inua maombolezo kuhusu Farao mfalme wa Misri; mwambie, 'Wewe ni kama simba mdogo juu ya mataifa, lakini kama jitu la kutisha, unatoka kwenye maji, unayachafua maji kwa miguu yako na kuyachafua maji yao.
Cilvēka bērns, sāc raudu dziesmu par Faraonu, Ēģiptes ķēniņu, un saki uz viņu: ak tautu lauva, tu esi pagalam! Un tu biji kā jūras zvērs jūrā un izlēci savās upēs un sajauci ūdeņus ar savām kājām un samini upes.
3 Bwana Yahwe asema hivi: Basi nitautandaza wavu wangu juu yako katika kusanyiko la watu wengi, na watawainua juu katika wavu wangu.
Tā saka Tas Kungs Dievs: Es tādēļ Savu tīklu izplētīšu pār tevi daudz tautu sapulcē, kas tevi izvilks Manā tīklā.
4 Nitakuacha katika nchi. Nitakutupa kwenye shamba na kufanya ndege wote wa angani watue juu yako; njaa ya wanyama wote waishio juu ya nchi watashibishwa na wewe.
Tad Es tevi metīšu uz zemi, Es tevi nosviedīšu uz lauku un visiem putniem apakš debess Es likšu mist uz tevis un visiem zvēriem virs zemes no tevis pieēsties,
5 Kwa kuwa nitaiweka nyama yako juu ya milima, na nitayajaza mabonde kwa funza wako waliokufa.
Un metīšu tavu maitu uz kalniem un pildīšu tās ielejas ar tavām miesām.
6 Kisha nitamwaga damu yako juu ya milima, na vitanda vya kijito vitajazwa kwa damu yako.
Un Es dzirdināšu zemi ar tām asinīm, kas no tevis izplūst līdz kalniem, un upes no tevis taps pildītas.
7 Kisha wakati nitakapokuzimisha, nitazifunika mbingu na kuzitia giza nyota zake; nitalifunika jua kwa mawingu, na mwezi hautatoa nuru yake usiku.
Un kad Es tevi izdzēsīšu, tad Es apsegšu debesi un aptumšošu viņas zvaigznes, sauli Es apklāšu ar mākoņiem, un mēneša gaišums vairs nespīdēs.
8 Mianga ya mbinguni nitaiweka giza juu yako, na nitaweka giza juu ya nchi-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
Visus spožos debess spīdekļus Es tevis dēļ aptumšošu un vedīšu tumsību pār tavu zemi, saka Tas Kungs Dievs.
9 Hivyo nitaitisha mioyo ya watu wengi katika nchi ambao huwajui, wakati nitakapoleta kuhusu uvunjifu miongoni mwa mataifa, miongoni mwa nchi ambazo hukuzijua.
Es arī darīšu skumīgas daudz tautu sirdis, kad Es tavu mocību iznesīšu starp tautām, tanīs valstīs, ko tu nepazīsti.
10 Nitawashangaza watu wengi kuhusiana na wewe; wafalme wao watatetemeka kwa hofu kuhusiana na wewe nitakapoutikisa upanga wangu mbele yao. Kila wakati kila mmoja atatetemeka kwa sababu yako, katika siku ya kuanguka kwako.
Un Es darīšu, ka daudz tautas par tevi iztrūcinājās, un viņu ķēniņiem mati celsies stāvu par tevi, kad Es cilāšu Savu zobenu viņu priekšā, un tie drebēs ik acumirkli ikviens par savu dvēseli tai dienā, kad tu kritīsi.
11 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja juu yako.
Jo tā saka Tas Kungs Dievs: Bābeles ķēniņa zobens nāks pār tevi.
12 Nitawafanya watu wako kuanguka kwa panga za mashujaa-kila shujaa ni tishio la mataifa. Hawa mashujaa watateketeza kiburi cha Misri na kuangamiza watu wake wote.
Un Es tavu pulku nogāzīšu caur vareno zobeniem, tie visi ir tie visbriesmīgākie starp tautām, tie izpostīs Ēģiptes lepnību, un viss viņas pulks taps izdeldēts.
13 Kwa kuwa nitaiharibu mifugo yote kutoka karibu na maji mengi; na mguu wa mtu hautayatibua tena, wala kwato za wanyama hazitayatibua.
Un visus viņas lopus Es izdeldēšu pie tā lielā ūdens, ka cilvēka kāja to vairs nesajauks, ir lopu nags to nesajauks.
