< Ezekieli 25 >

1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
And there is a word of Jehovah unto me, saying,
2 “Mwanadamu, weka uso wako juu ya watu wa Amoni na tabiri juu yao.
'Son of man, set thy face unto the sons of Ammon, and prophesy against them;
3 Waambie watu wa Amoni, 'Sikiliza neno la Bwana Yahwe. Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Kwa sababu umesema, “Aha!” juu ya patakatifu pangu wakati palipotiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli wakati ilipokuwa ukiwa, na juu ya nyumba ya Yuda wakati walipoenda utumwani,
and thou hast said to the sons of Ammon: Hear ye a word of the Lord Jehovah: Thus said the Lord Jehovah: Because of thy saying, Aha, to My sanctuary, Because it hath been polluted, And unto the ground of Israel, Because it hath been desolate, And unto the house of Judah, Because they have gone into a removal:
4 kwa hiyo, tazama, nitakupatia kwa watu katika mashariki kama milki yao. Watafanya kambi juu yako na kuweka mahema miongoni mwako. Watakula matunda yako na watakunywa maziwa yako.
Therefore, lo, I am giving thee to sons of the east for a possession, And they set their towers in thee, And have placed in thee their tabernacles. They eat thy fruit, and they drink thy milk,
5 Nitamfanya Raba malisho ya ngamia na watu wa Amoni shamba la mifugo. Kisha utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
And I have given Rabbah for a habitation of camels, And the sons of Ammon for the crouching of a flock, And ye have known that I [am] Jehovah.
6 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Umepigia makofi mikono yako na kupiga chapa miguu yako, na kufurahi pamoja na dharau ndani yako dhidi ya nchi ya Israeli.
For thus said the Lord Jehovah: Because of thy clapping the hand, And of thy stamping with the foot, And thou rejoicest with all thy despite in soul Against the ground of Israel,
7 Kwa hiyo, tazama! Nitanyoosha mkono wangu na kukupatia kama mateka kwa mataifa. Nitakukatilia mbali kutoka watu na kukuangamiza kutoka miongoni mwa nchi! Nitakuharibu, na utajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
Therefore, lo, I — I have stretched out My hand against thee, And have given thee for a portion to nations, And I have cut thee off from the peoples, And caused thee to perish from the lands; I destroy thee, and thou hast known that I [am] Jehovah.
8 Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu Moabu na Seiri husema “Tazama! Nyumba ya Yuda ni kama kila taifa jingine.”
Thus said the Lord Jehovah: Because of the saying of Moab and Seir: Lo, as all the nations [is] the house of Judah;
9 Kwa hiyo, tazama! ntafungua miteremko ya Moabu, kuanzia kwenye miji yake juu ya mpaka-uzuri wa Beth Yeshimothi, Baal Meoni, na Kiriathaimu-
Therefore, lo, I am opening the shoulder of Moab — From the cities — from his cities — from his frontier, The beauty of the land, Beth-Jeshimoth, Baal-Meon, and Kiriathaim,
10 kwa watu wa mashariki waliokuwa juu ya watu wa Amoni. Nitawapatia kama milki ili kwamba watu wa Amoni hawatakumbukwa miongoni mwa mataifa.
To the sons of the east, with the sons of Ammon, And I have given it for a possession, So that the sons of Ammon are not remembered among nations.
11 Hivyo nitafanya hukumu juu ya Moabu, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
And in Moab I do judgments, And they have known that I [am] Jehovah.
12 Bwana Yahwe asema hivi, Edomu amelipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda na amefanya makosa katika kufanya hivyo.
Thus said the Lord Jehovah: Because of the doings of Edom, In taking vengeance on the house of Judah, Yea, they are very guilty, And they have taken vengeance on them.
13 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Nitaunyoosha mkono wangu juu ya Edomu na kumharibu kila mtu na wanyama huko. Nitawaharibu, sehemu ya ukiwa, kutoka Temani hata Dedani. Wataanguka kwa upanga.
Therefore, thus said the Lord Jehovah: I have stretched out My hand against Edom, And I have cut off from it man and beast, And given it up — a waste, from Teman even to Dedan, By sword they do fall.
14 Nitaweka kisasi changu juu ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Israeli, na watafanya kwa Edomu kulingana na hasira yangu na ghadhabu yangu, na wakitajua kisasi changu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
And I have given My vengeance on Edom, By the hand of My people Israel, And they have done in Edom, According to My anger, and according to My fury, And they have known My vengeance, An affirmation of the Lord Jehovah.
15 Bwana Yahwe asema hivi, 'Wafilisti wamelipiza kisasi pamoja na uovu na kutoka ndani yao wamejaribu kuiharibu Yuda tena na tena.
Thus said the Lord Jehovah: Because of the doings of the Philistines in vengeance, And they take vengeance with despite in soul, To destroy — the enmity age-during!
16 Basi hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazam! Nitanyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti, na nitakalia mbali Wakerethi na kuwaharibu mabaki yaliyobaki karibu na pwani.
Therefore, thus said the Lord Jehovah: Lo, I am stretching out My hand against the Philistines, And I have cut off the Cherethim, And destroyed the remnant of the haven of the sea,
17 Kwa kuwa nitalipiza kisasi kikubwa dhidi yao pamoja na matendo ya ghadhabu kubwa ya adhabu, hivyo watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapolipiza kisasi juu yao.”'
And done upon them great vengeance with furious reproofs, And they have known that I [am] Jehovah, In My giving out My vengeance on them!

< Ezekieli 25 >