< Kutoka 8 >

1 Kisha Yahweh akazungumza na Musa, “Nenda kwa Farao na umwambie, 'Yahweh anasema hivi: Acha watu wangu waende hili wakaniabudu.
And Jehovah saith unto Moses, 'Go in unto Pharaoh: and thou hast said unto him, Thus said Jehovah, Send My people away, and they serve Me;
2 Ukikataa kuwaruhusu waende, nitaidhuru nchi yako yote kwa vyura.
and if thou art refusing to send away, lo, I am smiting all thy border with frogs;
3 Mito itajawa na vyura. Watatoka na kuingia nyumbani kwako, chumbani kwako, na kitandani kwako. Wataenda nyumbani mwa watumishi wako. Wataenda kwa watu wako, kwenye majiko yako, na vyombo vya kukandia mkate.
and the River hath teemed [with] frogs, and they have gone up and gone into thy house, and into the inner-chamber of thy bed, and on thy couch, and into the house of thy servants, and among thy people, and into thine ovens, and into thy kneading-troughs;
4 Vyura watakushambulia wewe, watu wako, na watumishi wako wote."”'
yea, on thee, and on thy people, and on all thy servants do the frogs go up.'
5 Yahweh akamwambia Musa, “Mwambie Aruni, 'Nyoosha mkono wako na gongo lako kwenye mito, mifereji, na kwenye mabwawa, na uwatoe vyura juu ya nchi ya Misri.”'
And Jehovah saith unto Moses, 'Say unto Aaron, Stretch out thy hand, with thy rod, against the streams, against the rivers, and against the ponds, and cause the frogs to come up against the land of Egypt.'
6 Aruni akanyoosha mkono juu ya maji ya Misri, na vyura wakatoka na kujaza nchi ya Misri.
And Aaron stretcheth out his hand against the waters of Egypt, and the frog cometh up, and covereth the land of Egypt;
7 Lakini wachawi walifanya vivyo hivyo na uchawi wao: waliwatoa vyura juu ya nchi ya Misri.
and the scribes do so with their flashings, and cause the frogs to come up against the land of Egypt.
8 Kisha Farao akawaita Musa na Aruni na kuwaambia, “Muombeni Yahweh iliawaondoe vyura kwangu na kwa watu wangu. Kisha nitawaacha watu waende, iliwamtolee dhabihu.”
And Pharaoh calleth for Moses and for Aaron, and saith, 'Make supplication unto Jehovah, that he turn aside the frogs from me, and from my people, and I send the people away, and they sacrifice to Jehovah.'
9 Musa akamwambia Farao, “Unaweza chukuwa fursa ya kuniambia lini nikuombee wewe, watumishi wako, na watu wako, ili vyura waondolewe kwako na nyumbani kwako na wabaki tu kwenye mito.”
And Moses saith to Pharaoh, 'Beautify thyself over me; when do I make supplication for thee, and for thy servants, and for thy people, to cut off the frogs from thee and from thy houses — only in the River they do remain?'
10 Farao akasema, “Kesho.” Musa akasema, “Acha iwe kama ulivyo sema, ili kwamba ujue hakuna Mungu mwengine kama Yahweh, Mungu wetu.
and he saith, 'To-morrow.' And he saith, According to thy word [it is], so that thou knowest that there is none like Jehovah our God,
11 Vyura wataondoka kutoka kwako, nyumbani mwako, kwa watumishi wako, na kwa watu wako. Watabaki tu kwenye mito.”
and the frogs have turned aside from thee, and from thy houses, and from thy servants, and from thy people; only in the River they do remain.'
12 Musa na Aruni wakaondoka kwa Farao. Kisha Musa akamlilia Yahweh kuhusu hao vyura alio waleta kwa Farao.
And Moses — Aaron also — goeth out from Pharaoh, and Moses crieth unto Jehovah, concerning the matter of the frogs which He hath set on Pharaoh;
13 Yahweh akafanya kama Musa alivyo omba: Vyura wakafa kwenye nyumba, nyuani, na mashambani.
and Jehovah doth according to the word of Moses, and the frogs die out of the houses, out of the courts, and out of the fields,
14 Watu wakawakusanya kwa mafungu, na nchi ikanuka.
and they heap them up together, and the land stinketh.
15 Lakini Farao alipoona kuna afadhali, aliufanya moyo wake kuwa mgumu na hakumsikiliza Musa na Aruni, kama Yahweh alivyo sema.
And Pharaoh seeth that there hath been a respite, and he hath hardened his heart, and hath not hearkened unto them, as Jehovah hath spoken.
16 Yahweh akamwambia Musa, “Mwambie Aruni, 'Nyoosha gongo lako na upige udongo chini, iliuwe chawa kati nchi yote ya Misri.”'
And Jehovah saith unto Moses, 'Say unto Aaron, Stretch out thy rod, and smite the dust of the land, and it hath become gnats in all the land of Egypt.'
17 Wakanya hivyo: Aruni akanyoosha mkono wake na gongo lake. Akaupiga udongo wa ardhi. Chawa wakaja juu ya watu na wanyama. Udongo wote kwenye ardhi ukawa chawa katika nchi ya Misri.
And they do so, and Aaron stretcheth out his hand with his rod, and smiteth the dust of the land, and the gnats are on man and on beast; all the dust of the land hath been gnats in all the land of Egypt.
