< Ezekieli 13 >

1 Tena, neno la Yahwe likanijia, kusema,
and to be word LORD to(wards) me to/for to say
2 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wanaotabiri katika Israeli, na uwaambie wale wanotabiri nje ya fikra zao wenyewe, 'Lisikilizeni neno la Yahwe.
son: child man to prophesy to(wards) prophet Israel [the] to prophesy and to say to/for prophet from heart their to hear: hear word LORD
3 Bwana Yahwe asema hivi: Ole wao manbii wajinga ambao wafwatao roho zao wenyewe, lakini wale wasioona kitu!
thus to say Lord YHWH/God woe! upon [the] prophet [the] foolish which to go: follow after spirit their and to/for lest to see: see
4 Israeli, manabii zako wamekuwa kama mbeha kwenye aridhi iliyoharibiwa na vita.
like/as fox in/on/with desolation prophet your Israel to be
5 Hamkwenda kwenye nyufa katika ukuta uliozunguka nyumba ya Israeli kwa ajili ya kuukarabati, ili kupigana katika vita katika siku ya Yahwe.
not to ascend: rise in/on/with breach and to wall up/off wall upon house: household Israel to/for to stand: stand in/on/with battle in/on/with day LORD
6 Watu wameona uongo na kufanya utabiri wa uongo, wale wasemao, “Hivi na hivi ndvyo Yahwe asemavyo.” Yahwe hajawatuma, lakini hata hivyo wamewafanya watu kutumaini kwamba ujumbe wao utakuwa kweli.
to see vanity: false and divination lie [the] to say utterance LORD and LORD not to send: depart them and to wait: hope to/for to arise: establish word
7 Je hamkusikia maono ya uongo na kufanya utabiri wa uongo, ninyi msemao, “Hivi na hivi ndivyo Yahwe asemavyo” Wakati mimi mwenyewe sikuongea?'
not vision vanity: false to see and divination lie to say and to say utterance LORD and I not to speak: speak
8 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu mmesikia maono ya uongo na kuwaambia uongo-kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo dhidi yenu:
to/for so thus to say Lord YHWH/God because to speak: speak you vanity: false and to see lie to/for so look! I to(wards) you utterance Lord YHWH/God
9 Mkono wangu utakuwa juu yenu ninyi manabii mliodanganya maono na wale waliofanya unabii wa uongo. Hawatakuwepo kwenye kusanyiko la watu wangu, au kuandikishwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli; hawataenda kwenye nchi ya Israeli. Kwa kuwa mtajua yakwamba mimi ni Bwana Yahwe!
and to be hand: power my to(wards) [the] prophet [the] to see vanity: false and [the] to divine lie in/on/with counsel people my not to be and in/on/with writing house: household Israel not to write and to(wards) land: soil Israel not to come (in): come and to know for I Lord YHWH/God
10 Kwa sababu hiyo, na kwa sababu wamewaongoza watu wangu kuwapotosha na kusema, “Amani!” wakati hakuna amani, wanajenga ukuta ambao wataupaka rangi ya chokaa.'
because and in/on/with because to stray [obj] people my to/for to say peace and nothing peace and he/she/it to build wall and behold they to overspread [obj] him whitewash
11 Waambie wale wanaopaka chokaa ukuta, 'Utaanguka chini; kutakuwa na mvua ya kufurika, na nitaleta mvua ya mawe kuufanya uanguke chini, na upepo wa dhoruba kupuliza hata kuuvunja chini.
to say to(wards) to overspread whitewash and to fall: fall to be rain to overflow and you(f. p.) stone hail to fall: fall and spirit: breath tempest to break up/open
12 Tazama, ukuta utaanguka chini. Je wengine hawakuwaambia, “Iko wapi chokaa mliyoipaka juu yake?”
and behold to fall: fall [the] wall not to say to(wards) you where? [the] coating which to overspread
13 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Nitaleta upepo wa dhoruba katika ghadhabu yangu, na kutakuwa na mafuriko ya mvua kwenye ghadhabu yangu! Mvua ya mawe katika ghadhabu yangu itauharibu kabisa.
to/for so thus to say Lord YHWH/God and to break up/open spirit: breath tempest in/on/with rage my and rain to overflow in/on/with face: anger my to be and stone hail in/on/with rage to/for consumption
14 Kwa kuwa nitaurarua chini ukuta ambao mlioufunika kwa chokaa, na nitaubomoa hata kwenye nchi na kuifunua misingi yake. Hivyo utaanguka, nanyi nyote mtaangamizwa katikati ya huo.
