< Ezekieli 3 >

1 Akanambia, “Mwanadamu, kile ulichokikuta, kula. Kula hili gombo, kisha nenda kaongee na nyumba ya Israeli.”
And he said to me, Son of Man, eat this volume, and go and speak to the children of Israel.
2 Basi nikafungua kinywa changu, na akanilisha hilo gombo.
So he opened my mouth, and caused me to eat the volume. And he said to me, Son of man,
3 Akanambia, “Mwana wa adamu, lisha tumbo lako na jaza tumbo lako kwa hili gombo ambalo nimekupa!” Basi nikalila, na lilikuwa tamu kama asali kwenye mdomo wangu.
your mouth shall eat, and your belly shall be filled with this volume that is given to you. So I ate it; and it was in my mouth as sweet as honey.
4 Kisha akanambia, “Mwana wa adamu, nenda kwenye nyumba ya Israeli na ongea maneno yangu kwao.
And he said to me, Son of man, go your way, and go in to the house of Israel, and speak my words to them.
5 Kwa kuwa hujatumwa kwa watu wenye maneno ya kushangaza au lugha ngumu, lakini kwa nyumba ya Israeli-
For you are not sent to a people of hard speech, [but] to the house of Israel;
6 sio kwa taifa lenye nguvu ya maneno ya ajabu au lugha ngumu ambao maneno yao hutaweza kuyaelewa! Kama nikikutuma kwao, watakusikiliza.
neither to many nations of other speech and other tongues, nor of harsh language, whose words you would not understand: although if I [had] sent you to such, they would have listened to you.
7 Lakini nyumba ya Israeli haitakuwa tayari kukusikiliza, kwa kuwa hawako tayari kunisikiliza mimi. Hivyo nyumba yote ya Israeli ni paji gumu na moyo mgumu.
But the house of Israel will not be willing to listen to you; for they will not listen to me: for all the house of Israel are stubborn and hard-hearted.
8 Kumbe nimeufanya uso wako kama kaidi kama nyuso zao na paji lako kuwa gumu kama mapaji yao.
And, behold, I have made your face strong against their faces, and I will strengthen your power against their power.
9 Nimekufanya paji lako kama almasi, gumu kuliko jiwe la kiberiti! Usiwaogope wala kufadhaika kwa nyuso zao, kwa kuwa ni nyumba ya uasi.”
And it shall be continually stronger than a rock: be not afraid of them, neither be dismayed at their faces, because it is a provoking house.
10 Kisha akanambia, “Mwana wa adamu, maneno yote niliyokutangazia-yachukue kwenye moyo wako na wasikize kwa sikio lako!
And he said to me, Son of man, receive into your heart all the words that I have spoken to you, and hear [them] with your ears.
11 Kisha nenda kwa watumwa, kwa watu wako, na uzungumze nao. Waambie, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo; iwapo watasikia au hapana.”
And go your way, go in to the captivity, to the children of your people, and you shall speak to them, and say to them, Thus says the Lord; whether they will hear, [or] whether they will forbear.
12 Kisha Roho akaniinua juu, na nikasikia nyuma yangu sauti yenye tetemeko la aridhi: “Ubarikiwe utukufu wa Yahwe kutoka mahali pake!”
Then the Spirit took me up, and I heard behind me the voice [as] of a great earthquake, [saying], Blessed [be] the glory of the Lord from his place.
13 Ilikuwa sauti ya mabawa ya viumbe hai vilipokuwa vikigusana kila kimoja, na sauti ya magurudumu ambayo yalikuwa pamoja na hivyo viumbe, na sauti ya tetemeko kubwa arithi.
And I perceived the sound of the wings of the living creatures clapping one to the other, and the sound of the wheels was near them, and the sound of the earthquake.
14 Roho akaniinua juu na kunichukua, Nikaenda kwa uchungu katika hasira kali rohoni mwangu, kwa kuwa mkono wa Yahwe ulikuwa na nguvu ukigandamiza juu yangu!
And the Spirit lifted me, and took me up, and I went in the impulse of my spirit; and the hand of the Lord was mighty upon me.
15 Hivyo nikaenda kwa watumwa huko Tel Abibu waliokuwa wakiishi karibu na Kebari Kanali, na niliishi miongoni mwao huko kwa mda wa miaka saba, kushinda kabisa katika mshangao.
