< Ezekieli 1 >

1 Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, na siku ya tano ya mwezi, ikawa kuhusu kwamba nilikuwa nikiishi miongoni mwa wafungwa karibu na Kebari Kanali. Mbingu zilifunguka, na kuona maono ya Mungu.
And it came to pass in the thirtieth year, in the fourth month on the fifth day of the month I being in the midst of them of the captivity, by the river Chebar, that the heavens were opened, and I saw visions of God.
2 Katika siku ya tano katika mwezi huo-ilikuwa mwaka wa tano wa utumwani wa Mfalme Yehoyakini-
On the fifth of the month, that was the fifth year of the captivity of King Jehoiachin,
3 Neno la Yahwe likamjia Ezekieli mwana wa Buzi kuhani, katika nchi ya Wakaldayo karibu na Keberi Kanali, na mkono wa Yahwe ulikuwa juu yake hapo.
in very deed came the word of Yahweh unto Ezekiel son of Buzi the priest in the land of the Chaldeans by the river Chebar, —yea the hand of Yahweh, came on him there.
4 Kisha nikaona, kulikuwa na upepo wa dhoruba unakuja kutoka kaskazini; wingu kubwa pamoja na moto wa nuru ndani yake na kung'aa ukizunguka ndani yake, na moto ulikuwa na rangi ya kaharabu ndani ya hilo wingu.
So then I beheld and lo! a tempestuous wind coming out of the North, a great cloud and a fire catching hold of itself, and it had a brightness round about, —and out of the midst thereof, as burnished copper to look upon out of the midst of the fire;
5 Katikati kulikuwa na viumbe vinne vinavyofanana. Mwonekano wao ulikuwa hivi: walikuwa wanamfanano wa mtu,
and out of the midst thereof, a likeness of four living ones, and this was their appearance, the likeness of a man, had they;
6 lakini walikuwa na sura nne kila mmoja, na kila mmoja alikuwa na mabawa manne.
and four faces each, and four wings each, had they;
7 Miguu yao ilikuwa imenyooka, lakini nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za ndama zilizokuwa zinang'aa kama shaba iliyosuguliwa.
and their feet were straight feet, —and the sole of their feet was like the sole of the foot of a calf, but sparkling, as shining bronze to look upon;
8 Bado walikuwa na mikono ya binadamu chini ya mabawa yao chini kwenye pande zote nne. Kwa wote wanne, nyuso zao na mabawa vilikuwa hivi:
and the hands of a man! were under their wings, on their four sides, —and their faces and their wings belonged to the four of them:
9 mabawa yao yalikuwa yameungana na kiumbe kingine, na hawakurudi walipokuwa wameenda; badala yake, kila mmoja alienda mbele.
joined to each other, were their wings, —they turned not when they went, each one straight before him, did they go;
10 Mfanano wa nyuso zao ulikuwa kama uso wa mwanadamu. Wanne hao walikuwa na uso wa simba kwa upande wa kuume. Hao wanne pia walikuwa na uso wa tai.
and the likeness of their faces was the face of a man, with the face of a lion to the right of the four of them, and the face of an ox on the left, of the four of them, —the face of an eagle, also had they four;
11 Nyuso zao zilikuwa hivyo, na mabawa yao yalikuwa yametawanyika juu, hivyo basi kila kiumbe kilikuwa na jozi ya za mabawa yaliyokuwa yameshikamana na bawa la kiumbe kingine, na pia jozi za mabawa yaliyokuwa yamefunika miili yao.
and their wings were spread above, — two of each joined one another, and two covered their bodies;
12 Kila mmoja alienda mbele, hivyo basi popote Roho alipowaelekeza kwanda, walienda bila kurudi.
and each one straight before him, did they go, —whithersoever the spirit was minded to go, they went, they turned not when they went.
13 Kama kwa mfanano wa hao viumbe hai, mwonekano wao ulikuwa ni kama kuchoma kaa la moto, kama mwonekano wa nuru; mng'ao wa moto pia ulihama karibu na miongoni mwa viumbe, na kulikuwa na nuru za radi.
As for the likeness of the living ones, their appearance was like live coals of fire burning up like the appearance of torches, the same went to and fro between the living ones, —and the fire had brightness and out of the fire, went forth a lightning.
14 Hao viumbe hai vilikuwa vikihama mbio mbele na nyuma, na walikuwa na mwonekano wa radi!
And the living ones ran and returned, —like the appearance of a flash of lightning.
15 Kisha nikawatazama wale viumbe hai; kulikuwa na gurudumu moja juu ya aridhi kando ya vile viumbe hai.
And I looked at the living ones, —and lo! one wheel upon the earth beside the living ones for each of his four faces,
16 Huu ndio ulikuwa mwonekano na umbo wa hizo gurudumu: kila gurudumu lilikuwa kama zabarajadi, na manne hayo yalikuwa na mfano mmoja; mwonekano wao na umbo vilikuwa kama gurudumu lililoungana na jingine.
