< Kutoka 40 >

1 Kisha Yahweh akasema na Musa na kumwambia,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
2 “Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka lazima wewe uandae hema la kukutania.
On [the] day of the month first on [day] one of the month you will set up [the] tabernacle of [the] tent of meeting.
3 Utaweka sanduku la ushuhuda ndani yake, na utaziba sanduku kwa pazia.
And you will put there [the] ark of the testimony and you will cover over the ark the curtain.
4 Utaleta ndani meza na kuandaa kwa mpangilio vitu vyake. Kisha utaleta kinara cha taa na kuandaa taa.
And you will bring the table and you will arrange arrangement its and you will bring the lampstand and you will lift up lamps its.
5 Nawe utaweka madhabahu ya dhahabu ya uvumba mbele ya sanduku la ushuhuda, na utaweka pazia katika mwingilio wa hema la kukutania.
And you will put [the] altar of gold for incense before [the] ark of the testimony and you will put [the] screen of the entrance of the tabernacle.
6 Utaweka madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa mbele ya mwingilio wa hema ya kukutania.
And you will put [the] altar of the burnt offering before [the] entrance of [the] tabernacle of [the] tent of meeting.
7 Utaweka ile saani kubwa katikati ya hema la kukutania na madhabahu na utaweka maji ndani yake.
And you will put the laver between [the] tent of meeting and between the altar and you will put there water.
8 Uandae nyuani inayoizunguka, na utundike pazia katika mwingilio wa nyuani.
And you will put the courtyard all around and you will put [the] screen of [the] gate of the courtyard.
9 Lazima uchukuwe mafuta ya upako na upake hema la kukutania na kila kitu kilichopo ndani yake. Lazima uitenge na samani zake kwangu; kisha itakuwa takatifu.
And you will take [the] oil of anointing and you will anoint the tabernacle and all that [is] in it and you will consecrate it and all articles its and it will be a holy thing.
10 Lazima upake mafuta madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake. Lazima utenge madhabhu kwa ajili yangu na itakuwa takatifu kwangu.
And you will anoint [the] altar of the burnt offering and all articles its and you will consecrate the altar and it will be the altar holiness of holiness.
11 Upake mafuta beseni la shaba na sakafu yake na uitenge kwa ajili yangu.
And you will anoint the laver and base its and you will consecrate it.
12 Umlete Aruni na wanae kwa mwingilio wa hema la kukutania na uwaoshe wote kwa maji.
And you will bring near Aaron and sons his to [the] entrance of [the] tent of meeting and you will wash them with water.
13 Utamfunika Aruni kwa mavazi yaliyo tengwa kwa ajili yangu, mpake mafuta na umtenge ili anitumikie kama kuhani.
And you will clothe Aaron [the] garments of holiness and you will anoint him and you will consecrate him and he will serve as a priest me.
14 Utawaleta wana wake na kuwafunika kwa nguo nzito.
And sons his you will bring near and you will clothe them tunics.
15 Utawapaka mafuta kama ulivyo mpaka baba yao ili wanitumikie kama makuhani. Upako wao utawafanya makuhani wa kudumu vizazi vyote vya watu wao.”
And you will anoint them just as you anointed father their and they will serve as priests me and it will become to be for them anointing their a priesthood of perpetuity to generations their.
16 Hivi ndivyo Musa alivyo sema; alifuata yote Yahweh aliyo muamuru. Alifanya vitu vyote hivi.
And he did Moses according to all that he had commanded Yahweh him so he did.
17 Hivyo hema la kukutania liliandaliwa siku ya kwanza ya mwezi wa mwaka wa pili.
And it was in the month first in the year second on [day] one of the month it was set up the tabernacle.
18 Musa alianda hema la kukutania, akaeka sakafu zake sehemu yake, akaanda fremu zake, akashikisha chuma zake, na akaanda minara na nguzo zake.
And he set up Moses the tabernacle and he put bases its and he set up frames its and he put bars its and he set up pillars its.
19 Alitandaza mfuniko juu ya hema la kukutania na kuweka hema juu yake, kama Yahweh alivyo muamuru.
And he spread out the tent over the tabernacle and he put [the] covering of the tent over it from to above just as he had commanded Yahweh Moses.
20 Alichukuwa amri za agano na kuweka kwenye sanduku. Pia aliweka nguzo kwenye sanduku na kuweka mfuniko wa kiti cha rehema.
And he took and he put the testimony into the ark and he put the poles on the ark and he put the atonement cover on the ark from to above.