14 Kisha nitayafanya maji yao kuwa matulivu na kufanya mito yao kukimbia kama mafuta-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
Tad Es viņu ūdeņus darīšu skaidrus un viņu upēm likšu tecēt kā eļļai, saka Tas Kungs Dievs,
15 Wakati nitakapoifanya nchi ya Misri sehemu iliyojitenga, wakati nchi iliyopungukiwa na vitu viijazavyo, wakati nitakapo washambulia wakaao ndani yake, watajua yakwamba mimi ni Yahwe.
Kad Es Ēģipti būšu darījis par posta vietu, un zeme no savas pilnības būs palikusi tukša, kad Es visus viņas iedzīvotājus būšu kāvis, - tad samanīs, ka Es esmu Tas Kungs.
16 Kutakuwa na maombolezo; binti za mataifa wataomboleza juu yake; wataomboleza juu ya Misri, juu ya watu wake wote wataomboleza-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
Šī ir tā raudu dziesma, un tā jādzied; tautu meitas šo raudu dziesmu dziedās; par Ēģipti un par visu viņas ļaužu pulku tās dziedās šo raudu dziesmu, saka Tas Kungs Dievs. -
17 Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na mbili, siku ya kumi na tano ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
Un divpadsmitā gadā, piecpadsmitā mēneša dienā Tā Kunga vārds uz mani notika sacīdams:
18 “Mwanadamu, omboleza kwa ajili watu wa misri na walete chini-yeye na binti za mataifa mashuhuri-hata chini ya dunia pamoja na wale walioshuka chini kwenye shimo.
Cilvēka bērns, žēlojies par Ēģiptes ļaužu pulku un nogremdē to līdz ar tām lepno tautu meitām zemes apakšā pie tiem, kas grimuši dziļumā.
19 'Je! wewe ni mzuri zaidi kuliko mtu mwingine yeyote? Nenda chini na lala chini pamoja na wasiotahiriwa.'
Par ko tu nu esi skaistāka? Kāp zemē un apgūlies pie neapgraizītiem.
20 Wataanguka miongoni mwao waliokuwa wameuawa kwa upanga. Upanga ulikuwa umewekwa! Alikuwa amepatiwa upanga; watamkamata na watu wake.
Tie kritīs starp zobena nokautiem. Viņa ir nodota zobenam; aizraujiet viņu ar visu viņas ļaužu pulku.
21 Hodari wa wapiganaji katika Sheoli atasema kuhusu Misri na rafiki zake, 'Wameshuka chini hapa! Watalala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale waliokuwa wameuawa kwa upanga.' (Sheol h7585)
Tie varoņu varenie un viņas palīgi ar viņu runās elles vidū: tie ir nogrimuši, tie guļ starp neapgraizītiem un zobena nokautiem. (Sheol h7585)
22 Ashuru yupo huko pamoja na kusanyiko lake. Makaburi yake yamemzunguka; wote waliuawa kwa upanga.
Tur ir Asurs ar visu savu ļaužu pulku, viņu kapi ir visapkārt ap viņu; tie visi nokauti, caur zobenu krituši.
23 Wale ambao makaburi yao yamewekwa katika maficho ya mashimo yaliyo huko, pamoja na kusanyiko lake. Makaburi yake yakiwazunguka wote waliokuwa wameuawa, walioanguka kwa upanga, wale walioleta hofu juu ya nchi ya walio hai.
Viņa kaps ir tai visdziļākā bedrē, un viņa ļaužu pulks ir visapkārt ap viņa kapu; visi nokauti, caur zobenu krituši, kas briesmas bija cēluši dzīvo zemē.
24 Elamu yupo huko pamoja na watu wake wote. Makaburi yake yamemzunguka; wote walikuwa wameuawa. Wale walioawa kwa upanga, walioshuka chini wasiotahiriwa hata sehemu ya chini kabisa ya dunia, waliowatia hofu juu ya nchi ya walio hai na wale waliobeba aibu yao wenyewe, pamoja na wale washukao chini kwenye shimo.
Tur ir Elams ar visu savu ļaužu pulku visapkārt ap viņa kapu; tie visi nokauti, caur zobenu krituši; tie grimuši neapgraizīti zemes apakšā, kas briesmas bija cēluši dzīvo zemē, tie nes savu kaunu pie tiem, kas grimuši dziļumā.