The appearance of the wheels and of their structure was like a Tarshish-stone to look upon, and they four had one likeness, —and their appearance and their structure were just as would be a wheel in the midst of a wheel.
17 Wakati yale magurudumu yalipokuwa yakitembea, yalienda bila kurudi kwenye mwelekeo wowote viumbe vilipokuwa vimeelekea.
Upon their four sides, when they went, so did they go, —they turned not when they went.
18 Kama kwa upande kingo, walikuwa warefu na wakutisha, kwa upande kingo kulikuwa na macho yamezunguka kote.
As for their rings, they were so high that they were terrible, -and their rings full of eyes round about, had they four.
19 Popote vile viumbe hai vilipokuwa vikielekea, yale magurudumu yalielekea karibu nao. Wakati vile viumbe hai vilipoinuka kutoka kwenye nchi, na yale magurudumu yaliinuka pia.
And when the living ones went, the wheels went beside them, —and when the living ones were lifted up from the earth, the wheels were lifted up:
20 Popote Roho alipokwenda, walikwenda, na yale magurudumu yaliinuka karibu nao, roho wa kiumbe hai ilikuwa magurudumu.
whithersoever the spirit was minded to go, they went—thither was the spirit minded to go, —and the wheels would be lifted up along with them, for the spirit of the living one was in the wheels:
21 Popote vile viumbe vilipoelekea, magurudumu pia yalielekea huko; na wakati wale viumbe viliposimama hata hivyo, magurudumu yalisimama bado; wakati viumbe viliposimama kutoka kwenye nchi, magurudumu yalisimama karibu nao, kwa sababu yule roho wa wale viumbe alikuwa kwenye magurudumu.
when they went, these went, and when they stood, these stood, —and when they were lifted up from off the earth, the wheels were lifted up along with them, for the spirit of the living one was in the wheels.
22 Juu ya vichwa vya wale viumbe hai kulikuwa na mfanano wa anga la kutanuka; ilikuwa inang'aa kama mfano wa barafu juu ya vichwa vyao.
And there was a likeness over the heads of the living one—an expanse, like terrible crystal to look upon, -stretched forth over their heads above.
23 Chini ya anga, kila mabawa ya kiumbe kimoja yalinyooshwa mbele na kugusana kila mabawa na kiumbe kimoja. Pia kila kiumbe hai kilikuwa na jozi moja kwa ajili ya kujifunika vyenyewe; kila kimoja kilikuwa na jozi moja kwa ajili ya kujifunika mwili wake mwenyewe.
And under the expanse, their wings were straight, one towards another, —each one had two covering on this side, and each one had two covering on that side, their bodies.
24 Kisha nikasikia sauti ya mabawa yao. Kama mlio wa maji mengi. Kama sauti ya mwenye enzi popote walipoelekea. Kama sauti ya jeshi. Popote pale waliposimama, walishusha mabawa yao.
And I heard the sound of their wings, as the sound of many waters, as the sound of the Almighty, when they went, the sound of a storm as the sound of a host, —when they stood, they let down their wings,
25 Sauti ikaja kutoka juu ya anga juu ya vichwa vyao popote waliposimama na kushusha mabawa yao.
And there was a voice above the expanse that was over their head, —when they stood, they let down their wings.
26 Juu ya anga juu ya vichwa vyao kulikuwa na mfanao wa kiti cha enzi ambacho kilikuwa na mwonekano wa jiwe la samawati, na juu mfano wa kiti cha enzi kilifanana kama mwonekano wa mwanadamu.
And above the expanse that was over their heads, as the appearance of a sapphire stone, was the likeness of a throne, —and upon the likeness of a throne, was a likeness as the appearance of a man upon it above.
27 Nikaona umbo lenye mwonekano wa chuma chenye kung'aa pamoja na moto ndani yake kutoka kwenye mwonekano wa juu ya nyonga zake juu; Nikaona kutoka kwenye mwonekano wa nyonga zake upande wa chini mwonekano wa moto na mng'ao umezunguka kote.
And I saw as burnished copper to look upon, as the appearance of fire within it round about, from the appearance of his loins and upwards and from the appearance of his loins and downwards, saw I as the appearance of fire, and he had brightness round about:
28 Kama mwonekano wa upinde wa mvua kwenye mawingu katika siku ya mvua ulikuwa na mwonekano wa taa iliyowaka imeizunguka. ulikuwa na mwonekano unaofanana na utukufu wa Yahwe. Wakati nilipouona, nilihisi kwenye uso wangu, na nikasikia sauti ikiongea.
as the appearance of the bow which is in a cloud on a day of rain, so was the appearance of the brightness round about, that was the appearance of the likeness of the glory of Yahweh, and when I saw, I fell upon my face, and heard a voice of one speaking.

< Ezekieli 1 >