18 Wachawi walijaribu kufanya chawa kwa uganga wao lakini hawakuweza. Palikuwa na chawa kwa watu na kwa wanyama.
And the scribes do so with their flashings, to bring out the gnats, and they have not been able, and the gnats are on man and on beast;
19 Kisha wachawi wakamwambia Farao, “Hichi ni kidole cha Mungu.” Lakini moyo wa Farao ulikuwa Mgumu, hivyo akakataa kuwasikiliza. Ilikuwa kama Yahweh alivyo sema Farao atafanya.
and the scribes say unto Pharaoh, 'It [is] the finger of God;' and the heart of Pharaoh is strong, and he hath not hearkened unto them, as Jehovah hath spoken.
20 Yahweh akamwambia Musa, “Inuka asubui mapema na usimame mbele ya Farao anapoenda mtoni. Umwambie, 'Yahweh anasema hivi: “Acha watu wangu waende wakaniabudu mimi.
And Jehovah saith unto Moses, 'Rise early in the morning, and station thyself before Pharaoh, lo, he is going out to the waters, and thou hast said unto him, Thus said Jehovah, Send My people away, and they serve Me;
21 Lakini usipo acha watu wangu waende nitatuma kundi la nzi kwako, watumishi wako, na watu wako, na kwenye nyumba zenu. Nyumba za wa Misri zitajawa na makundi ya nzi, na ata ardhi wanayo simama itajawa na nzi.
for, if thou art not sending My people away, lo, I am sending against thee, and against thy servants, and against thy people, and against thy houses, the beetle, and the houses of the Egyptians have been full of the beetle, and also the ground on which they are.
22 Lakini katika siku hiyo nitaitendea nchi ya Gosheni tofauti, nchi ambayo watu wangu wanaishi, ilikwamba kusiwe na makundi ya nzi huko. Hili litatokea ili kwamba mjue mimi ni Yahweh katika hii nchi.
'And I have separated in that day the land of Goshen, in which My people are staying, that the beetle is not there, so that thou knowest that I [am] Jehovah in the midst of the land,
23 Nitaweka utofauti kati ya watu wangu na watu wako. Hii ishara ya nguvu zangu itatokea kesho"”'
and I have put a division between My people and thy people: to-morrow is this sign.'
24 Yahweh akafanya hivyo, na kundi kubwa la nzi likaja nyumbani mwa Farao na nyumbani mwa watumishi wake. Katika nchi yote ya Misri, nchi iliharibiwa na makundi ya nzi.
And Jehovah doth so, and the grievous beetle entereth the house of Pharaoh, and the house of his servants, and in all the land of Egypt the land is corrupted from the presence of the beetle.
25 Farao akawaita Musa na Aruni na kuwaambia, “Nendeni, mtolee Mungu wenu dhabihu kwenye nchi yetu.”
And Pharaoh calleth unto Moses and to Aaron, and saith, 'Go, sacrifice to your God in the land;'
26 Musa akasema, “Sio vyema sisi kufanya hivyo, kwa kuwa dhabihu tunazo mtolea Yahweh Mungu wetu zinachukiza kwa Wamisri. Kama tutatoa dhabihu mbele ya macho yao zilizo chukizo kwa Wamisri, hawata tupiga mawe?
and Moses saith, 'Not right to do so, for the abomination of the Egyptians we do sacrifice to Jehovah our God; lo, we sacrifice the abomination of the Egyptians before their eyes — and they do not stone us!
27 Hapana, ni safari ya siku tatu kwenda nyikani ambayo lazima tuende, ili kiutoa dhabihu kwa Yahweh Mungu wetu, kama anavyo tuamuru.”
A journey of three days we go into the wilderness, and have sacrificed to Jehovah our God, as He saith unto us.'
28 Farao akasema, “Nitakuruhusu kwenda kumtolea dhabihu Yahweh Mungu wenu nyikani. Ila usiende mbali sana. Niombee.”
And Pharaoh saith, 'I send you away, and ye have sacrificed to Jehovah your God in the wilderness, only go not very far off; make ye supplication for me;'
29 Musa akasema, “Wakati tu nitakapoenda kutoka kwako, nitamuomba Yahweh ili makundi ya nzi yatoke kwako, wewe Farao, na watumishi wako na watu kesho. Lakini usifanye udhalimu tena kwa kutowaacha watu wetu waende kumtolea dhabihu Yahweh.”
and Moses saith, 'Lo, I am going out from thee, and have made supplication unto Jehovah, and the beetle hath turned aside from Pharaoh, from his servants, and from his people — to-morrow, only let not Pharaoh add to deceive — in not sending the people away to sacrifice to Jehovah.'
30 Musa akaenda nje kutoka kwa Farao na kumuomba Yahweh.
And Moses goeth out from Pharaoh, and maketh supplication unto Jehovah,
31 Yahweh akafanya kama Musa alivyo muomba: alitoa makundi ya nzi kutoka kwa Farao, watumishi wake, na watu wake. Hakuna ata mmoja aliye baki.
and Jehovah doth according to the word of Moses, and turneth aside the beetle from Pharaoh, from his servants, and from his people — there hath not been left one;
32 Lakini Farao aliufanya moyo wake mgumu tena, na hakuwaacha watu waende.
and Pharaoh hardeneth his heart also at this time, and hath not sent the people away.

< Kutoka 8 >