< Ezekieli 25 >

1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
And the word of the Lord came to me, saying,
2 “Mwanadamu, weka uso wako juu ya watu wa Amoni na tabiri juu yao.
Son of man, set your face steadfastly against the children of Ammon, and prophesy against them;
3 Waambie watu wa Amoni, 'Sikiliza neno la Bwana Yahwe. Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Kwa sababu umesema, “Aha!” juu ya patakatifu pangu wakati palipotiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli wakati ilipokuwa ukiwa, na juu ya nyumba ya Yuda wakati walipoenda utumwani,
and you shall say to the children of Ammon, Hear you the word of the Lord; thus says the Lord; Forasmuch as you have rejoiced against my sanctuary, because it was profaned; and against the land of Israel, because it was laid waste; and against the house of Juda, because they went into captivity;
4 kwa hiyo, tazama, nitakupatia kwa watu katika mashariki kama milki yao. Watafanya kambi juu yako na kuweka mahema miongoni mwako. Watakula matunda yako na watakunywa maziwa yako.
therefore, behold, I [will] deliver you to the children of Kedem for an inheritance, and they shall lodge in you with their stuff, and they shall pitch their tents in you: they shall eat your fruits, and they shall drink your milk.
5 Nitamfanya Raba malisho ya ngamia na watu wa Amoni shamba la mifugo. Kisha utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
And I will give up the city of Ammon for camels' pastures, and the children of Ammon for a pasture of sheep: and you shall know that I am the Lord.
6 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Umepigia makofi mikono yako na kupiga chapa miguu yako, na kufurahi pamoja na dharau ndani yako dhidi ya nchi ya Israeli.
For thus says the Lord; Because you have clapped your hands, and stamped with your foot, and heartily rejoiced against the land of Israel;
7 Kwa hiyo, tazama! Nitanyoosha mkono wangu na kukupatia kama mateka kwa mataifa. Nitakukatilia mbali kutoka watu na kukuangamiza kutoka miongoni mwa nchi! Nitakuharibu, na utajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
therefore I will stretch out my hand against you, and I will make you a spoil to the nations; and I will utterly destroy you from amongst the peoples, and I will completely cut you off from out of the countries: and you shall know that I am the Lord.
8 Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu Moabu na Seiri husema “Tazama! Nyumba ya Yuda ni kama kila taifa jingine.”
Thus says the Lord; Because Moab has said, Behold, are not the house of Israel and Juda like all the [other] nations?
9 Kwa hiyo, tazama! ntafungua miteremko ya Moabu, kuanzia kwenye miji yake juu ya mpaka-uzuri wa Beth Yeshimothi, Baal Meoni, na Kiriathaimu-
Therefore, behold, I will weaken the shoulder of Moab from his frontier cities, [even] the choice land, the house of Bethasimuth above the fountain of the city, by the sea-side.
10 kwa watu wa mashariki waliokuwa juu ya watu wa Amoni. Nitawapatia kama milki ili kwamba watu wa Amoni hawatakumbukwa miongoni mwa mataifa.
I have given him the children of Kedem in addition to the children of Ammon for an inheritance, that there may be no remembrance of the children of Ammon.
11 Hivyo nitafanya hukumu juu ya Moabu, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
And I will execute vengeance on Moab; and they shall know that I am the Lord.
12 Bwana Yahwe asema hivi, Edomu amelipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda na amefanya makosa katika kufanya hivyo.
Thus says the Lord; Because of what the Idumeans have done in taking vengeance on the house of Juda, and [because they] have remembered injuries, and have exacted full recompense;
13 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Nitaunyoosha mkono wangu juu ya Edomu na kumharibu kila mtu na wanyama huko. Nitawaharibu, sehemu ya ukiwa, kutoka Temani hata Dedani. Wataanguka kwa upanga.
therefore thus says the Lord; I will also stretch out my hand upon Idumea, and will utterly destroy out of it man and beast; and will make it desolate; and they that are pursued out of Thaeman shall fall by the sword.
14 Nitaweka kisasi changu juu ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Israeli, na watafanya kwa Edomu kulingana na hasira yangu na ghadhabu yangu, na wakitajua kisasi changu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
And I will execute my vengeance on Idumea by the hand of my people Israel: and they shall deal in Idumea according to mine anger and according to my wrath, and they shall know my vengeance, says the Lord.
15 Bwana Yahwe asema hivi, 'Wafilisti wamelipiza kisasi pamoja na uovu na kutoka ndani yao wamejaribu kuiharibu Yuda tena na tena.
Therefore thus says the Lord, Because the Philistines have wrought revengefully, and raised up vengeance rejoicing from their heart to destroy [the Israelites] to a man;
16 Basi hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazam! Nitanyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti, na nitakalia mbali Wakerethi na kuwaharibu mabaki yaliyobaki karibu na pwani.
therefore thus says the Lord; Behold, I [will] stretch out my hand upon the Philistines, and will utterly destroy the Cretans, and will cut off the remnant that dwell by the sea-coast.
17 Kwa kuwa nitalipiza kisasi kikubwa dhidi yao pamoja na matendo ya ghadhabu kubwa ya adhabu, hivyo watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapolipiza kisasi juu yao.”'
And I will execute great vengeance upon them; and they shall know that I am the Lord, when I have brought my vengeance upon them.

< Ezekieli 25 >