21 Aliichukuwa sanduku na kuweka ndani ya hema la kukutania. Aliandaa pazia ili lizibe sanduku la ushuhuda, kama Yahweh alivyo muamuru.
And he brought the ark into the tabernacle and he set up [the] curtain of the screen and he covered over [the] ark of the testimony just as he had commanded Yahweh Moses.
22 Alieka meza kwenye hema la kukutania, kwa upande wa kaskazini mwa hema la kukutania, nje ya pazia.
And he put the table in [the] tent of meeting on [the] side of the tabernacle north-ward from [the] outside of the curtain.
23 Alieka mkate kwa mpangilio katika meza ya Yahweh, kama Yahweh alivyo amuru.
And he arranged on it an arrangement of bread before Yahweh just as he had commanded Yahweh Moses.
24 Alieka kinara cha taa kwenye hema la kukutania, upande wa pili wa meza, kusini mwa hema la kukutani.
And he put the lampstand in [the] tent of meeting opposite to the table on [the] side of the tabernacle south-ward.
25 Aliwasha taa mbele za Yahweh, kama Yahweh alivyo muamuru.
And he lifted up the lamps before Yahweh just as he had commanded Yahweh Moses.
26 Aliweka madhabahu ya dhahabu ya uvumba ndani ya hema la kukutania mbele ya pazia.
And he put [the] altar of gold in [the] tent of meeting before the curtain.
27 Alichoma uvumba wa manukato hapo, kama Yahweh alivyo muamuru.
And he made smoke on it incense of perfume just as he had commanded Yahweh Moses.
28 Alitundika pazia katika hema ya kukutania.
And he set up [the] screen of the entrance of the tabernacle.
29 Aliweka madhabahu ya sadaka ya kuteketeza katika hema ya kukutania. Aliitolea sadaka ya kuteketeza na sadaka ya unga, kama Yahweh alivyo muamuru.
And [the] altar of the burnt offering he set up [the] entrance of [the] tabernacle of [the] tent of meeting and he offered up on it the burnt offering and the grain offering just as he had commanded Yahweh Moses.
30 Aliweka beseni katikati ya hema ya kukutunia na madhabahu, na maji ya kuoshea.
And he put the laver between [the] tent of meeting and between the altar and he put there water for washing.
31 Musa, Aruni, na wanae waliosha mikono yao na miguu kwenye beseni
And they washed from it Moses and Aaron and sons his hands their and feet their.
32 muda wowote walipoenda kwenye hema ya kukutania na muda wowote walipoenda kwenye madhabahu. Walijisafisha, kama Yahweh alivyo muamuru Musa.
When went they into [the] tent of meeting and when drew near they to the altar they washed just as he had commanded Yahweh Moses.
33 Musa alianda nyuani nyuma ya hema ya kukutania na madhabahu. Alianda pazia katika mwingilio wa nyuani. Katika hili, Musa alimaliza kazi.
And he set up the courtyard around the tabernacle and the altar and he put [the] screen of [the] gate of the courtyard and he finished Moses the work.
34 Kisha wingu likafunika hema ya kukutania, na utukufu wa Yahweh ukafunika hema ya kukutania.
And it covered the cloud [the] tent of meeting and [the] glory of Yahweh it filled the tabernacle.
35 Musa hakuweza kuingia hema ya kukutania kwasababu wingu lilikuwa juu yake, na kwasababu utukufu wa Yahweh ulijaza hema ya kukutania.
And not he was able Moses to go into [the] tent of meeting for it had settled down over it the cloud and [the] glory of Yahweh it had filled the tabernacle.
36 Muda wowote wingu lilipo chukuliwa juu kutoka hema ya kukutania, watu wa Israeli waliendelea na safari yao.
And when was taken up the cloud from over the tabernacle they set out [the] people of Israel in all journeyings their.
37 Lakini kama wingu haliku nyanyuka juu kutoka hema ya kukutania, kisha basi watu hawaku safiri. Walibaki hadi siku lilipo nyanyuliwa juu.
And if not it was taken up the cloud and not they set out until [the] day was taken up it.
38 Kwa kuwa wingu la Yahweh lilikuwa juu ya hema ya kukutania mchana, na moto wake ulikuwa juu yake usiku, wazi kwa watu wote wa Israeli kipindi chote cha safari yao.
For [the] cloud of Yahweh [was] over the tabernacle by day and fire it was night on it to [the] eyes of all [the] house of Israel in all journeyings their.

< Kutoka 40 >