< Ezekieli 11 >

1 Kisha Roho akaniacha juu na kunileta kwenye lango la mashariki la nyumba ya Yahwe, kuelekea mashariki, na tazama, kwenye njia ya mlango wa lango kulikuwa na watu ishirini na tano. Nikamwona Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu, miongoni mwao.
I podniósł mię duch, a przywiódł mię do bramy domu Pańskiego wschodniej, która patrzy na wschód słońca; a oto w wejściu onej bramy było dwadzieścia i pięć mężów, między którymi widziałem Jazanijasza, syna Assurowego, i Pelatyjasza, syna Banaja szowego, książąt ludu;
2 Mungu akanambia, “Mwana wa adamu, hawa ndio wale watu walioshauri udhalimu, na kuamua mipango miovu kwenye huu mji.
Tedy mi rzekł: Synu człowieczy! onić to są mężowie, którzy zamyślają o nieprawości, a radzą złą radę w tem mieście,
3 Wakisema, 'Mda wa kujenga nyumba sio sasa; huu mji ni sufuria, na sisi ni nyama.'
Mówiąc: Nie budujmy domów blisko; boby tak miasto było kotłem, a my mięsem.
4 Kwa hiyo tabiri juu yao. Tabiri, mwana wa adamu.”'
Dlatego prorokuj przeciwko nim, prorokuj, synu człowieczy!
5 Kisha Roho wa Yahwe akanijaza na akaniambia, “akisema: Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: kama usemavyo, nyumba ya Israeli; kwa kuwa najua kinachoendelea kwenye fikra zenu.
Tedy przypadł na mię duch Pański, i rzekł do mnie: Mów: Tak mówi Pan: Takeście mówili, domie Izraelski! bo co wam kolwiek przychodzi na myśl, to Ja znam;
6 Mmewazidisha watu mliowaua kwenye huu mji na kuijaza mitaa kwa hao.
Wielkieście mnóstwo pobili w tem mieście, a napełniliście ulice jego pobitymi.
7 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Wale watu milowaua, ambao mmeilaza miili yao kati ya Yerusalemu, ni nyama, na huu mji ni sufuria. Lakini mnaenda kutolewa nje kutoka kati ya huu mji.
Dlatego tak mówi panujący Pan: Którzy są pobici od was, którycheście składali w pośrodku jego, oni są mięsem, a miasto kotłem; ale was wywiodą z pośrodku jego.
8 Mmeuogopa upanga, kwa hiyo nauleta huo upanga juu yenu-huu ndio usemi wa Bwana Yahwe.
Baliście się miecza; ale miecz przywiodę na was, mówi panujący Pan.
9 Nitawatoa nje kutoka kati ya mji, na kuwaweka kwenye mikono ya wageni, kwa kuwa nitaleta hukumu dhidi yenu.
A wywiodę was z pośrodku jego, a podam was w ręce obcych, i wykonam nad wami sądy.
10 Mtaanguka kwa upanga. Nitawahukumu kati ya mipaka ya Israeli hivyo mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
Od miecza polężecie, na granicach Izraelskich osądzę was, i dowiecie się, żem Ja Pan.
11 Huu mji hautakua sufuria yenu ya kupikia, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitawahukumu kati ya mipaka ya Israeli.
Miasto nie będzie wam kotłem, ani wy będziecie w pośród jego mięsem; na granicach Izraelskich osądzę was,
12 Kisha mtajua yakwamba mimi ni Yahwe, yule ambaye hamuishe kwenye amri zake na ambaye hamkuzishika sheria zake. Badala yake, mmebeba hukumu za mataifa wanayowazunguka.”
I dowiecie się, żem Ja Pan; ponieważeście w ustawach moich nie chodzili, a sądów moich nie czynili, aleście według sądów tych narodów, którzy około was są, czynili.
13 Ikawa kwamba nilipokuwa natabiri, Pelatia mwana wa Benaya, akafa. Hivyo nikaanguka kwenye uso wangu na kulia kwa sauti na kusema, “Ee, Bwana Yahwe, Je utayaharibu kabisa mabaki ya Israeli?”