and to overthrow [obj] [the] wall which to overspread whitewash and to touch him to(wards) [the] land: soil and to reveal: uncover foundation his and to fall: fall and to end: destroy in/on/with midst her and to know for I LORD
15 Ndivyo nitakavouangamiza kwa ghadhabu yangu ukuta na wale walioupaka chokaa. Nitawaambia, “Ukuta hautaonekana tena, wala watu wanaoupaka chokaa-
and to end: expend [obj] rage my in/on/with wall and in/on/with to overspread [obj] him whitewash and to say to/for you nothing [the] wall and nothing [the] to overspread [obj] him
16 manabii wa Israeli wale waliotabiri kuhusu Yerusalemu na wale waliokuwa wameona amani kwa ajili yake. Lakini hakuna amani! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
prophet Israel [the] to prophesy to(wards) Jerusalem and [the] to see to/for her vision peace and nothing peace utterance Lord YHWH/God
17 Hivyo wewe, mwanadamu, weka uso wako dhidi ya binti za watu wako wale wanaotabiri kwa akili zao wenyewe, na kutabiri dhidi yao.
and you(m. s.) son: child man to set: make face your to(wards) daughter people your [the] to prophesy from heart their and to prophesy upon them
18 Sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Ole kwa wanawake washonao hiziri kwenye kila sehemu ya mkono wao na kutengeza vitambaa vya shela kwa ajili ya vichwa vyao kwa kila kipimo, ili kuwinda watu. Je mtawawinda watu wangu ila kuokoa maisha yenu wenyewe?
and to say thus to say Lord YHWH/God woe! to/for to sew amulet upon all joint hand: themselves my and to make [the] veil upon head all height to/for to hunt soul soul to hunt to/for people my and soul to/for you to live
19 Ninyi mmenikufuru mbele ya watu wangu kwa ajili ya makonzi ya shayiri na vipande vya mkate, kuwaua watu ambao hawakutakiwa kufa, na kuyalinda maisha ya wale ambao hawatakiwi kuendelea kuishi, kwa sababu ya uongo wenu kwa watu wangu walio wasikiliza.
and to profane/begin: profane [obj] me to(wards) people my in/on/with handful barley and in/on/with morsel food: bread to/for to die soul which not to die and to/for to live soul which not to live in/on/with to lie you to/for people my to hear: hear lie
20 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Niko kinyume dhidi ya hirizi ambazo mlizozitumia kuyakamata kwa hila maisha ya watu kana kwamba wamekuwa ndege. Naam, nitazichana kutoka kwenye mikono yenu; na wale watu mlio watega kama ndege-nitawaacha waende huru.
to/for so thus to say Lord YHWH/God look! I to(wards) amulet your which you(f. p.) to hunt there [obj] [the] soul to/for to fly and to tear [obj] them from upon arm your and to send: let go [obj] [the] soul which you(m. p.) to hunt [obj] soul to/for to fly
21 Nitavichana mbali vitambaa vya shela na kuwaokoa watu wangu kutoka kwenye mikono yangu, kwa hiyo hawatategwa tena kwenye mikono yenu. Mtajua kwamba mimi ni Yahwe.
and to tear [obj] veil your and to rescue [obj] people my from hand: power your and not to be still in/on/with hand: power your to/for net and to know for I LORD
22 Kwa sababu mmeuvunja moyo wa mtu mwenye haki kwa uongo, ingawa hata mimi sikutamani kuvunjwa kwake moyo, na kwa sababu mmemtia moyo badala yake matendo ya mtu mwovu ili kwamba asitaweze kurudi kutoka kwenye njia yake kuokoa maisha yake-
because be disheartened heart righteous deception and I not to pain him and to/for to strengthen: strengthen hand: themselves wicked to/for lest to return: repent from way: conduct his [the] bad: evil to/for to live him
23 kwa hiyo hamtayaona tena maono ya uongo au kuendelea kufanya utabiri, kwa kuwa nitawaokoa watu wangu kutoka kwenye mkono wako. Nanyi mtajua kwamba mimi ni Yahwe.'”
to/for so vanity: false not to see and divination not to divine still and to rescue [obj] people my from hand: power your and to know for I LORD

< Ezekieli 13 >