< Ezekieli 18 >

1 Neno la Yahwe likanijia tena, kusema,
Пак дойде към мене Господното слово и рече:
2 “Je mnamaana gani, ninyi mliotumia hii mithali kuhusiana na nchi ya Israeli na kusema, 'Wababa wamekula zabibu mbichi, na meno ya watoto imetiwa ganzi'?
Що искате да кажете вие, които употребявате тая поговорка относно Израилевата земя, като казвате: Бащите ядоха кисело грозде, а на чадата оскоминяха зъбите?
3 Kama nishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-bila shaka hakutakuwa na fursa yoyote tena kwa ajili yenu kuitumia hii mithali katika Israeli.
Заклевам се в живота Си, казва Господ Иеова, няма вече да има повод да употребите тая поговорка в Израил.
4 Tazama! Kila uhai ni mali yangu-uhai wa baba na uhai wa mwana pia, ni mali yangu! roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa!
Ето, всичките души са Мои; както душата на бащата, така и душата на сина е Моя; душата, която е съгрешила, тя ще умре.
5 Itasemwaje kuhusu mtu mwenye haki na achukuaye yaliyo halali na haki-
Но ако е някой праведен и постъпва законно и право,
6 kama asipokula juu ya milima au kuinua macho yake kwa sananmu za nyumba ya Israeli, na hakumnajisi mke wa jirani yake, wala kumsemesha mwanamke katika kipindi chake cha mwezi, je! Yu mwenye haki?
ако не яде по планините, нито подига очите си към идолите на Израилевия дом, не осквернява жената на ближния си, нито се приближава до жена, кога е в нечистотата си,
7 Je! Itasemwaje kuhusu mtu ambaye hakumkandamiza yeyote, na kumrudisha mdeni wake kwa kile kilichokuwa kimewekwa kwa ajili ya rehani, na hakuiba lakini kuwapatia chakula wenye njaa na kuwafunika uchi kwa nguo, je yu mwenye haki?
ако не насилва човека, но връща на длъжника залога му, не граби с насилие, но дава хляба си на гладния и покрива с дрехи голия,
8 Je! Itasemwaje kuhusu mtu ambaye hakuchukua faida kubwa kwa ile pesa aliyokopa, na hakuchukua faida kubwa kwa kile alichokiuza?
ако не дава с лихва и не взема придобивка, оттегля ръката си от неправда, върши правосъдие между човека и човека,
9 Amesemwa kwamba amechukua yaliyo halali na kuimarisha uaminifu kati ya watu. Kama huyo mtu akitembea katika sheria zangu na kuzishika hukumu zangu kufanya kwa uaminifu, kisha ahadi kwa ajili ya mtu mwenye haki ni hii: Ataishi hakika! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
ходи в повеленията Ми, и пази съдбите Ми, за да постъпва вярно; такъв човек е праведен, непременно той ще живее, казва Господ Иеова.
10 Lakini akizaa mwana mnyang'anyi mmwaga damu na kufanya mengi katika haya mambo kama yalivyotajwa hapa,
Ако той роди син разбойник, който пролива кръв и върши коя да било от тия работи,
11 hata kama baba yake hakufanya mojawapo katika haya mambo, lakini akala juu ya milima na akamnajisi mke wa jirani yake, Je! itasemwaje juu yake?
и който, освен че не изпълнява ни една от тия длъжности, но и яде по планините и осквернява жената на ближния си,
12 Huyu mtu huwakandamiza maskini na wahitaji, na huwakamata na kuwanyang'anya, na hawarudishii dhamana, na huyanua macho yake kwa sanamu na kufanya matendo maovu,
насилва сиромаха и немощния, граби с насилие, не връща залога, подига очите си към идолите и прави мерзости,
13 na hukopesha pesa kwa faida ya juu sana na kufanya faida kubwa juu ya anachokiuza, Je! huyo mtu ataishi? Hakika hataishi! Atakufa hakika na damu yake itakuwa juu yake kwa sababu amefanya haya mambo ya chuki.
дава с лихва и взема придобивка; такъв човек ще живее ли? Няма да живее. Като е сторил всички тия мерзости, непременно ще умре; кръвта му ще бъде върху него.
14 Lakini Tazama! tuseme kuna mtu aliyezaa mwana, na mwana wake huona dhambi zote za baba yake alizozifanya, na kupitia kuziona, hakuyafanya hayo mambo.
Но ако тоя роди син, който като гледа всичките грехове, които баща му е сторил, бои се и не върши такива работи,
15 Huyo mwana hakula juu ya milima, na hakuinua macho yake kwa sanamu za nyumba ya Israeli, na hakumtia unajisi mke wa jirani yake, Je! itasemwaje juu yake?
не яде по планините, нито подига очите си към идолите на Израилевия дом, не осквернява жената на ближния си,
16 Yule mwana hakumkandamiza yeyote, au kutwaa dhamana, au kupoteza vitu, lakini badala yake kutoa chakula chake kwa wenye njaa na kuwafunika wenye uchi kwa nguo.
не насилва човека нито задържа залог, не граби с насилие, но дава хляба си на гладния и покрива с дреха голия,
17 Huyo mwana hakumkandamiza yeyote au au kuchukua faida ambayo ni ya juu sana au kufanya manufaa kwa ajili ya mkopo, lakini ameyashika maagizo yangu na kuenenda sawa sawa na sheria zangu; huyo mwana hatakufa kwa ajili ya dhambi za baba yake: Ataishi hakika!
не угнетява сиромаха, не взема лихва и придобивка, извършва съдбите Ми, и ходи в повеленията Ми; такъв човек няма да умре за беззаконието на баща си; непременно ще живее.