A gdym prorokował, tedy Pelatyjasz, syn Banajaszowy, umarł: dlatego upadłem na twarz moję, a wołając głosem wielkim, rzekłem: Ach, panujący Panie! do gruntu wygładzisz ostatki Izraelskie.
14 Neno la Yahwe likanijia, likisema,
I stało się słowo Pańskie do mnie, mówiąc:
15 “Mwana wa adamu, ndugu zako! Ndugu zako! Watu wa ukoo wako na nyumba yote ya Israeli! Wote hao ndio hao ambao inasemekana wale wanaoishi Yerusalemu, 'Wako mbali sana kutoka kwa Yahwe! Hii nchi tulipewa sisi kama milki yetu.'
Synu człowieczy! bracia twoi, bracia twoi, powinowaci twoi, i wszystek dom Izraelski, wszystek mówię dom, cić są, którym mówili obywatele Jeruzalemscy: Oddalcie się od Pana; namci dana jest ta ziemia w osiadłość.
16 Kwa hiyo sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: kote nimewapitisha mbali kati ya mataifa, na kote nimewasambaza kati ya nchi, bado nimekuwa patakatifu kwa ajili yao kwa mda kidogo kwenye nchi ambazo walizoenda.'
Przetoż mów: Tak mówi panujący Pan: Chociażem ich daleko zagnał między narody, i chociażem ich rozproszył po ziemiach, wszakże będę im świątnicą i przez ten mały czas w ziemiach, do których przyjdą.
17 Kwa hiyo sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Nitawakusanya kutoka kwa watu, na kuwakutanisha kutoka kwenye nchi mlizokuwa mmetawanyika, na nitawapatia nchi ya Israeli.'
Przetoż mów: Tak mówi panujący Pan: Zgromadzę was z narodów, a zbiorę was z ziem, do którycheście rozproszeni, i dam wam ziemię Izraelską.
18 Kisha wataenda huko na kuondoa kila kitu chenye karaha na kila chukizo kutoka hiyo sehemu.
I wnijdą tam, a zniosą wszystkie splugawienia jej, i wszystkie jej obrzydliwości z niej.
19 Nitawapatia moyo mmoja, na nitaweka roho mpya kati yao. Nitaondoa moyo wa jiwe kutoka kwenye miili wao na kuwapatia moyo wa nyama,
Bo im dam serce jedno, i ducha nowego dam do wnętrzności waszych, i odejmę sece kamienne z ciała ich, a dam im serce mięsiste,
20 ili kwamba waweze kutembea kwenye amri zangu, watayachukua maagizo yangu na kuyatenda. Kisha watakuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wao.
Aby w ustawach moich chodzili, a sądów moich strzegli, i czynili je; i będą ludem moim, a Ja będę Bogiem ich.
21 Lakini kwa wale watembeao kwa kujifanya kuendeleza mambo yao ya karaha na machukizo yao, nitaleta tabia yao kwenye vichwa vyao-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
Ale którychby serce chodziło za żądzami plugastw swoich, i obrzydliwości swoich, tych drogę obrócę na głowy ich, mówi panujący Pan.
22 Makerubi wakainua mabawa yao na magurudumu yaliyokuwa karibu nao, na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
Tedy podnieśli Cherubinowie skrzydła swoje, i koła z nimi, a chwała Boga Izraelskiego była nad nimi z wierzchu.
23 Kisha utukufu wa Yahwe ukaenda juu kutoka katikati ya mji na kusimama kwenye mlima hata mashariki mwa mji.
I odeszła chwała Pańska z pośrodku miasta, a stanęła na górze, która jest na wschód miasta.
24 Roho akanichukua juu na kunileta hata Ukaldayo, hata uhamishoni, katika maono kutoka kwa Roho wa Mungu, na maono niliyokuwa nimeyaona yakaenda juu yakaniacha.
A duch podniósł mię, i zaś mię przywiódł do ziemi Chaldejskiej do pojmanych, w widzeniu w Duchu Bożym. I odeszło odemnie widzenie, którem widział.
25 Kisha nikawaambia wale watumwa mambo yote ya Yahwe niliyokuwa nimeyaona.
I mówiłem do pojmanych te wszystkie rzeczy Pańskie, które mi ukazał.

< Ezekieli 11 >