Then I passed through the air and came into the captivity, and went round [to] them that lived by the river of Chobar who were there; and I sat there seven days, conversant in the midst of them.
16 Kisha ikatokea baada ya siku saba kwamba neno la Yahwe likanijia, likisema,
And after the seven days the word of the Lord came to me, saying, Son of man,
17 “Mwana wa adamu, nimekufanya uwe mwangalizi kwa ajili ya nyumba ya Israeli, hivyo sikiliza neno kutoka kinywani mwangu, na uwapatie onyo langu.
I have made you a watchman to the house of Israel; and you shall hear a word of my mouth, and shall threaten them from me.
18 Nitakaposema kwa waovu, 'Utakufa hakika' na usimuonye au kuzungumza onyo kwa waovu kuhusu matendo yao maovu hivyo anaweza kuishi-yule muovu atakufa kwa ajili ya dhambi yake, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako.
When I say to the wicked, You shall surely die; and you have not warned him, to give warning to the wicked, to turn from his ways, that he should live; that wicked man shall die in his iniquity; but his blood will I require at your hand.
19 Lakini kama ukimuonya muovo, na asiuache uovu wake au kutoka matendo yake maovu, kisha atakufa kwa dhambi yake, lakini utaokoa maisha yako mwenyewe.
But if you warn the wicked, and he turn not from his wickedness, and from his way, that wicked man shall die in his iniquity, and you shall deliver your soul.
20 Kama mwenye haki ataicha haki yake na kutenda yasiyohaki, na nikaweka kizuizi mbele yake, atakufa. Kwasababu hukumuonya, atakufa katika dhambi yake, na sintokumbuka matendo ya haki aliyoyafanya, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako.
And when the righteous turns away from his righteousness, and commits a trespass, and I shall bring punishment before him, he shall die, because you did not warn him: he shall even die in his sins, because his righteousness shall not be remembered; but his blood will I require at your hand.
21 Lakini kama ukimuonya mwenye mtu mwenye haki kuacha kufanya dhambi halafu akaacha kutenda dhambi, ataishi hakika tangu alipo unywa; na utakuwa umeokoa maisha yako mwenyewe.”
But if you warn the righteous not to sin, and he sin not, the righteous shall surely live, because you have warned him; and you shall deliver your own soul.
22 Hivyo mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu huko, akanambia, “Inuka! nenda uwandani, na nitaongea na wewe huko!”
And the hand of the Lord came upon me; and he said to me, Arise, and go forth into the plain, and there shall you be spoken to.
23 Nikainuka na kwenda uwandani, na huko utukufu wa Yahwe ulisimama, kama utukufu ambao niliokuwa nimeuona karibu na Kebari Kanali; hivyo nikaanguka kifudifudi.
And I arose, and went forth to the plain: and, behold, the glory of the Lord stood there, according to the vision, and according to the glory of the Lord, which I saw by the river of Chobar: and I fell on my face.
24 Roho akaja kwangu na kusimama juu ya miguu yangu; akaongea na mimi, na kunambia, “Nenda na jifungie mwenyewe kwenye nyumba yako,
Then the Spirit came upon me, and set me on my feet, and spoke to me, and said to me, Go in, and shut yourself up in the midst of your house.
25 kwa sasa, mwana wa adamu, wataweka kamba juu yako na kukufunga ili usiweze kutoka nje miongoni mwao.
And you, son of man, behold, bonds are prepared for you, and they shall bind you with them, and you shall not come forth of the midst of them.
26 Nitaufanya ulimi wako ugandamane na paa ya mdomo wako, ili kwamba uwe kimya, na hutaweza kuwakemea, kwa kuwa ni nyumba ya waasi.
Also I will bind your tongue, and you shall be dumb, and shall not be to them a reprover: because it is a provoking house.
27 Lakini nitakapozungumza na wewe, nitafungua mdomo wako hivyo utawaambia, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.' Yeye asikiaye na asikie; yeye asiyesikia na asisikie, kwa kuwa wao ni nyumba ya kuasi!”
But when I speak to you, I will open your mouth, and you shall say to them, Thus says the Lord, He that hears, let him hear; and he that is disobedient, let him be disobedient: because it is a provoking house.

< Ezekieli 3 >