18 Baba yake, kwa kuwa aliwakandamiza wengine kwa nguvu nyingi na kumnyang'anya ndugu yake, na kufanya yasiyo mema miongoni mwa watu wake-tazama, atakufa katika uovu wake.
Баща му, понеже жестоко е угнетявал, грабил от брата си с насилие, и правил между людете си това, което не е добро, ето, той ще умре за беззаконието си.
19 Lakini ninyi husema, 'Kwa nini mwana asibebe uovu wa baba yake?' Kwa sababu mwana hubeba yaliyo halali na haki na kuzitunza amri zangu; huzifanya. Ataishi hakika!
Но вие казвате: Защо не понася синът наказанието на бащиното си беззаконие? Когато синът е постъпвал законно и право, пазил всичките Ми повеления, и ги е извършвал, той непременно ще живее.
20 Yule atendaye dhambi, ndiye ambaye atakufa. Mwana hatabeba uovu wa baba yake, na baba hatabeba uovu wa mwana wake. Haki ya yule atendaye haki itakuwa juu yakwe mwenyewe, na uovu wa mwenye uovu utakuwa juu yake mwenyewe.
Душата, която греши, тя ще умре; синът няма да понесе наказанието на бащиното беззаконие, нито ще понесе бащата наказанието на синовото беззаконие; правдата на праведния ще бъде за него, и беззаконието на беззаконника ще бъде за него.
21 Lakini kama mwovu ageukapo kutoka dhambi zake zote alizofanya, na kuzitunza sheria zangu zote na kufanya yaliyo halali na haki, kisha hakika ataishi na hatakufa.
Но ако беззаконникът се обърне от всичките грехове, които е сторил, пази всичките Ми повеления, и постъпва законно и право, непременно той ще живее, няма да умре.
22 Makosa yote aliyoyafanya hayatakumbukwa juu yake. Ataishi kwa hiyo haki aliyoitenda.
Никое от престъпленията, които е извършил, няма да се помни против него; чрез правдата, която е сторил, ще живее.
23 Je! Nitafurahia juu ya kifo cha mwovu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na sio katika kugeuka kwake kutoka njia yake ili kwamba aweze kuishi?
Благоволя ли Аз в смъртта на нечестивия? казва Господ Иеова, а не по-добре да се обърне от пътя си и да живее?
24 Lakini kama mtu mwenye haki ageukapo kutoka kwenye haki yake na kufanya maovu na kutenda machukizo kama machukizo yote ambayo mtu mwovu afanyayo, basi ataishi? Haki yake yote aliyoifanya haitakumbukwa wakati atakaponisaliti katika uhaini wake. Hivyo atakufa katika dhambi alizofanya.
Когато обаче праведният се отвърне от правдата си и стори неправда, като извърши всичките мерзости, които нечестивият върши, тогава ще живее ли? Ни едно от праведните дела, които е сторил, няма да се помни; за престъплението, което е извършил, и за греха, който е сторил, за тях ще умре.
25 Lakini ninyi husema, 'Njia ya Bwana si sawa!' sikilizeni, nyumba ya Israeli! Je njia zangu haziko sawa? Je si njia ambazo haziko sawa?
Но вие казвате: Господният път не е прав. Слушайте сега, доме Израилев: Моят ли път не е прав? Не са ли криви вашите пътища?
26 Wakati mtu mwenye haki ageukapo kutoka kwenye makosa yake, na kufanya maovu na kufa kwa sababu ya hayo, kisha atakufa katika uovu ambao alioufanya.
Когато се отвърне праведният от правдата си и извърши неправдата, ще умре за нея; поради неправдата, която е извършил, той ще умре.
27 Lakini wakati mtu mwovu ageukapo kutoka uovu wake alioufanya na kufanya yaliyo halali na haki, kisha ataulinda uhai wake.
А пък когато нечестивият се обърне от нечестието, което е извършил и постъпи законно и право, той ще опази жива душата си.
28 Kwa kuwa ameona na kugeuka kutokana na makosa yake yote ambayo aliyoyafanya. Hakika ataishi, na hatakufa.
Понеже се е смилил и се е обърнал от всичките престъпления, които е сторил, непременно ще живее, няма да умре.
29 Lakini nyumba ya Israeli husema, 'Njia ya Bwana haiko sawa!' Ni namna gani njia zangu si sawa, nyumba ya Israeli? Ni njia zenu ndizo si sawa.
Но Израилевият дом казва: Господният път не е прав. Доме Израилев, Моите ли пътища не са прави? Не са ли криви вашите пътища?
30 Kwa hiyo nitamuhukumu kila mtu miongoni mwenu kulingana na njia zake, nyumba ya Israeli! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo. Tubuni na rudini kutoka kwenye makosa yenu yote ili kwamba wasiwe kikwazo cha uovu dhidi yenu.
Затова, доме Израилев, Аз ще ви съдя, всеки според постъпките му, казва Господ Иеова. Покайте се, и обърнете се от всичките си престъпления, та да ви не погуби беззаконието.
31 Tupilia mbali makosa yenu yote mliyoyafanya; jifanyieni moyo mpya na roho mpya. Kwa nini mfe, nyumba ya Israeli?
Отхвърлете от себе си всичките престъпления, с които беззаконствувахте, и направете си ново сърце и нов дух; защо да умрете, доме Израилев?
32 Kwa kuwa sifurahii kifo cha yule afaye-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-hivyo tubuni na muishi!”
Понеже Аз не благоволя в смъртта на оня, който умира, казва Господ Иеова; затова, върнете се и живейте.

< Ezekieli 18 >