25 Wamemuwekea kitanda kwa ajili ya Elamu na watu wake wote kati ya wachinjaji; kaburi lake limemzunguka. Wote hawajatahiriwa, kukatwa vipande kwa upanga, kwa sababu waliwaleta mashujaa wao juu ya nchi ya walio hai. Hivyo wamechukua aibu yao wenyewe, pamoja na wale washukao kwenye shimo miongoni mwa wote waliouawa, wale washukao kwenda shimoni. Elamu yu miongoni mwa wale waliokuwa wameuawa.
Pie nokautiem cisas sataisītas viņam un visam viņa ļaužu pulkam, viņu kapi ir visapkārt ap viņu; tie visi, neapgraizīti, caur zobenu ir nokauti; tāpēc ka tie briesmas cēluši dzīvo zemē, tie nes savu kaunu pie tiem, kas grimuši dziļumā, - viņš guldināts nokauto vidū.
26 Mesheki, Tubali, na watu wake wote wako huko! Makaburi yao yamewazunguka. Wote hawajatahiriwa, wameuawa kwa upanga, kwa sababu walileta utiisho wao juu ya nchi ya walio hai.
Tur ir Mešehs un Tūbals ar visu savu ļaužu pulku, visapkārt ap viņu ir viņu kapi, tie visi, neapgraizīti, ir nokauti ar zobenu, tāpēc ka bija briesmas cēluši dzīvo zemē.
27 Wasilale pamoja mashujaa walioanguka wa wasiotahiriwa walioshuka chini kwa Sheoli pamoja na silaha zao zote za vita, na pamoja na panga zao zote walizoziweka chini ya vichwa vyao na maovu yao juu ya mifupa yao. Kwa kuwa walikuwa tishio kwa mashujaa katika nchi ya walio hai. (Sheol h7585)
Tie neguļ pie tiem kritušiem neapgraizīto varoņiem, kas ellē nogrimuši ar savām bruņām, kam zobeni likti apakš galvām; viņu noziegumi nākuši pār viņu kauliem, tāpēc ka bija varoņi par briesmām dzīvo zemē. (Sheol h7585)
28 Basi wewe, Misri, utavunjika kati yao wasiotahiriwa! Utalala karibu nao waliokuwa wamekatwa vipande vipande kwa upanga.
Arī tu tapsi satriekts neapgraizītu vidū un gulēsi pie zobena nokautiem.
29 Edomu yuko huko na wafalme na viongozi wake wote. Walikuwa wamehifadhiwa katika uwezo wao pamoja na wale walioawa kwa upanga. Pamoja na wasiotahiriwa wamelala, pamoja na wale walioshuka kwenye shimo.
Tur ir Edoms, viņa ķēniņi un visi viņa lielkungi, kas ar savu varoņu godu ir likti pie zobena nokautiem; tie guļ pie neapgraizītiem un pie tiem, kas grimuši dziļumā.
30 Wakuu wa kaskazini wako huko-wote na Wasidoni wote walioshuka chini pamoja na hao waliokuwa wamekatwa vipande vipande. Walikuwa na nguvu na kuwafanya wengine kuogopa, lakini sasa wako huko kwa aibu, wasiotahiriwa pamoja na wale waliokatwa vipande vipande kwa upanga. Wamebeba aibu yao wenyewe, pamoja nao waendao kwenye shimo.
Tur ir visi ziemeļa valdnieki un visi Sidonieši, kas nogrimuši pie nokautiem un kaunā likti, lai gan ar savu varu bijuši par iztrūcināšanu, un tie guļ neapgraizīti pie tiem, kas zobena nokauti, un nes savu kaunu pie tiem, kas nogrimuši dziļumā. -
31 Farao ataona na kupata faraja kuhusu kundi lake waliokatwa vipande vipande kwa upanga -Farao na jeshi lake lote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Faraons tos redzēs un iepriecināsies ar visu savu ļaužu pulku; ar zobenu ir nokauti, Faraons un viss viņa karaspēks, saka Tas Kungs Dievs.
32 Natamuweka kama utiisho wangu katika nchi ya walio hai, lakini atakuwa amelazwa chini katikati yao wasiotahiriwa, miongoni mwa wale walio katwa vipande kwa upanga, Farao na makundi yake yote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Jo Es viņam esmu licis briesmas celt dzīvo zemē, un viņš ir nolikts neapgraizīto vidū pie tiem, kas zobena nokauti, Faraons ar visu savu ļaužu pulku, saka Tas Kungs Dievs.

< Ezekieli 32 >